< Ayubu 30 >

1 “Lakini sasa watu wadogo kwa umri kuniliko wananidhihaki, watu ambao baba zao ningekataa kwa dharau kuwaweka pamoja na mbwa wangu wa kulinda kondoo.
But now they that are younger than I have me in derision, whose fathers I disdained to set with the dogs of my flock.
2 Nguvu za mikono yao zingekuwa na faida gani kwangu, kwa kuwa nguvu zao zilikuwa zimewaishia?
Yea, the strength of their hands, whereto should it profit me? men in whom ripe age is perished.
3 Wakiwa wamekonda kutokana na kupungukiwa na kwa njaa, walizurura usiku katika nchi kame iliyo ukiwa.
They are gaunt with want and famine; they gnaw the dry ground, in the gloom of wasteness and desolation.
4 Katika vichaka walikusanya mimea ya chumvi, nacho chakula chao kilikuwa mizizi ya mti wa mfagio.
They pluck salt-wort with wormwood; and the roots of the broom are their food.
5 Walifukuzwa mbali na watu wao, wakipigiwa kelele kama wevi.
They are driven forth from the midst of men; they cry after them as after a thief.
6 Walilazimika kuishi katika mikondo ya vijito vilivyokauka, kwenye majabali na mahandaki.
In the clefts of the valleys must they dwell, in holes of the earth and of the rocks.
7 Kwenye vichaka walilia kama punda, na walijisongasonga pamoja kwenye vichaka.
Among the bushes they bray; under the nettles they are gathered together.
8 Wao ni watoto wa wapumbavu wenye asili ya ubaya, waliofukuzwa watoke katika nchi.
They are children of churls, yea, children of ignoble men; they were scourged out of the land.
9 “Nao sasa wana wao wananidhihaki katika nyimbo; nimekuwa kitu cha dhihaka kwao.
And now I am become their song, yea, I am a byword unto them.
10 Wananichukia sana na kujitenga nami, wala hawasiti kunitemea mate usoni.
They abhor me, they flee far from me, and spare not to spit in my face.
11 Sasa kwa kuwa Mungu ameilegeza kamba ya upinde wangu na kunitesa, wamekuwa huru kunitendea waonavyo.
For He hath loosed my cord, and afflicted me, and they have cast off the bridle before me.
12 Kuume kwangu kundi linashambulia; wao huitegea miguu yangu tanzi, na kunizingira.
Upon my right hand rise the brood; they entangle my feet, and they cast up against me their ways of destruction.
13 Huizuia njia yangu, nao hufanikiwa katika kuniletea maafa, nami sina yeyote wa kunisaidia.
They break up my path, they further my calamity, even men that have no helper.
14 Wananijia kama watu wapitao katika ufa mpana; katikati ya magofu huja na kunishambulia.
As through a wide breach they come; in the midst of the ruin they roll themselves upon me.
15 Vitisho vimenifunika; heshima yangu imetoweshwa kama kwa upepo, salama yangu imetoweka kama wingu.
Terrors are turned upon me, they chase mine honour as the wind; and my welfare is passed away as a cloud.
16 “Sasa maisha yangu yamefikia mwisho; siku za mateso zimenikamata.
And now my soul is poured out within me; days of affliction have taken hold upon me.
17 Usiku mifupa yangu inachoma; maumivu yanayonitafuna hayatulii kamwe.
In the night my bones are pierced, and fall from me, and my sinews take no rest.
18 Kwa uwezo wake mkuu Mungu huwa kwangu kama nguo; hushikamana nami kama ukosi wa vazi langu.
By the great force of my disease is my garment disfigured; it bindeth me about as the collar of my coat.
19 Yeye amenitupa kwenye matope, nami nimekuwa kama mavumbi na majivu.
He hath cast me into the mire, and I am become like dust and ashes.
20 “Ee Bwana, ninakulilia wewe lakini hunijibu; ninasimama, nawe unanitazama tu.
I cry unto Thee, and Thou dost not answer me; I stand up, and Thou lookest at me.
21 Wewe unanigeukia bila huruma; unanishambulia kwa nguvu za mkono wako.
Thou art turned to be cruel to me; with the might of Thy hand Thou hatest me.
22 Unaninyakua na kunipeperusha kwa upepo; umenirusha huku na huko kwenye dhoruba kali.
Thou liftest me up to the wind, Thou causest me to ride upon it; and Thou dissolvest my substance.
23 Ninajua utanileta mpaka kifoni, mahali ambapo wenye uhai wote wamewekewa.
For I know that Thou wilt bring me to death, and to the house appointed for all living.
24 “Hakika hakuna yeyote amshambuliaye mhitaji, anapoomba msaada katika shida yake.
Surely none shall put forth his hand to a ruinous heap, neither because of these things shall help come in one's calamity,
25 Je, sikulia kwa ajili ya wale waliokuwa katika taabu? Je, nafsi yangu haikusononeka kwa ajili ya maskini?
If I have not wept for him that was in trouble, and if my soul grieved not for the needy.
26 Lakini nilipotazamia mema, mabaya yalinijia; nilipotafuta nuru, ndipo giza lilipokuja.
Yet, when I looked for good, there came evil; and when I waited for light, there came darkness.
27 Kusukwasukwa ndani yangu kamwe hakutulii; siku za mateso zinanikabili.
Mine inwards boil, and rest not; days of affliction are come upon me.
28 Ninazunguka nikiwa nimeungua, lakini si kwa jua; ninasimama katika kusanyiko nikiomba msaada.
I go mourning without the sun; I stand up in the assembly, and cry for help.
29 Nimekuwa ndugu wa mbweha, rafiki wa mabundi.
I am become a brother to jackals, and a companion to ostriches.
30 Ngozi yangu imekuwa nyeusi nayo inachunika; mifupa yangu inaungua kwa homa.
My skin is black, and falleth from me, and my bones are burned with heat.
31 Kinubi changu kimegeuka kuwa maombolezo, nayo filimbi yangu imekuwa sauti ya kilio.
Therefore is my harp turned to mourning, and my pipe into the voice of them that weep.

< Ayubu 30 >