< Ayubu 3 >
1 Baada ya jambo hili, Ayubu akafumbua kinywa chake na kuilaani siku ya kuzaliwa kwake.
Depois disto Jó abriu sua boca, e amaldiçoou seu dia.
Pois Jó respondeu, e disse:
3 “Siku ya kuzaliwa kwangu na ipotelee mbali, nao usiku ule iliposemekana, ‘Mtoto wa kiume amezaliwa!’
Pereça o dia em que nasci, e a noite [em que] se disse: Um homem foi concebido.
4 Siku ile na iwe giza; Mungu juu na asiiangalie; nayo nuru isiiangazie.
Torne-se aquele dia em trevas; Deus não lhe dê atenção desde acima, nem claridade brilhe sobre ele.
5 Giza na kivuli kikuu kiikalie tena; wingu na likae juu yake; weusi na uifunike nuru yake.
Reivindiquem-no para si trevas e sombra de morte; nuvens habitem sobre ele; a escuridão do dia o espante.
6 Usiku ule na ushikwe na giza kuu; usihesabiwe katika siku za mwaka, wala usihesabiwe katika siku za mwezi wowote.
Tome a escuridão aquela noite; não seja contada entre os dias do ano, nem faça parte do número dos meses.
7 Usiku ule na uwe tasa; sauti ya furaha na isisikike ndani yake.
Ah se aquela noite fosse solitária, e música de alegria não viesse a ela!
8 Wale wazilaanio siku wailaani hiyo siku, wale walio tayari kumwamsha Lewiathani.
Amaldiçoem-na os que amaldiçoam o dia, os que se preparam para levantar seu pranto.
9 Nyota zake za alfajiri na ziwe giza; nao ungojee mwanga bila mafanikio, wala usiuone mwonzi wa kwanza wa mapambazuko,
Escureçam-se as estrelas de sua manhã; espere a luz, e não venha, e as pálpebras não vejam o amanhecer;
10 kwa sababu huo usiku haukunifungia mlango wa tumbo la mama yangu, ili kuyaficha macho yangu kutokana na taabu.
Pois não fechou as portas do ventre onde eu estava, nem escondeu de meus olhos o sofrimento.
11 “Kwa nini sikuangamia wakati wa kuzaliwa? Kwa nini sikufa nilipokuwa ninatoka tumboni?
Por que eu não morri desde a madre, ou perdi a vida ao sair do ventre?
12 Kwa nini pakawa na magoti ya kunipokea na matiti ili nipate kunyonyeshwa?
Por que joelhos me receberam? E por que seios me amamentaram?
13 Kwa maana sasa ningekuwa nimepumzika kwa amani. Ningekuwa nimelala na kupumzika
Pois agora eu jazeria e repousaria; dormiria, e então haveria repouso para mim;
14 pamoja na wafalme na washauri wa dunia, waliojijengea mahali ambapo sasa ni magofu,
Com os reis e os conselheiros da terra, que edificavam para si os desertos;
15 pamoja na watawala waliokuwa na dhahabu, waliozijaza nyumba zao kwa fedha.
Ou com os príncipes que tinham ouro, que enchiam suas casas de prata.
16 Au kwa nini sikufichwa ardhini kama mtoto aliyezaliwa mfu, kama mtoto mchanga ambaye kamwe hakuuona mwanga?
Ou [por que] não fui como um aborto oculto, como as crianças que nunca viram a luz?
17 Huko waovu huacha kusumbua na huko waliochoka hupumzika.
Ali os maus deixam de perturbar, e ali repousam os cansados de forças.
18 Wafungwa nao hufurahia utulivu wao, hawasikii tena sauti ya kukemea ya kiongozi wa watumwa.
Ali os prisioneiros juntamente repousam; [e] não ouvem a voz do opressor.
19 Wadogo na wakubwa wamo humo, na mtumwa ameachiwa huru kutoka kwa bwana wake.
Ali estão o pequeno e o grande; e o servo livre [está] de seu senhor.
20 “Mbona nuru inawaangazia wale walio taabuni, na hao wenye uchungu kupewa uhai,
Por que se dá luz ao sofredor, e vida aos amargos de alma,
21 wale wanaotamani kifo ambacho hakiji, wale watafutao kufa zaidi ya kutafuta hazina iliyofichwa,
Que esperam a morte, e ela não chega, e que a buscam mais que tesouros;
22 ambao hujawa na furaha, na hushangilia wafikapo kaburini?
Que saltam de alegram e ficam contentes quando acham a sepultura?
23 Kwa nini uhai hupewa mtu ambaye njia yake imefichika, ambaye Mungu amemzungushia boma?
[E também] ao homem cujo caminho é oculto, e a quem Deus [o] encobriu?
24 Kwa maana kulia kwangu kwa uchungu kwanijia badala ya chakula; kusononeka kwangu kunamwagika kama maji.
Pois antes do meu pão vem meu suspiro; e meus gemidos correm como águas.
25 Lile nililokuwa naliogopa limenijia; lile nililokuwa ninalihofia limenipata.
Pois aquilo eu temia tanto veio a mim, e aquilo que tinha medo me aconteceu.
26 Sina amani, wala utulivu; sina pumziko, bali taabu tu.”
Não tenho tido descanso, nem tranquilidade, nem repouso; mas perturbação veio sobre mim.