< Ayubu 30 >
1 “Lakini sasa watu wadogo kwa umri kuniliko wananidhihaki, watu ambao baba zao ningekataa kwa dharau kuwaweka pamoja na mbwa wangu wa kulinda kondoo.
« Mais maintenant, ceux qui sont plus jeunes que moi me tournent en dérision, dont j'ai considéré les pères comme indignes d'être mis avec mes chiens de berger.
2 Nguvu za mikono yao zingekuwa na faida gani kwangu, kwa kuwa nguvu zao zilikuwa zimewaishia?
A quoi me sert la force de leurs mains? des hommes chez qui l'âge mûr a péri?
3 Wakiwa wamekonda kutokana na kupungukiwa na kwa njaa, walizurura usiku katika nchi kame iliyo ukiwa.
Ils sont décharnés par le manque et la famine. Ils rongent la terre aride, dans la pénombre du désert et de la désolation.
4 Katika vichaka walikusanya mimea ya chumvi, nacho chakula chao kilikuwa mizizi ya mti wa mfagio.
Ils cueillent des herbes salées près des buissons. Les racines de l'arbre à balais sont leur nourriture.
5 Walifukuzwa mbali na watu wao, wakipigiwa kelele kama wevi.
Ils sont chassés du milieu des hommes. Ils crient après eux comme après un voleur,
6 Walilazimika kuishi katika mikondo ya vijito vilivyokauka, kwenye majabali na mahandaki.
de sorte qu'ils vivent dans des vallées effrayantes, et dans les trous de la terre et des rochers.
7 Kwenye vichaka walilia kama punda, na walijisongasonga pamoja kwenye vichaka.
Ils braillent dans les buissons. Ils sont rassemblés sous les orties.
8 Wao ni watoto wa wapumbavu wenye asili ya ubaya, waliofukuzwa watoke katika nchi.
Ce sont des enfants de fous, oui, des enfants de méchants. Ils ont été chassés du pays à coups de fouet.
9 “Nao sasa wana wao wananidhihaki katika nyimbo; nimekuwa kitu cha dhihaka kwao.
« Maintenant, je suis devenu leur chant. Oui, je suis un mot d'ordre pour eux.
10 Wananichukia sana na kujitenga nami, wala hawasiti kunitemea mate usoni.
Ils m'abhorrent, ils se tiennent à l'écart de moi, et n'hésitez pas à me cracher au visage.
11 Sasa kwa kuwa Mungu ameilegeza kamba ya upinde wangu na kunitesa, wamekuwa huru kunitendea waonavyo.
Car il a détaché son cordon, et m'a fait souffrir; et ils se sont libérés de toute contrainte devant moi.
12 Kuume kwangu kundi linashambulia; wao huitegea miguu yangu tanzi, na kunizingira.
A ma droite se lève la populace. Ils ont repoussé mes pieds. Ils ont jeté contre moi leurs méthodes de destruction.
13 Huizuia njia yangu, nao hufanikiwa katika kuniletea maafa, nami sina yeyote wa kunisaidia.
Ils marquent mon chemin. Ils favorisent ma destruction sans l'aide de personne.
14 Wananijia kama watu wapitao katika ufa mpana; katikati ya magofu huja na kunishambulia.
Ils arrivent comme par une large brèche. Ils s'enroulent au milieu des ruines.
15 Vitisho vimenifunika; heshima yangu imetoweshwa kama kwa upepo, salama yangu imetoweka kama wingu.
Les terreurs se sont retournées contre moi. Ils chassent mon honneur comme le vent. Mon bien-être s'est éteint comme un nuage.
16 “Sasa maisha yangu yamefikia mwisho; siku za mateso zimenikamata.
« Maintenant mon âme est répandue au-dedans de moi. Des jours d'affliction se sont emparés de moi.
17 Usiku mifupa yangu inachoma; maumivu yanayonitafuna hayatulii kamwe.
Au temps de la nuit, mes os sont percés en moi, et les douleurs qui me rongent ne prennent aucun repos.
18 Kwa uwezo wake mkuu Mungu huwa kwangu kama nguo; hushikamana nami kama ukosi wa vazi langu.
Mon vêtement est défiguré par une grande force. Il me lie comme le col de ma tunique.
19 Yeye amenitupa kwenye matope, nami nimekuwa kama mavumbi na majivu.
Il m'a jeté dans la boue. Je suis devenu comme de la poussière et des cendres.
20 “Ee Bwana, ninakulilia wewe lakini hunijibu; ninasimama, nawe unanitazama tu.
Je crie vers toi, et tu ne me réponds pas. Je me lève, et tu me regardes.
21 Wewe unanigeukia bila huruma; unanishambulia kwa nguvu za mkono wako.
Tu t'es retourné pour être cruel envers moi. De la force de ta main, tu me persécutes.
22 Unaninyakua na kunipeperusha kwa upepo; umenirusha huku na huko kwenye dhoruba kali.
Tu me soulèves au vent, et tu me pousses avec lui. Vous me dissolvez dans la tempête.
23 Ninajua utanileta mpaka kifoni, mahali ambapo wenye uhai wote wamewekewa.
Car je sais que tu me feras mourir, à la maison désignée pour tous les vivants.
24 “Hakika hakuna yeyote amshambuliaye mhitaji, anapoomba msaada katika shida yake.
« Cependant, on ne tend pas la main dans sa chute? Ou dans sa calamité donc crier au secours?
25 Je, sikulia kwa ajili ya wale waliokuwa katika taabu? Je, nafsi yangu haikusononeka kwa ajili ya maskini?
N'ai-je pas pleuré sur celui qui était dans la détresse? Mon âme n'a-t-elle pas été affligée par les nécessiteux?
26 Lakini nilipotazamia mema, mabaya yalinijia; nilipotafuta nuru, ndipo giza lilipokuja.
J'ai cherché le bien, et le mal est venu. Quand j'ai attendu la lumière, l'obscurité est venue.
27 Kusukwasukwa ndani yangu kamwe hakutulii; siku za mateso zinanikabili.
Mon cœur est troublé, et ne se repose pas. Des jours d'affliction sont venus sur moi.
28 Ninazunguka nikiwa nimeungua, lakini si kwa jua; ninasimama katika kusanyiko nikiomba msaada.
Je suis en deuil sans le soleil. Je me lève dans l'assemblée, et je crie à l'aide.
29 Nimekuwa ndugu wa mbweha, rafiki wa mabundi.
Je suis un frère pour les chacals, et un compagnon des autruches.
30 Ngozi yangu imekuwa nyeusi nayo inachunika; mifupa yangu inaungua kwa homa.
Ma peau devient noire et se détache de moi. Mes os sont brûlés par la chaleur.
31 Kinubi changu kimegeuka kuwa maombolezo, nayo filimbi yangu imekuwa sauti ya kilio.
C'est pourquoi ma harpe s'est changée en deuil, et ma pipe dans la voix de ceux qui pleurent.