< Ayubu 30 >

1 “Lakini sasa watu wadogo kwa umri kuniliko wananidhihaki, watu ambao baba zao ningekataa kwa dharau kuwaweka pamoja na mbwa wangu wa kulinda kondoo.
But now they that are younger than I hold me in derision, Whose fathers I would have disdained to set with the dogs of my flock.
2 Nguvu za mikono yao zingekuwa na faida gani kwangu, kwa kuwa nguvu zao zilikuwa zimewaishia?
Of what use to me would be even the strength of their hands, To whom old age is lost?
3 Wakiwa wamekonda kutokana na kupungukiwa na kwa njaa, walizurura usiku katika nchi kame iliyo ukiwa.
By want and hunger they are famished; They gnaw the dry desert, The darkness of desolate wastes.
4 Katika vichaka walikusanya mimea ya chumvi, nacho chakula chao kilikuwa mizizi ya mti wa mfagio.
They gather purslain among the bushes, And the root of the broom is their bread.
5 Walifukuzwa mbali na watu wao, wakipigiwa kelele kama wevi.
They are driven from the society of men; There is a cry after them as after a thief.
6 Walilazimika kuishi katika mikondo ya vijito vilivyokauka, kwenye majabali na mahandaki.
They dwell in gloomy valleys, In caves of the earth and in rocks.
7 Kwenye vichaka walilia kama punda, na walijisongasonga pamoja kwenye vichaka.
They bray among the bushes; Under the brambles are they stretched out.
8 Wao ni watoto wa wapumbavu wenye asili ya ubaya, waliofukuzwa watoke katika nchi.
An impious and low-born race, They are beaten out of the land.
9 “Nao sasa wana wao wananidhihaki katika nyimbo; nimekuwa kitu cha dhihaka kwao.
And now I am become their song; Yea, I am their by-word!
10 Wananichukia sana na kujitenga nami, wala hawasiti kunitemea mate usoni.
They abhor me, they stand aloof from me; They forbear not to spit before my face.
11 Sasa kwa kuwa Mungu ameilegeza kamba ya upinde wangu na kunitesa, wamekuwa huru kunitendea waonavyo.
Yea, they let loose the reins, and humble me; They cast off the bridle before me.
12 Kuume kwangu kundi linashambulia; wao huitegea miguu yangu tanzi, na kunizingira.
On my right hand riseth up the brood; They thrust away my feet; They cast up against me their destructive ways.
13 Huizuia njia yangu, nao hufanikiwa katika kuniletea maafa, nami sina yeyote wa kunisaidia.
They break up my path; They hasten my fall, —They who have no helper!
14 Wananijia kama watu wapitao katika ufa mpana; katikati ya magofu huja na kunishambulia.
They come upon me as through a wide breach; Through the ruins they rush in upon me.
15 Vitisho vimenifunika; heshima yangu imetoweshwa kama kwa upepo, salama yangu imetoweka kama wingu.
Terrors are turned against me; They pursue my prosperity like the wind, And my welfare passeth away like a cloud.
16 “Sasa maisha yangu yamefikia mwisho; siku za mateso zimenikamata.
And now my soul poureth itself out upon me; Days of affliction have taken hold of me.
17 Usiku mifupa yangu inachoma; maumivu yanayonitafuna hayatulii kamwe.
By night my bones are pierced; they are torn from me, And my gnawers take no rest.
18 Kwa uwezo wake mkuu Mungu huwa kwangu kama nguo; hushikamana nami kama ukosi wa vazi langu.
Through the violence of my disease is my garment changed; It bindeth me about like the collar of my tunic.
19 Yeye amenitupa kwenye matope, nami nimekuwa kama mavumbi na majivu.
He hath cast me into the mire, And I am become like dust and ashes.
20 “Ee Bwana, ninakulilia wewe lakini hunijibu; ninasimama, nawe unanitazama tu.
I call upon Thee, but thou dost not hear me; I stand up before thee, but thou regardest me not.
21 Wewe unanigeukia bila huruma; unanishambulia kwa nguvu za mkono wako.
Thou art become cruel to me; With thy strong hand dost thou lie in wait for me.
22 Unaninyakua na kunipeperusha kwa upepo; umenirusha huku na huko kwenye dhoruba kali.
Thou liftest me up, and causest me to ride upon the wind; Thou meltest me away in the storm.
23 Ninajua utanileta mpaka kifoni, mahali ambapo wenye uhai wote wamewekewa.
I know that thou wilt bring me to death, To the place of assembly for all the living.
24 “Hakika hakuna yeyote amshambuliaye mhitaji, anapoomba msaada katika shida yake.
When He stretcheth out his hand, prayer availeth nothing; When He bringeth destruction, vain is the cry for help.
25 Je, sikulia kwa ajili ya wale waliokuwa katika taabu? Je, nafsi yangu haikusononeka kwa ajili ya maskini?
Did not I weep for him that was in trouble? Was not my soul grieved for the poor?
26 Lakini nilipotazamia mema, mabaya yalinijia; nilipotafuta nuru, ndipo giza lilipokuja.
But when I looked for good, then evil came; When I looked for light, then came darkness.
27 Kusukwasukwa ndani yangu kamwe hakutulii; siku za mateso zinanikabili.
My bowels boil, and have no rest; Days of anguish have come upon me.
28 Ninazunguka nikiwa nimeungua, lakini si kwa jua; ninasimama katika kusanyiko nikiomba msaada.
I am black, but not by the sun; I stand up, and utter my cries in the congregation.
29 Nimekuwa ndugu wa mbweha, rafiki wa mabundi.
I am become a brother to jackals, And a companion to ostriches.
30 Ngozi yangu imekuwa nyeusi nayo inachunika; mifupa yangu inaungua kwa homa.
My skin is black, and falleth from me, And my bones burn with heat.
31 Kinubi changu kimegeuka kuwa maombolezo, nayo filimbi yangu imekuwa sauti ya kilio.
My harp also is turned to mourning, And my pipe to notes of grief.

< Ayubu 30 >