< Ayubu 3 >
1 Baada ya jambo hili, Ayubu akafumbua kinywa chake na kuilaani siku ya kuzaliwa kwake.
Post haec aperuit Iob os suum, et maledixit diei suo,
3 “Siku ya kuzaliwa kwangu na ipotelee mbali, nao usiku ule iliposemekana, ‘Mtoto wa kiume amezaliwa!’
Pereat dies in qua natus sum, et nox in qua dictum est: Conceptus est homo.
4 Siku ile na iwe giza; Mungu juu na asiiangalie; nayo nuru isiiangazie.
Dies ille vertatur in tenebras, non requirat eum Deus desuper, et non illustretur lumine.
5 Giza na kivuli kikuu kiikalie tena; wingu na likae juu yake; weusi na uifunike nuru yake.
Obscurent eum tenebrae et umbra mortis, occupet eum caligo, et involvatur amaritudine.
6 Usiku ule na ushikwe na giza kuu; usihesabiwe katika siku za mwaka, wala usihesabiwe katika siku za mwezi wowote.
Noctem illam tenebrosus turbo possideat, non computetur in diebus anni, nec numeretur in mensibus:
7 Usiku ule na uwe tasa; sauti ya furaha na isisikike ndani yake.
Sit nox illa solitaria, nec laude digna:
8 Wale wazilaanio siku wailaani hiyo siku, wale walio tayari kumwamsha Lewiathani.
Maledicant ei qui maledicunt diei, qui parati sunt suscitare Leviathan:
9 Nyota zake za alfajiri na ziwe giza; nao ungojee mwanga bila mafanikio, wala usiuone mwonzi wa kwanza wa mapambazuko,
Obtenebrentur stellae caligine eius: expectet lucem et non videat, nec ortum surgentis aurorae:
10 kwa sababu huo usiku haukunifungia mlango wa tumbo la mama yangu, ili kuyaficha macho yangu kutokana na taabu.
Quia non conclusit ostia ventris, qui portavit me, nec abstulit mala ab oculis meis.
11 “Kwa nini sikuangamia wakati wa kuzaliwa? Kwa nini sikufa nilipokuwa ninatoka tumboni?
Quare non in vulva mortuus sum, egressus ex utero non statim perii?
12 Kwa nini pakawa na magoti ya kunipokea na matiti ili nipate kunyonyeshwa?
Quare exceptus genibus? cur lactatus uberibus?
13 Kwa maana sasa ningekuwa nimepumzika kwa amani. Ningekuwa nimelala na kupumzika
Nunc enim dormiens silerem, et somno meo requiescerem:
14 pamoja na wafalme na washauri wa dunia, waliojijengea mahali ambapo sasa ni magofu,
Cum regibus et consulibus terrae, qui aedificant sibi solitudines:
15 pamoja na watawala waliokuwa na dhahabu, waliozijaza nyumba zao kwa fedha.
Aut cum principibus, qui possident aurum, et replent domos suas argento:
16 Au kwa nini sikufichwa ardhini kama mtoto aliyezaliwa mfu, kama mtoto mchanga ambaye kamwe hakuuona mwanga?
Aut sicut abortivum absconditum non subsisterem, vel qui concepti non viderunt lucem.
17 Huko waovu huacha kusumbua na huko waliochoka hupumzika.
Ibi impii cessaverunt a tumultu, et ibi requieverunt fessi robore.
18 Wafungwa nao hufurahia utulivu wao, hawasikii tena sauti ya kukemea ya kiongozi wa watumwa.
Et quondam vincti pariter sine molestia, non audierunt vocem exactoris.
19 Wadogo na wakubwa wamo humo, na mtumwa ameachiwa huru kutoka kwa bwana wake.
Parvus et magnus ibi sunt, et servus liber a domino suo.
20 “Mbona nuru inawaangazia wale walio taabuni, na hao wenye uchungu kupewa uhai,
Quare misero data est lux, et vita his, qui in amaritudine animae sunt?
21 wale wanaotamani kifo ambacho hakiji, wale watafutao kufa zaidi ya kutafuta hazina iliyofichwa,
qui expectant mortem, et non venit, quasi effodientes thesaurum:
22 ambao hujawa na furaha, na hushangilia wafikapo kaburini?
Gaudentque vehementer cum invenerint sepulchrum.
23 Kwa nini uhai hupewa mtu ambaye njia yake imefichika, ambaye Mungu amemzungushia boma?
Viro cuius abscondita est via, et circumdedit eum Deus tenebris?
24 Kwa maana kulia kwangu kwa uchungu kwanijia badala ya chakula; kusononeka kwangu kunamwagika kama maji.
Antequam comedam suspiro: et tamquam inundantes aquae, sic rugitus meus:
25 Lile nililokuwa naliogopa limenijia; lile nililokuwa ninalihofia limenipata.
Quia timor, quem timebam, evenit mihi: et quod verebar accidit.
26 Sina amani, wala utulivu; sina pumziko, bali taabu tu.”
Nonne dissimulavi? nonne silui? nonne quievi? et venit super me indignatio.