< Ayubu 3 >
1 Baada ya jambo hili, Ayubu akafumbua kinywa chake na kuilaani siku ya kuzaliwa kwake.
Después de esto, Job abrió la boca y maldijo el día de su nacimiento.
3 “Siku ya kuzaliwa kwangu na ipotelee mbali, nao usiku ule iliposemekana, ‘Mtoto wa kiume amezaliwa!’
“Que perezca el día en que nací, la noche que dijo: “Hay un niño concebido”.
4 Siku ile na iwe giza; Mungu juu na asiiangalie; nayo nuru isiiangazie.
Que ese día sea la oscuridad. No dejes que Dios desde arriba lo busque, ni dejar que la luz lo ilumine.
5 Giza na kivuli kikuu kiikalie tena; wingu na likae juu yake; weusi na uifunike nuru yake.
Que las tinieblas y la sombra de la muerte la reclamen para sí. Deja que una nube se detenga en ella. Que todo lo que hace el día negro lo aterrorice.
6 Usiku ule na ushikwe na giza kuu; usihesabiwe katika siku za mwaka, wala usihesabiwe katika siku za mwezi wowote.
En cuanto a esa noche, que la oscuridad espesa se apodere de ella. Que no se regocije entre los días del año. Que no entre en el número de los meses.
7 Usiku ule na uwe tasa; sauti ya furaha na isisikike ndani yake.
He aquí, que esa noche sea estéril. Que no venga ninguna voz alegre.
8 Wale wazilaanio siku wailaani hiyo siku, wale walio tayari kumwamsha Lewiathani.
Que lo maldigan los que maldicen el día, que están listos para despertar al Leviatán.
9 Nyota zake za alfajiri na ziwe giza; nao ungojee mwanga bila mafanikio, wala usiuone mwonzi wa kwanza wa mapambazuko,
Que las estrellas de su crepúsculo sean oscuras. Que busque la luz, pero no la tenga, ni dejar que vea los párpados de la mañana,
10 kwa sababu huo usiku haukunifungia mlango wa tumbo la mama yangu, ili kuyaficha macho yangu kutokana na taabu.
porque no cerró las puertas del vientre de mi madre, ni ocultó los problemas a mis ojos.
11 “Kwa nini sikuangamia wakati wa kuzaliwa? Kwa nini sikufa nilipokuwa ninatoka tumboni?
“¿Por qué no he muerto desde el vientre? ¿Por qué no renuncié al espíritu cuando mi madre me dio a luz?
12 Kwa nini pakawa na magoti ya kunipokea na matiti ili nipate kunyonyeshwa?
¿Por qué me recibieron las rodillas? ¿O por qué el pecho, que debo amamantar?
13 Kwa maana sasa ningekuwa nimepumzika kwa amani. Ningekuwa nimelala na kupumzika
Por ahora debería haberme acostado y callado. Debería haber dormido, así habría descansado,
14 pamoja na wafalme na washauri wa dunia, waliojijengea mahali ambapo sasa ni magofu,
con reyes y consejeros de la tierra, que construyeron lugares de desecho para sí mismos;
15 pamoja na watawala waliokuwa na dhahabu, waliozijaza nyumba zao kwa fedha.
o con príncipes que tenían oro, que llenaron sus casas de plata;
16 Au kwa nini sikufichwa ardhini kama mtoto aliyezaliwa mfu, kama mtoto mchanga ambaye kamwe hakuuona mwanga?
o como un nacimiento intempestivo oculto no había sido, como niños que nunca vieron la luz.
17 Huko waovu huacha kusumbua na huko waliochoka hupumzika.
Allí los malvados dejan de molestar. Allí descansan los cansados.
18 Wafungwa nao hufurahia utulivu wao, hawasikii tena sauti ya kukemea ya kiongozi wa watumwa.
Allí los prisioneros están a gusto juntos. No oyen la voz del capataz.
19 Wadogo na wakubwa wamo humo, na mtumwa ameachiwa huru kutoka kwa bwana wake.
Los pequeños y los grandes están allí. El siervo es libre de su amo.
20 “Mbona nuru inawaangazia wale walio taabuni, na hao wenye uchungu kupewa uhai,
“¿Por qué se da luz al que está en la miseria? vida a los amargados del alma,
21 wale wanaotamani kifo ambacho hakiji, wale watafutao kufa zaidi ya kutafuta hazina iliyofichwa,
que anhelan la muerte, pero no llega; y cavar para ello más que para los tesoros ocultos,
22 ambao hujawa na furaha, na hushangilia wafikapo kaburini?
que se regocijan en exceso, y se alegran, cuando pueden encontrar la tumba?
23 Kwa nini uhai hupewa mtu ambaye njia yake imefichika, ambaye Mungu amemzungushia boma?
Por qué se da luz a un hombre cuyo camino está oculto, a los que Dios ha cobijado?
24 Kwa maana kulia kwangu kwa uchungu kwanijia badala ya chakula; kusononeka kwangu kunamwagika kama maji.
Porque mis suspiros llegan antes de comer. Mis gemidos se derraman como agua.
25 Lile nililokuwa naliogopa limenijia; lile nililokuwa ninalihofia limenipata.
Porque lo que temo viene sobre mí, lo que me da miedo viene a mí.
26 Sina amani, wala utulivu; sina pumziko, bali taabu tu.”
No estoy tranquilo, ni tengo descanso; pero los problemas vienen”.