< Ayubu 30 >

1 “Lakini sasa watu wadogo kwa umri kuniliko wananidhihaki, watu ambao baba zao ningekataa kwa dharau kuwaweka pamoja na mbwa wangu wa kulinda kondoo.
Nyní pak posmívají se mi mladší mne, jejichž bych otců nechtěl byl postaviti se psy stáda svého.
2 Nguvu za mikono yao zingekuwa na faida gani kwangu, kwa kuwa nguvu zao zilikuwa zimewaishia?
Ač síla rukou jejich k čemu by mi byla? Zmařena jest při nich starost jejich.
3 Wakiwa wamekonda kutokana na kupungukiwa na kwa njaa, walizurura usiku katika nchi kame iliyo ukiwa.
Nebo chudobou a hladem znuzeni, utíkali na planá, tmavá, soukromná a pustá místa.
4 Katika vichaka walikusanya mimea ya chumvi, nacho chakula chao kilikuwa mizizi ya mti wa mfagio.
Kteříž trhali zeliny po chrastinách, ano i koření, a jalovec za pokrm byl jim.
5 Walifukuzwa mbali na watu wao, wakipigiwa kelele kama wevi.
Z prostřed lidí vyháníni byli; povolávali za nimi, jako za zlodějem,
6 Walilazimika kuishi katika mikondo ya vijito vilivyokauka, kwenye majabali na mahandaki.
Tak že musili bydliti v výmolích potoků, v děrách země a skálí.
7 Kwenye vichaka walilia kama punda, na walijisongasonga pamoja kwenye vichaka.
V chrastinách řvali, pod trní se shromažďovali,
8 Wao ni watoto wa wapumbavu wenye asili ya ubaya, waliofukuzwa watoke katika nchi.
Lidé nejnešlechetnější, nýbrž lidé bez poctivosti, menší váhy i než ta země.
9 “Nao sasa wana wao wananidhihaki katika nyimbo; nimekuwa kitu cha dhihaka kwao.
Nyní, pravím, jsem jejich písničkou, jsa jim učiněn za přísloví.
10 Wananichukia sana na kujitenga nami, wala hawasiti kunitemea mate usoni.
V ošklivosti mne mají, vzdalují se mne, a na tvář mou nestydí se plvati.
11 Sasa kwa kuwa Mungu ameilegeza kamba ya upinde wangu na kunitesa, wamekuwa huru kunitendea waonavyo.
Nebo Bůh mou vážnost odjal, a ssoužil mne; pročež uzdu před přítomností mou svrhli.
12 Kuume kwangu kundi linashambulia; wao huitegea miguu yangu tanzi, na kunizingira.
Po pravici mládež povstává, nohy mi podrážejí, tak že šlapáním protřeli ke mně stezky nešlechetnosti své.
13 Huizuia njia yangu, nao hufanikiwa katika kuniletea maafa, nami sina yeyote wa kunisaidia.
Mou pak stezku zkazili, k bídě mé přidali, ač jim to nic nepomůže.
14 Wananijia kama watu wapitao katika ufa mpana; katikati ya magofu huja na kunishambulia.
Jako širokou mezerou vskakují, a k vyplénění mému valí se.
15 Vitisho vimenifunika; heshima yangu imetoweshwa kama kwa upepo, salama yangu imetoweka kama wingu.
Obrátily se na mne hrůzy, stihají jako vítr ochotnost mou, nebo jako oblak pomíjí zdraví mé.
16 “Sasa maisha yangu yamefikia mwisho; siku za mateso zimenikamata.
A již ve mně rozlila se duše má, pochytili mne dnové trápení mého,
17 Usiku mifupa yangu inachoma; maumivu yanayonitafuna hayatulii kamwe.
Kteréž v noci vrtá kosti mé ve mně; pročež ani nervové moji neodpočívají.
18 Kwa uwezo wake mkuu Mungu huwa kwangu kama nguo; hushikamana nami kama ukosi wa vazi langu.
Oděv můj mění se pro násilnou moc bolesti, kteráž mne tak jako obojek sukně mé svírá.
19 Yeye amenitupa kwenye matope, nami nimekuwa kama mavumbi na majivu.
Uvrhl mne do bláta, tak že jsem již podobný prachu a popelu.
20 “Ee Bwana, ninakulilia wewe lakini hunijibu; ninasimama, nawe unanitazama tu.
Volám k tobě, ó Bože, a neslyšíš mne; postavuji se, ale nehledíš na mne.
21 Wewe unanigeukia bila huruma; unanishambulia kwa nguvu za mkono wako.
Obrátils mi se v ukrutného nepřítele, silou ruky své mi odporuješ.
22 Unaninyakua na kunipeperusha kwa upepo; umenirusha huku na huko kwenye dhoruba kali.
Vznášíš mne u vítr, sázíš mne na něj, a k rozplynutí mi přivodíš zdravý soud.
23 Ninajua utanileta mpaka kifoni, mahali ambapo wenye uhai wote wamewekewa.
Nebo vím, že mne k smrti odkážeš, a do domu, do něhož se shromažďuje všeliký živý.
24 “Hakika hakuna yeyote amshambuliaye mhitaji, anapoomba msaada katika shida yake.
Jistě žeť nevztáhne Bůh do hrobu ruky, by pak, když je stírá, i volali.
25 Je, sikulia kwa ajili ya wale waliokuwa katika taabu? Je, nafsi yangu haikusononeka kwa ajili ya maskini?
Zdaliž jsem neplakal nad tím, kdož okoušel zlých dnů? Duše má kormoutila se nad nuzným.
26 Lakini nilipotazamia mema, mabaya yalinijia; nilipotafuta nuru, ndipo giza lilipokuja.
Když jsem dobrého čekal, přišlo mi zlé; nadál jsem se světla, ale přišla mrákota.
27 Kusukwasukwa ndani yangu kamwe hakutulii; siku za mateso zinanikabili.
Vnitřností mé zevřely, tak že se ještě neupokojily; předstihli mne dnové trápení.
28 Ninazunguka nikiwa nimeungua, lakini si kwa jua; ninasimama katika kusanyiko nikiomba msaada.
Chodím osmahlý, ne od slunce, povstávaje, i mezi mnohými křičím.
29 Nimekuwa ndugu wa mbweha, rafiki wa mabundi.
Bratrem učiněn jsem draků, a tovaryšem mladých pstrosů.
30 Ngozi yangu imekuwa nyeusi nayo inachunika; mifupa yangu inaungua kwa homa.
Kůže má zčernala na mně, a kosti mé vyprahly od horkosti.
31 Kinubi changu kimegeuka kuwa maombolezo, nayo filimbi yangu imekuwa sauti ya kilio.
A protož v kvílení obrátila se harfa má, a píšťalka má v hlas plačících.

< Ayubu 30 >