< Ayubu 3 >

1 Baada ya jambo hili, Ayubu akafumbua kinywa chake na kuilaani siku ya kuzaliwa kwake.
Aftir these thingis Joob openyde his mouth,
2 Kisha akasema:
and curside his dai, and seide, Perische the dai in which Y was borun,
3 “Siku ya kuzaliwa kwangu na ipotelee mbali, nao usiku ule iliposemekana, ‘Mtoto wa kiume amezaliwa!’
and the nyyt in which it was seid, The man is conceyued.
4 Siku ile na iwe giza; Mungu juu na asiiangalie; nayo nuru isiiangazie.
Thilke dai be turnede in to derknessis; God seke not it aboue, and be it not in mynde, nethir be it liytned with liyt.
5 Giza na kivuli kikuu kiikalie tena; wingu na likae juu yake; weusi na uifunike nuru yake.
Derknessis make it derk, and the schadewe of deeth and myist occupie it; and be it wlappid with bittirnesse.
6 Usiku ule na ushikwe na giza kuu; usihesabiwe katika siku za mwaka, wala usihesabiwe katika siku za mwezi wowote.
Derk whirlwynde holde that niyt; be it not rikynyd among the daies of the yeer, nethir be it noumbrid among the monethes.
7 Usiku ule na uwe tasa; sauti ya furaha na isisikike ndani yake.
Thilke nyyt be soleyn, and not worthi of preisyng.
8 Wale wazilaanio siku wailaani hiyo siku, wale walio tayari kumwamsha Lewiathani.
Curse thei it, that cursen the dai, that ben redi to reise Leuyathan.
9 Nyota zake za alfajiri na ziwe giza; nao ungojee mwanga bila mafanikio, wala usiuone mwonzi wa kwanza wa mapambazuko,
Sterris be maad derk with the derknesse therof; abide it liyt, and se it not, nethir the bigynnyng of the morwetid risyng vp.
10 kwa sababu huo usiku haukunifungia mlango wa tumbo la mama yangu, ili kuyaficha macho yangu kutokana na taabu.
For it closide not the doris of the wombe, that bar me, nethir took awei yuels fro min iyen.
11 “Kwa nini sikuangamia wakati wa kuzaliwa? Kwa nini sikufa nilipokuwa ninatoka tumboni?
Whi was not Y deed in the wombe? whi yede Y out of the wombe, and perischide not anoon?
12 Kwa nini pakawa na magoti ya kunipokea na matiti ili nipate kunyonyeshwa?
Whi was Y takun on knees? whi was Y suclid with teetis?
13 Kwa maana sasa ningekuwa nimepumzika kwa amani. Ningekuwa nimelala na kupumzika
For now Y slepynge schulde be stille, and schulde reste in my sleep,
14 pamoja na wafalme na washauri wa dunia, waliojijengea mahali ambapo sasa ni magofu,
with kyngis, and consuls of erthe, that bilden to hem soleyn places;
15 pamoja na watawala waliokuwa na dhahabu, waliozijaza nyumba zao kwa fedha.
ethir with prynces that han gold in possessioun, and fillen her housis with siluer;
16 Au kwa nini sikufichwa ardhini kama mtoto aliyezaliwa mfu, kama mtoto mchanga ambaye kamwe hakuuona mwanga?
ethir as a `thing hid not borun Y schulde not stonde, ethir whiche conseyued sien not liyt.
17 Huko waovu huacha kusumbua na huko waliochoka hupumzika.
There wickid men ceessiden of noise, and there men maad wery of strengthe restiden.
18 Wafungwa nao hufurahia utulivu wao, hawasikii tena sauti ya kukemea ya kiongozi wa watumwa.
And sum tyme boundun togidere with out disese thei herden not the voys of the wrongful axere.
19 Wadogo na wakubwa wamo humo, na mtumwa ameachiwa huru kutoka kwa bwana wake.
A litil man and greet man be there, and a seruaunt free fro his lord.
20 “Mbona nuru inawaangazia wale walio taabuni, na hao wenye uchungu kupewa uhai,
Whi is liyt youun to the wretche, and lijf to hem that ben in bitternesse of soule?
21 wale wanaotamani kifo ambacho hakiji, wale watafutao kufa zaidi ya kutafuta hazina iliyofichwa,
Whiche abiden deeth, and it cometh not;
22 ambao hujawa na furaha, na hushangilia wafikapo kaburini?
as men diggynge out tresour and ioien greetly, whanne thei han founde a sepulcre?
23 Kwa nini uhai hupewa mtu ambaye njia yake imefichika, ambaye Mungu amemzungushia boma?
Whi is liyt youun to a man, whos weie is hid, and God hath cumpassid hym with derknessis?
24 Kwa maana kulia kwangu kwa uchungu kwanijia badala ya chakula; kusononeka kwangu kunamwagika kama maji.
Bifore that Y ete, Y siyhe; and as of watir flowynge, so is my roryng.
25 Lile nililokuwa naliogopa limenijia; lile nililokuwa ninalihofia limenipata.
For the drede, which Y dredde, cam to me; and that, that Y schamede, bifelde.
26 Sina amani, wala utulivu; sina pumziko, bali taabu tu.”
Whether Y dissymilide not? whether Y was not stille? whether Y restide not? and indignacioun cometh on me.

< Ayubu 3 >