< Ayubu 30 >

1 “Lakini sasa watu wadogo kwa umri kuniliko wananidhihaki, watu ambao baba zao ningekataa kwa dharau kuwaweka pamoja na mbwa wangu wa kulinda kondoo.
Et maintenant, je suis la risée d'hommes plus jeunes que moi, dont je n'aurais pas daigné mettre les pères parmi les chiens de mon troupeau.
2 Nguvu za mikono yao zingekuwa na faida gani kwangu, kwa kuwa nguvu zao zilikuwa zimewaishia?
Qu'aurais-je fait de la force de leurs bras? Ils sont privés de toute vigueur.
3 Wakiwa wamekonda kutokana na kupungukiwa na kwa njaa, walizurura usiku katika nchi kame iliyo ukiwa.
Desséchés par la misère et la faim, ils broutent le désert, un sol depuis longtemps aride et désolé.
4 Katika vichaka walikusanya mimea ya chumvi, nacho chakula chao kilikuwa mizizi ya mti wa mfagio.
Ils cueillent sur les buissons des bourgeons amers, ils n'ont pour pain que la racine des genêts.
5 Walifukuzwa mbali na watu wao, wakipigiwa kelele kama wevi.
On les écarte de la société des hommes, on crie après eux comme après le voleur.
6 Walilazimika kuishi katika mikondo ya vijito vilivyokauka, kwenye majabali na mahandaki.
Ils habitent dans d'affreuses vallées, dans les cavernes de la terre et les rochers.
7 Kwenye vichaka walilia kama punda, na walijisongasonga pamoja kwenye vichaka.
On entend leurs cris sauvages parmi les broussailles, ils se couchent ensemble sous les ronces:
8 Wao ni watoto wa wapumbavu wenye asili ya ubaya, waliofukuzwa watoke katika nchi.
gens insensés, race sans nom, bannis avec mépris de la terre habitée!
9 “Nao sasa wana wao wananidhihaki katika nyimbo; nimekuwa kitu cha dhihaka kwao.
Et maintenant je suis l'objet de leurs chansons, je suis en butte à leurs propos.
10 Wananichukia sana na kujitenga nami, wala hawasiti kunitemea mate usoni.
Ils ont horreur de moi, ils me fuient, ils ne détournent pas leur crachat de mon visage.
11 Sasa kwa kuwa Mungu ameilegeza kamba ya upinde wangu na kunitesa, wamekuwa huru kunitendea waonavyo.
Ils se donnent libre carrière pour m'outrager, ils rejettent tout frein devant moi.
12 Kuume kwangu kundi linashambulia; wao huitegea miguu yangu tanzi, na kunizingira.
Des misérables se lèvent à ma droite, ils cherchent à ébranler mes pieds, ils frayent jusqu'à moi leurs routes meurtrières.
13 Huizuia njia yangu, nao hufanikiwa katika kuniletea maafa, nami sina yeyote wa kunisaidia.
Ils ont bouleversé mes sentiers, ils travaillent à ma ruine, eux à qui personne ne porterait secours.
14 Wananijia kama watu wapitao katika ufa mpana; katikati ya magofu huja na kunishambulia.
Ils fondent sur moi, comme par une large brèche, ils se précipitent parmi les décombres.
15 Vitisho vimenifunika; heshima yangu imetoweshwa kama kwa upepo, salama yangu imetoweka kama wingu.
Les terreurs m'assiègent, ma prospérité est emportée comme un souffle, mon bonheur a passé comme un nuage.
16 “Sasa maisha yangu yamefikia mwisho; siku za mateso zimenikamata.
Et maintenant, mon âme s'épanche en moi, les jours d'affliction m'ont saisi.
17 Usiku mifupa yangu inachoma; maumivu yanayonitafuna hayatulii kamwe.
La nuit perce mes os, les consume, le mal qui me ronge ne dort pas.
18 Kwa uwezo wake mkuu Mungu huwa kwangu kama nguo; hushikamana nami kama ukosi wa vazi langu.
Par sa violence, mon vêtement a perdu sa forme, il me serre comme une tunique.
19 Yeye amenitupa kwenye matope, nami nimekuwa kama mavumbi na majivu.
Dieu m'a jeté dans la fange, je suis comme la poussière et la cendre.
20 “Ee Bwana, ninakulilia wewe lakini hunijibu; ninasimama, nawe unanitazama tu.
Je crie vers toi, et tu ne me réponds pas; je me tiens debout, et tu me regardes avec indifférence.
21 Wewe unanigeukia bila huruma; unanishambulia kwa nguvu za mkono wako.
Tu deviens cruel à mon égard, tu m'attaques avec toute la force de ton bras.
22 Unaninyakua na kunipeperusha kwa upepo; umenirusha huku na huko kwenye dhoruba kali.
Tu m'enlèves, tu me fais voler au gré du vent, et tu m'anéantis dans le fracas de la tempête.
23 Ninajua utanileta mpaka kifoni, mahali ambapo wenye uhai wote wamewekewa.
Car, je le sais, tu me mènes à la mort, au rendez-vous de tous les vivants.
24 “Hakika hakuna yeyote amshambuliaye mhitaji, anapoomba msaada katika shida yake.
Cependant celui qui va périr n'étendra-t-il pas les mains et, dans sa détresse, ne poussera-t-il pas un cri?
25 Je, sikulia kwa ajili ya wale waliokuwa katika taabu? Je, nafsi yangu haikusononeka kwa ajili ya maskini?
N'avais-je pas des larmes pour l'infortuné? Mon cœur ne s'est-il pas attendri sur l'indigent?
26 Lakini nilipotazamia mema, mabaya yalinijia; nilipotafuta nuru, ndipo giza lilipokuja.
J'attendais le bonheur, et le malheur est arrivé; j'espérais la lumière, et les ténèbres sont venues.
27 Kusukwasukwa ndani yangu kamwe hakutulii; siku za mateso zinanikabili.
Mes entrailles bouillonnent sans relâche, les jours d'affliction ont fondu sur moi.
28 Ninazunguka nikiwa nimeungua, lakini si kwa jua; ninasimama katika kusanyiko nikiomba msaada.
Je marche dans le deuil, sans soleil; si je me lève dans l'assemblée, c'est pour pousser des cris.
29 Nimekuwa ndugu wa mbweha, rafiki wa mabundi.
Je suis devenu le frère des chacals, le compagnon des filles de l'autruche.
30 Ngozi yangu imekuwa nyeusi nayo inachunika; mifupa yangu inaungua kwa homa.
Ma peau livide tombe en lambeaux, mes os sont brûlés par un feu intérieur.
31 Kinubi changu kimegeuka kuwa maombolezo, nayo filimbi yangu imekuwa sauti ya kilio.
Ma cithare ne rend plus que des accords lugubres, mon chalumeau que des sons plaintifs.

< Ayubu 30 >