< Ayubu 30 >
1 “Lakini sasa watu wadogo kwa umri kuniliko wananidhihaki, watu ambao baba zao ningekataa kwa dharau kuwaweka pamoja na mbwa wangu wa kulinda kondoo.
Et maintenant j’excite les moqueries de gens plus jeunes que moi, dont les pères m’inspiraient trop de mépris pour les mettre avec les chiens de mon troupeau.
2 Nguvu za mikono yao zingekuwa na faida gani kwangu, kwa kuwa nguvu zao zilikuwa zimewaishia?
Aussi bien, à quoi m’eût servi le concours de leurs mains? Pour eux il n’y a point de maturité.
3 Wakiwa wamekonda kutokana na kupungukiwa na kwa njaa, walizurura usiku katika nchi kame iliyo ukiwa.
Epuisés par les privations et la faim, ils rôdent dans le désert, lugubre région de désolation et d’horreur,
4 Katika vichaka walikusanya mimea ya chumvi, nacho chakula chao kilikuwa mizizi ya mti wa mfagio.
cueillant des plantes sauvages près des arbrisseaux, se nourrissant de la racine des genêts.
5 Walifukuzwa mbali na watu wao, wakipigiwa kelele kama wevi.
On les chasse du milieu des hommes et on les poursuit de cris comme des voleurs.
6 Walilazimika kuishi katika mikondo ya vijito vilivyokauka, kwenye majabali na mahandaki.
Ils sont contraints d’habiter dans d’effrayants ravins, dans les excavations du sol et les crevasses des rochers.
7 Kwenye vichaka walilia kama punda, na walijisongasonga pamoja kwenye vichaka.
Ils grognent au milieu des buissons et s’entassent sous les broussailles;
8 Wao ni watoto wa wapumbavu wenye asili ya ubaya, waliofukuzwa watoke katika nchi.
troupe méprisable, gens sans aveu, ils se voient expulsés du pays!
9 “Nao sasa wana wao wananidhihaki katika nyimbo; nimekuwa kitu cha dhihaka kwao.
Et à présent, ils me chansonnent; je suis pour eux un thème à railleries.
10 Wananichukia sana na kujitenga nami, wala hawasiti kunitemea mate usoni.
Ils me témoignent leur dégoût, ils s’écartent de moi et ne se privent pas de me cracher à la figure.
11 Sasa kwa kuwa Mungu ameilegeza kamba ya upinde wangu na kunitesa, wamekuwa huru kunitendea waonavyo.
C’Est que Dieu a brisé les rênes que je tenais en mains, et il m’a humilié; ces gens ont secoué le frein que je leur imposais.
12 Kuume kwangu kundi linashambulia; wao huitegea miguu yangu tanzi, na kunizingira.
A ma droite se lève une jeunesse insolente, qui fait glisser mes pas et se fraie vers moi ses routes de malheur.
13 Huizuia njia yangu, nao hufanikiwa katika kuniletea maafa, nami sina yeyote wa kunisaidia.
Ils défoncent mon chemin, coopèrent à ma ruine, sans avoir besoin d’assistance.
14 Wananijia kama watu wapitao katika ufa mpana; katikati ya magofu huja na kunishambulia.
Ils montent à' l’assaut comme par une large brèche, ils se précipitent au milieu du fracas.
15 Vitisho vimenifunika; heshima yangu imetoweshwa kama kwa upepo, salama yangu imetoweka kama wingu.
Des terreurs me poursuivent, chassant comme le vent mon honneur; ma prospérité a passé comme un nuage.
16 “Sasa maisha yangu yamefikia mwisho; siku za mateso zimenikamata.
Et maintenant mon âme se fond en moi, les jours de misère m’ont enserré.
17 Usiku mifupa yangu inachoma; maumivu yanayonitafuna hayatulii kamwe.
La nuit ronge les os de mon corps, mes nerfs ne jouissent d’aucun repos.
18 Kwa uwezo wake mkuu Mungu huwa kwangu kama nguo; hushikamana nami kama ukosi wa vazi langu.
Par l’extrême violence du choc mon vêtement se déforme: elle m’étreint comme l’encolure d’une tunique.
19 Yeye amenitupa kwenye matope, nami nimekuwa kama mavumbi na majivu.
Dieu m’a plongé dans la fange, et j’ai l’air d’être poussière et cendre.
20 “Ee Bwana, ninakulilia wewe lakini hunijibu; ninasimama, nawe unanitazama tu.
Je crie vers toi, et tu ne me réponds pas; je me tiens là, et tu me regardes fixement.
21 Wewe unanigeukia bila huruma; unanishambulia kwa nguvu za mkono wako.
Tu es devenu inexorable pour moi, tu me combats avec toute la force de ta main.
22 Unaninyakua na kunipeperusha kwa upepo; umenirusha huku na huko kwenye dhoruba kali.
Tu m’enlèves sur les ailes du vent, tu m’y fais chevaucher, et tu me fais fondre dans la tempête.
23 Ninajua utanileta mpaka kifoni, mahali ambapo wenye uhai wote wamewekewa.
Car je sais bien que tu me mènes à la mort, au rendez-vous de tous les vivants.
24 “Hakika hakuna yeyote amshambuliaye mhitaji, anapoomba msaada katika shida yake.
Mais est-ce qu’on n’étend pas la main quand on s’effondre? Ne crie-t-on pas au secours lorsqu’on succombe au malheur?
25 Je, sikulia kwa ajili ya wale waliokuwa katika taabu? Je, nafsi yangu haikusononeka kwa ajili ya maskini?
Moi-même n’ai-je pas pleuré sur les victimes du sort? Mon cœur ne s’est-il point serré à la vue du malheureux?
26 Lakini nilipotazamia mema, mabaya yalinijia; nilipotafuta nuru, ndipo giza lilipokuja.
J’Espérais le bien, et le mal a fondu sur moi; j’attendais la lumière, les ténèbres sont venues.
27 Kusukwasukwa ndani yangu kamwe hakutulii; siku za mateso zinanikabili.
Mes entrailles bouillonnent sans relâche, les jours de misère m’ont assailli.
28 Ninazunguka nikiwa nimeungua, lakini si kwa jua; ninasimama katika kusanyiko nikiomba msaada.
Je marche tout noirci et non par le fait du soleil. Je me lève dans l’assemblée et pousse des cris.
29 Nimekuwa ndugu wa mbweha, rafiki wa mabundi.
Je suis devenu le frère des chacals, le compagnon des autruches.
30 Ngozi yangu imekuwa nyeusi nayo inachunika; mifupa yangu inaungua kwa homa.
Ma peau, toute noircie, se détache de moi, et mes os sont brûlés par le feu de la fièvre.
31 Kinubi changu kimegeuka kuwa maombolezo, nayo filimbi yangu imekuwa sauti ya kilio.
Et ainsi ma harpe s’est changée en instrument de deuil, et ma flûte émet des sanglots.