< Ayubu 3 >

1 Baada ya jambo hili, Ayubu akafumbua kinywa chake na kuilaani siku ya kuzaliwa kwake.
Después de esto Job comenzó a hablar, maldiciendo el día de su nacimiento.
2 Kisha akasema:
Y dijo:
3 “Siku ya kuzaliwa kwangu na ipotelee mbali, nao usiku ule iliposemekana, ‘Mtoto wa kiume amezaliwa!’
“Que el día en que nací sea borrado, así como la noche en que se anunció que un niño había sido concebido.
4 Siku ile na iwe giza; Mungu juu na asiiangalie; nayo nuru isiiangazie.
Que ese día se convierta en tinieblas. Que el Dios de arriba no lo recuerde. Que no brille la luz sobre él.
5 Giza na kivuli kikuu kiikalie tena; wingu na likae juu yake; weusi na uifunike nuru yake.
Cúbranlo con oscuridad y sombra de muerte. Una nube negra debería ensombrecerlo. Debería ser tan aterrador como la oscuridad de un eclipse de día.
6 Usiku ule na ushikwe na giza kuu; usihesabiwe katika siku za mwaka, wala usihesabiwe katika siku za mwezi wowote.
Borren esa noche como si nunca hubiera existido. No la cuenten en el calendario. Que no tenga día en ningún mes.
7 Usiku ule na uwe tasa; sauti ya furaha na isisikike ndani yake.
“Que en esa noche no nazcan niños, que no se escuchen sonidos de felicidad.
8 Wale wazilaanio siku wailaani hiyo siku, wale walio tayari kumwamsha Lewiathani.
Que la maldigan los que maldicen ciertos días, los que tienen el poder de sacar al Leviatán.
9 Nyota zake za alfajiri na ziwe giza; nao ungojee mwanga bila mafanikio, wala usiuone mwonzi wa kwanza wa mapambazuko,
Que sus estrellas de la madrugada permanezcan oscuras. Que al buscar la luz, no vea ninguna, que no vea el resplandor del amanecer
10 kwa sababu huo usiku haukunifungia mlango wa tumbo la mama yangu, ili kuyaficha macho yangu kutokana na taabu.
porque no cerró el vientre de mi madre para impedirme ver los problemas.
11 “Kwa nini sikuangamia wakati wa kuzaliwa? Kwa nini sikufa nilipokuwa ninatoka tumboni?
“¿Por qué no nací muerto? ¿Por qué no morí al nacer?
12 Kwa nini pakawa na magoti ya kunipokea na matiti ili nipate kunyonyeshwa?
¿Por qué hubo un regazo para que me acostara, y pechos para que me amamantaran?
13 Kwa maana sasa ningekuwa nimepumzika kwa amani. Ningekuwa nimelala na kupumzika
Ahora estaría acostado en paz, durmiendo y descansando
14 pamoja na wafalme na washauri wa dunia, waliojijengea mahali ambapo sasa ni magofu,
junto con los reyes de este mundo y sus funcionarios cuyos palacios ahora yacen en ruinas;
15 pamoja na watawala waliokuwa na dhahabu, waliozijaza nyumba zao kwa fedha.
o con los nobles que coleccionaban oro y llenaban sus casas de plata.
16 Au kwa nini sikufichwa ardhini kama mtoto aliyezaliwa mfu, kama mtoto mchanga ambaye kamwe hakuuona mwanga?
¿Por qué no fui un aborto, enterrado en secreto, un bebé que nunca vio la luz?
17 Huko waovu huacha kusumbua na huko waliochoka hupumzika.
Allí, en la tumba, los malvados no dan más problemas, y los que ya no tienen fuerzas tienen su descanso.
18 Wafungwa nao hufurahia utulivu wao, hawasikii tena sauti ya kukemea ya kiongozi wa watumwa.
Allí los prisioneros descansan y no escuchan las órdenes de sus opresores.
19 Wadogo na wakubwa wamo humo, na mtumwa ameachiwa huru kutoka kwa bwana wake.
Tanto los pequeños como los grandes están allí, y los esclavos son liberados de sus amos.
20 “Mbona nuru inawaangazia wale walio taabuni, na hao wenye uchungu kupewa uhai,
¿Por qué Dios da vida a los que sufren, a los que viven amargamente,
21 wale wanaotamani kifo ambacho hakiji, wale watafutao kufa zaidi ya kutafuta hazina iliyofichwa,
a los que esperan una muerte que no llega y a los que buscan la muerte más desesperadamente que la caza de un tesoro?
22 ambao hujawa na furaha, na hushangilia wafikapo kaburini?
¡Son tan increíblemente felices cuando llegan a la tumba!
23 Kwa nini uhai hupewa mtu ambaye njia yake imefichika, ambaye Mungu amemzungushia boma?
¿Por qué se da luz a quien no sabe a dónde va, a quien Dios ha cercado?
24 Kwa maana kulia kwangu kwa uchungu kwanijia badala ya chakula; kusononeka kwangu kunamwagika kama maji.
“Mis gemidos son el pan que como, y mis lágrimas son el agua que bebo.
25 Lile nililokuwa naliogopa limenijia; lile nililokuwa ninalihofia limenipata.
Porque todo lo que temía me ha sucedido; todo lo que temía me ha sobrevenido.
26 Sina amani, wala utulivu; sina pumziko, bali taabu tu.”
No tengo paz, ni tranquilidad, ni descanso. Lo único que siento es rabia”.

< Ayubu 3 >