< Ayubu 3 >

1 Baada ya jambo hili, Ayubu akafumbua kinywa chake na kuilaani siku ya kuzaliwa kwake.
Après cela, Job ouvrit la bouche et maudit le jour de sa naissance.
2 Kisha akasema:
Il prit la parole et dit:
3 “Siku ya kuzaliwa kwangu na ipotelee mbali, nao usiku ule iliposemekana, ‘Mtoto wa kiume amezaliwa!’
Périsse le jour où je suis né, Et la nuit qui dit: Un enfant mâle est conçu!
4 Siku ile na iwe giza; Mungu juu na asiiangalie; nayo nuru isiiangazie.
Ce jour! Qu’il se change en ténèbres, Que Dieu n’en ait point souci dans le ciel, Et que la lumière ne rayonne plus sur lui!
5 Giza na kivuli kikuu kiikalie tena; wingu na likae juu yake; weusi na uifunike nuru yake.
Que l’obscurité et l’ombre de la mort s’en emparent, Que des nuées établissent leur demeure au-dessus de lui, Et que de noirs phénomènes l’épouvantent!
6 Usiku ule na ushikwe na giza kuu; usihesabiwe katika siku za mwaka, wala usihesabiwe katika siku za mwezi wowote.
Cette nuit! Que les ténèbres en fassent leur proie, Qu’elle disparaisse de l’année, Qu’elle ne soit plus comptée parmi les mois!
7 Usiku ule na uwe tasa; sauti ya furaha na isisikike ndani yake.
Que cette nuit devienne stérile, Que l’allégresse en soit bannie!
8 Wale wazilaanio siku wailaani hiyo siku, wale walio tayari kumwamsha Lewiathani.
Qu’elle soit maudite par ceux qui maudissent les jours, Par ceux qui savent exciter le léviathan!
9 Nyota zake za alfajiri na ziwe giza; nao ungojee mwanga bila mafanikio, wala usiuone mwonzi wa kwanza wa mapambazuko,
Que les étoiles de son crépuscule s’obscurcissent, Qu’elle attende en vain la lumière, Et qu’elle ne voie point les paupières de l’aurore!
10 kwa sababu huo usiku haukunifungia mlango wa tumbo la mama yangu, ili kuyaficha macho yangu kutokana na taabu.
Car elle n’a pas fermé le sein qui me conçut, Ni dérobé la souffrance à mes regards.
11 “Kwa nini sikuangamia wakati wa kuzaliwa? Kwa nini sikufa nilipokuwa ninatoka tumboni?
Pourquoi ne suis-je pas mort dans le ventre de ma mère? Pourquoi n’ai-je pas expiré au sortir de ses entrailles?
12 Kwa nini pakawa na magoti ya kunipokea na matiti ili nipate kunyonyeshwa?
Pourquoi ai-je trouvé des genoux pour me recevoir, Et des mamelles pour m’allaiter?
13 Kwa maana sasa ningekuwa nimepumzika kwa amani. Ningekuwa nimelala na kupumzika
Je serais couché maintenant, je serais tranquille, Je dormirais, je reposerais,
14 pamoja na wafalme na washauri wa dunia, waliojijengea mahali ambapo sasa ni magofu,
Avec les rois et les grands de la terre, Qui se bâtirent des mausolées,
15 pamoja na watawala waliokuwa na dhahabu, waliozijaza nyumba zao kwa fedha.
Avec les princes qui avaient de l’or, Et qui remplirent d’argent leurs demeures.
16 Au kwa nini sikufichwa ardhini kama mtoto aliyezaliwa mfu, kama mtoto mchanga ambaye kamwe hakuuona mwanga?
Ou je n’existerais pas, je serais comme un avorton caché, Comme des enfants qui n’ont pas vu la lumière.
17 Huko waovu huacha kusumbua na huko waliochoka hupumzika.
Là ne s’agitent plus les méchants, Et là se reposent ceux qui sont fatigués et sans force;
18 Wafungwa nao hufurahia utulivu wao, hawasikii tena sauti ya kukemea ya kiongozi wa watumwa.
Les captifs sont tous en paix, Ils n’entendent pas la voix de l’oppresseur;
19 Wadogo na wakubwa wamo humo, na mtumwa ameachiwa huru kutoka kwa bwana wake.
Le petit et le grand sont là, Et l’esclave n’est plus soumis à son maître.
20 “Mbona nuru inawaangazia wale walio taabuni, na hao wenye uchungu kupewa uhai,
Pourquoi donne-t-il la lumière à celui qui souffre, Et la vie à ceux qui ont l’amertume dans l’âme,
21 wale wanaotamani kifo ambacho hakiji, wale watafutao kufa zaidi ya kutafuta hazina iliyofichwa,
Qui espèrent en vain la mort, Et qui la convoitent plus qu’un trésor,
22 ambao hujawa na furaha, na hushangilia wafikapo kaburini?
Qui seraient transportés de joie Et saisis d’allégresse, s’ils trouvaient le tombeau?
23 Kwa nini uhai hupewa mtu ambaye njia yake imefichika, ambaye Mungu amemzungushia boma?
A l’homme qui ne sait où aller, Et que Dieu cerne de toutes parts?
24 Kwa maana kulia kwangu kwa uchungu kwanijia badala ya chakula; kusononeka kwangu kunamwagika kama maji.
Mes soupirs sont ma nourriture, Et mes cris se répandent comme l’eau.
25 Lile nililokuwa naliogopa limenijia; lile nililokuwa ninalihofia limenipata.
Ce que je crains, c’est ce qui m’arrive; Ce que je redoute, c’est ce qui m’atteint.
26 Sina amani, wala utulivu; sina pumziko, bali taabu tu.”
Je n’ai ni tranquillité, ni paix, ni repos, Et le trouble s’est emparé de moi.

< Ayubu 3 >