< Ayubu 30 >

1 “Lakini sasa watu wadogo kwa umri kuniliko wananidhihaki, watu ambao baba zao ningekataa kwa dharau kuwaweka pamoja na mbwa wangu wa kulinda kondoo.
Porém agora se riem de mim os de menos edade do que eu, cujos paes eu teria desdenhado de pôr com os cães do meu rebanho.
2 Nguvu za mikono yao zingekuwa na faida gani kwangu, kwa kuwa nguvu zao zilikuwa zimewaishia?
De que tambem me serviria a força das suas mãos? já de velhice se tinham esgotado n'elles.
3 Wakiwa wamekonda kutokana na kupungukiwa na kwa njaa, walizurura usiku katika nchi kame iliyo ukiwa.
De mingua e fome andavam sós, e recolhiam-se para os logares seccos, tenebrosos, assolados e desertos.
4 Katika vichaka walikusanya mimea ya chumvi, nacho chakula chao kilikuwa mizizi ya mti wa mfagio.
Apanhavam malvas junto aos arbustos, e o seu mantimento eram as raizes dos zimbros.
5 Walifukuzwa mbali na watu wao, wakipigiwa kelele kama wevi.
Do meio dos homens foram expulsos, e gritavam contra elles, como contra o ladrão:
6 Walilazimika kuishi katika mikondo ya vijito vilivyokauka, kwenye majabali na mahandaki.
Para habitarem nos barrancos dos valles, e nas cavernas da terra e das rochas.
7 Kwenye vichaka walilia kama punda, na walijisongasonga pamoja kwenye vichaka.
Bramavam entre os arbustos, e ajuntavam-se debaixo das ortigas.
8 Wao ni watoto wa wapumbavu wenye asili ya ubaya, waliofukuzwa watoke katika nchi.
Eram filhos de doidos, e filhos de gente sem nome, e da terra foram expulsos.
9 “Nao sasa wana wao wananidhihaki katika nyimbo; nimekuwa kitu cha dhihaka kwao.
Porém agora sou a sua canção, e lhes sirvo de rifão.
10 Wananichukia sana na kujitenga nami, wala hawasiti kunitemea mate usoni.
Abominam-me, e fogem para longe de mim, e do meu rosto não reteem o seu escarro.
11 Sasa kwa kuwa Mungu ameilegeza kamba ya upinde wangu na kunitesa, wamekuwa huru kunitendea waonavyo.
Porque Deus desatou o meu cordão, e me opprimiu, pelo que sacudiram de si o freio perante o meu rosto.
12 Kuume kwangu kundi linashambulia; wao huitegea miguu yangu tanzi, na kunizingira.
Á direita se levantam os moços; empurram os meus pés, e preparam contra mim os seus caminhos de destruição.
13 Huizuia njia yangu, nao hufanikiwa katika kuniletea maafa, nami sina yeyote wa kunisaidia.
Desbarataram-me o meu caminho: promovem a minha miseria: não teem ajudador.
14 Wananijia kama watu wapitao katika ufa mpana; katikati ya magofu huja na kunishambulia.
Veem contra mim como por uma grande brecha, e revolvem-se entre a assolação.
15 Vitisho vimenifunika; heshima yangu imetoweshwa kama kwa upepo, salama yangu imetoweka kama wingu.
Sobrevieram-me pavores; como vento perseguem a minha honra, e como nuvem passou a minha felicidade.
16 “Sasa maisha yangu yamefikia mwisho; siku za mateso zimenikamata.
E agora derrama-se em mim a minha alma: os dias da afflicção se apoderaram de mim.
17 Usiku mifupa yangu inachoma; maumivu yanayonitafuna hayatulii kamwe.
De noite se me traspassam os meus ossos, e os pulsos das minhas veias não descançam.
18 Kwa uwezo wake mkuu Mungu huwa kwangu kama nguo; hushikamana nami kama ukosi wa vazi langu.
Pela grandeza da força das dôres se demudou o meu vestido, e elle como o cabeção da minha tunica me cinge.
19 Yeye amenitupa kwenye matope, nami nimekuwa kama mavumbi na majivu.
Lançou-me na lama, e fiquei similhante ao pó e á cinza.
20 “Ee Bwana, ninakulilia wewe lakini hunijibu; ninasimama, nawe unanitazama tu.
Clamo a ti, porém tu não me respondes: estou em pé, porém para mim não attentas.
21 Wewe unanigeukia bila huruma; unanishambulia kwa nguvu za mkono wako.
Tornaste-te a ser cruel contra mim: com a força da tua mão resistes violentamente.
22 Unaninyakua na kunipeperusha kwa upepo; umenirusha huku na huko kwenye dhoruba kali.
Levantas-me sobre o vento, fazes-me cavalgar sobre elle, e derretes-me o ser.
23 Ninajua utanileta mpaka kifoni, mahali ambapo wenye uhai wote wamewekewa.
Porque eu sei que me levarás á morte e á casa do ajuntamento determinado a todos os viventes.
24 “Hakika hakuna yeyote amshambuliaye mhitaji, anapoomba msaada katika shida yake.
Porém não estenderá a mão para o montão de terra, se houve clamor n'elles contra mim na sua desventura.
25 Je, sikulia kwa ajili ya wale waliokuwa katika taabu? Je, nafsi yangu haikusononeka kwa ajili ya maskini?
Porventura, não chorei sobre aquelle que estava afflicto? ou não se angustiou a minha alma pelo necessitado?
26 Lakini nilipotazamia mema, mabaya yalinijia; nilipotafuta nuru, ndipo giza lilipokuja.
Todavia aguardando eu o bem, então me veiu o mal, e esperando eu a luz, veiu a escuridão.
27 Kusukwasukwa ndani yangu kamwe hakutulii; siku za mateso zinanikabili.
As minhas entranhas ferveram e não estão quietas: os dias da afflicção me surprehenderam.
28 Ninazunguka nikiwa nimeungua, lakini si kwa jua; ninasimama katika kusanyiko nikiomba msaada.
Denegrido ando, porém não do sol, e, levantando-me na congregação, clamo por soccorro.
29 Nimekuwa ndugu wa mbweha, rafiki wa mabundi.
Irmão me fiz dos dragões, e companheiro dos abestruzes.
30 Ngozi yangu imekuwa nyeusi nayo inachunika; mifupa yangu inaungua kwa homa.
Ennegreceu-se a minha pelle sobre mim, e os meus ossos estão queimados do calor.
31 Kinubi changu kimegeuka kuwa maombolezo, nayo filimbi yangu imekuwa sauti ya kilio.
Pelo que se trocou a minha harmonia em lamentação, e o meu orgão em voz dos que choram.

< Ayubu 30 >