< Ayubu 30 >
1 “Lakini sasa watu wadogo kwa umri kuniliko wananidhihaki, watu ambao baba zao ningekataa kwa dharau kuwaweka pamoja na mbwa wangu wa kulinda kondoo.
But now those who are younger than I have me in derision, whose fathers I disdained to set with the dogs of my flock.
2 Nguvu za mikono yao zingekuwa na faida gani kwangu, kwa kuwa nguvu zao zilikuwa zimewaishia?
Yea, the strength of their hands, to what should it profit me? Men in whom ripe age is perished.
3 Wakiwa wamekonda kutokana na kupungukiwa na kwa njaa, walizurura usiku katika nchi kame iliyo ukiwa.
They are gaunt with want and famine. They gnaw the dry ground in the gloom of waste and desolation.
4 Katika vichaka walikusanya mimea ya chumvi, nacho chakula chao kilikuwa mizizi ya mti wa mfagio.
They pluck mallows by the bushes, and the roots of the juniper are their food.
5 Walifukuzwa mbali na watu wao, wakipigiwa kelele kama wevi.
They are driven forth from the midst of men. They cry out after them as after a thief,
6 Walilazimika kuishi katika mikondo ya vijito vilivyokauka, kwenye majabali na mahandaki.
so that they dwell in frightful valleys, in holes of the earth and of the rocks.
7 Kwenye vichaka walilia kama punda, na walijisongasonga pamoja kwenye vichaka.
Among the bushes they bray, under the nettles they are gathered together.
8 Wao ni watoto wa wapumbavu wenye asili ya ubaya, waliofukuzwa watoke katika nchi.
They are sons of fools, yea, sons of base men. They were scourged out of the land.
9 “Nao sasa wana wao wananidhihaki katika nyimbo; nimekuwa kitu cha dhihaka kwao.
And now I have become their song, Yea, I am a byword to them.
10 Wananichukia sana na kujitenga nami, wala hawasiti kunitemea mate usoni.
They abhor me. They stand aloof from me, and do not spare to spit in my face.
11 Sasa kwa kuwa Mungu ameilegeza kamba ya upinde wangu na kunitesa, wamekuwa huru kunitendea waonavyo.
For he has loosed his cord, and afflicted me. And they have cast off the bridle before me.
12 Kuume kwangu kundi linashambulia; wao huitegea miguu yangu tanzi, na kunizingira.
Upon my right hand rise the rabble. They thrust aside my feet, and they cast up against me their ways of destruction.
13 Huizuia njia yangu, nao hufanikiwa katika kuniletea maafa, nami sina yeyote wa kunisaidia.
They mar my path. They set forward my calamity, even men who have no helper.
14 Wananijia kama watu wapitao katika ufa mpana; katikati ya magofu huja na kunishambulia.
As through a wide breach they come. In the midst of the ruin they roll themselves upon me.
15 Vitisho vimenifunika; heshima yangu imetoweshwa kama kwa upepo, salama yangu imetoweka kama wingu.
Terrors are turned upon me. They chase my honor as the wind, and my welfare is passed away as a cloud.
16 “Sasa maisha yangu yamefikia mwisho; siku za mateso zimenikamata.
And now my soul is poured out within me. Days of affliction have taken hold upon me.
17 Usiku mifupa yangu inachoma; maumivu yanayonitafuna hayatulii kamwe.
In the night season my bones are pierced in me, and the pains that gnaw me take no rest.
18 Kwa uwezo wake mkuu Mungu huwa kwangu kama nguo; hushikamana nami kama ukosi wa vazi langu.
By the great force my garment is disfigured. It binds me about as the collar of my coat.
19 Yeye amenitupa kwenye matope, nami nimekuwa kama mavumbi na majivu.
He has cast me into the mire, and I have become like dust and ashes.
20 “Ee Bwana, ninakulilia wewe lakini hunijibu; ninasimama, nawe unanitazama tu.
I cry to thee, and thou do not answer me. I stand up, and thou gaze at me.
21 Wewe unanigeukia bila huruma; unanishambulia kwa nguvu za mkono wako.
Thou have turned to be cruel to me. With the might of thy hand thou persecute me.
22 Unaninyakua na kunipeperusha kwa upepo; umenirusha huku na huko kwenye dhoruba kali.
Thou lift me up to the wind. Thou cause me to ride upon it, and thou disintegrate me in the storm.
23 Ninajua utanileta mpaka kifoni, mahali ambapo wenye uhai wote wamewekewa.
For I know that thou will bring me to death, and to the house appointed for all living.
24 “Hakika hakuna yeyote amshambuliaye mhitaji, anapoomba msaada katika shida yake.
However does not a man stretch out the hand in his fall? Or in his calamity therefore cry for help?
25 Je, sikulia kwa ajili ya wale waliokuwa katika taabu? Je, nafsi yangu haikusononeka kwa ajili ya maskini?
Did I not weep for him who was in trouble? Was not my soul grieved for the needy?
26 Lakini nilipotazamia mema, mabaya yalinijia; nilipotafuta nuru, ndipo giza lilipokuja.
When I looked for good, then evil came. And when I waited for light, there came darkness.
27 Kusukwasukwa ndani yangu kamwe hakutulii; siku za mateso zinanikabili.
My heart is troubled, and does not rest. Days of affliction have come upon me.
28 Ninazunguka nikiwa nimeungua, lakini si kwa jua; ninasimama katika kusanyiko nikiomba msaada.
I go mourning without the sun. I stand up in the assembly, and cry for help.
29 Nimekuwa ndugu wa mbweha, rafiki wa mabundi.
I am a brother to jackals, and a companion to ostriches.
30 Ngozi yangu imekuwa nyeusi nayo inachunika; mifupa yangu inaungua kwa homa.
My skin is black, and falls from me. And my bones are burned with heat.
31 Kinubi changu kimegeuka kuwa maombolezo, nayo filimbi yangu imekuwa sauti ya kilio.
Therefore my harp has turned to mourning, and my pipe into the voice of those who weep.