< Ayubu 3 >
1 Baada ya jambo hili, Ayubu akafumbua kinywa chake na kuilaani siku ya kuzaliwa kwake.
Entonces, abriendo su boca y maldiciendo el día de su nacimiento,
3 “Siku ya kuzaliwa kwangu na ipotelee mbali, nao usiku ule iliposemekana, ‘Mtoto wa kiume amezaliwa!’
Perezca el día de mi nacimiento y la noche en que se dijo: Un niño es concebido.
4 Siku ile na iwe giza; Mungu juu na asiiangalie; nayo nuru isiiangazie.
Que ese día, hubiera sido oscuro; y Dios no hubiera tomado nota de esto desde lo alto, y no hubiera resplandecido la luz del día;
5 Giza na kivuli kikuu kiikalie tena; wingu na likae juu yake; weusi na uifunike nuru yake.
Deja que la oscuridad y la noche negra sea su redentor; deja que se cubra con una nube; Deja que las sombras oscuras del día te envíen miedo.
6 Usiku ule na ushikwe na giza kuu; usihesabiwe katika siku za mwaka, wala usihesabiwe katika siku za mwezi wowote.
En cuanto a esa noche que la oscuridad espesa la tome; Que no tenga gozo entre los días del año; Que no venga en el número de los meses.
7 Usiku ule na uwe tasa; sauti ya furaha na isisikike ndani yake.
En cuanto a esa noche, que hubiera sido estéril; Que ninguna voz de alegría hubiera sonado en ella;
8 Wale wazilaanio siku wailaani hiyo siku, wale walio tayari kumwamsha Lewiathani.
Que la maldigan los que ponen una maldición en el día; que están listos para despertar a Leviatán.
9 Nyota zake za alfajiri na ziwe giza; nao ungojee mwanga bila mafanikio, wala usiuone mwonzi wa kwanza wa mapambazuko,
Sean oscuras sus estrellas de la mañana; Que esté buscando luz, pero que no la tenga; Que no vea los rayos del alba.
10 kwa sababu huo usiku haukunifungia mlango wa tumbo la mama yangu, ili kuyaficha macho yangu kutokana na taabu.
Porque no cerró las puertas del vientre de mi madre, ni oculto los problemas de mis ojos.
11 “Kwa nini sikuangamia wakati wa kuzaliwa? Kwa nini sikufa nilipokuwa ninatoka tumboni?
¿Por qué la muerte no me tomó cuando salí del cuerpo de mi madre, por qué no, cuando salí del vientre, entregue mi espíritu?
12 Kwa nini pakawa na magoti ya kunipokea na matiti ili nipate kunyonyeshwa?
¿Por qué hubo rodillas que me recibieron o por qué los pechos para que me den leche?
13 Kwa maana sasa ningekuwa nimepumzika kwa amani. Ningekuwa nimelala na kupumzika
Porque entonces podría haber ido a mi descanso en silencio, y en el sueño, haber estado en paz,
14 pamoja na wafalme na washauri wa dunia, waliojijengea mahali ambapo sasa ni magofu,
Con los reyes y los sabios de la tierra, que edificaron grandes casas para sí mismos;
15 pamoja na watawala waliokuwa na dhahabu, waliozijaza nyumba zao kwa fedha.
O con los gobernantes que tenían oro, y cuyas casas estaban llenas de plata;
16 Au kwa nini sikufichwa ardhini kama mtoto aliyezaliwa mfu, kama mtoto mchanga ambaye kamwe hakuuona mwanga?
O como un aborto de niño que nunca podría haber existido; Como niños pequeños que no han visto la luz.
17 Huko waovu huacha kusumbua na huko waliochoka hupumzika.
Allí dejan de perturbar los malvados, y aquellos cuyas fuerzas han llegado a su fin tienen descanso.
18 Wafungwa nao hufurahia utulivu wao, hawasikii tena sauti ya kukemea ya kiongozi wa watumwa.
Allí los prisioneros están en paz juntos. La voz del capataz no vuelve a sus oídos.
19 Wadogo na wakubwa wamo humo, na mtumwa ameachiwa huru kutoka kwa bwana wake.
El pequeño y el grande están allí, y el siervo está libre de su amo.
20 “Mbona nuru inawaangazia wale walio taabuni, na hao wenye uchungu kupewa uhai,
¿Por qué le da luz al que está en problemas, y la vida al alma amarga;
21 wale wanaotamani kifo ambacho hakiji, wale watafutao kufa zaidi ya kutafuta hazina iliyofichwa,
Para aquellos cuyo deseo es la muerte, pero no viene; que la buscan más que la riqueza secreta;
22 ambao hujawa na furaha, na hushangilia wafikapo kaburini?
¿Que se alegran con gran gozo y se regocijan cuando llegan a su último lugar de descanso;
23 Kwa nini uhai hupewa mtu ambaye njia yake imefichika, ambaye Mungu amemzungushia boma?
Pporque se le da luz a un hombre que no sabe por donde va, y que está acorralado por Dios?
24 Kwa maana kulia kwangu kwa uchungu kwanijia badala ya chakula; kusononeka kwangu kunamwagika kama maji.
En lugar de mi comida tengo pena, y de mí salen gritos de dolor como agua.
25 Lile nililokuwa naliogopa limenijia; lile nililokuwa ninalihofia limenipata.
Porque lo que estaba temiendo ha venido sobre mi y de lo cual tengo miedo me aconteció.
26 Sina amani, wala utulivu; sina pumziko, bali taabu tu.”
No tengo paz, ni silencio, ni descanso; nada más que el dolor viene sobre mí.