< Ayubu 3 >

1 Baada ya jambo hili, Ayubu akafumbua kinywa chake na kuilaani siku ya kuzaliwa kwake.
after so to open Job [obj] lip his and to lighten [obj] day his
2 Kisha akasema:
and to answer Job and to say
3 “Siku ya kuzaliwa kwangu na ipotelee mbali, nao usiku ule iliposemekana, ‘Mtoto wa kiume amezaliwa!’
to perish day to beget in/on/with him and [the] night to say to conceive great man
4 Siku ile na iwe giza; Mungu juu na asiiangalie; nayo nuru isiiangazie.
[the] day [the] he/she/it to be darkness not to seek him god from above and not to shine upon him light
5 Giza na kivuli kikuu kiikalie tena; wingu na likae juu yake; weusi na uifunike nuru yake.
to redeem: redeem him darkness and shadow to dwell upon him cloud to terrify him darkness day
6 Usiku ule na ushikwe na giza kuu; usihesabiwe katika siku za mwaka, wala usihesabiwe katika siku za mwezi wowote.
[the] night [the] he/she/it to take: take him darkness not to rejoice in/on/with day year in/on/with number month not to come (in): come
7 Usiku ule na uwe tasa; sauti ya furaha na isisikike ndani yake.
behold [the] night [the] he/she/it to be solitary not to come (in): come triumphing in/on/with him
8 Wale wazilaanio siku wailaani hiyo siku, wale walio tayari kumwamsha Lewiathani.
to curse him to curse day [the] ready to rouse Leviathan
9 Nyota zake za alfajiri na ziwe giza; nao ungojee mwanga bila mafanikio, wala usiuone mwonzi wa kwanza wa mapambazuko,
to darken star twilight his to await to/for light and nothing and not to see: see in/on/with eyelid dawn
10 kwa sababu huo usiku haukunifungia mlango wa tumbo la mama yangu, ili kuyaficha macho yangu kutokana na taabu.
for not to shut door belly: womb my and to hide trouble from eye my
11 “Kwa nini sikuangamia wakati wa kuzaliwa? Kwa nini sikufa nilipokuwa ninatoka tumboni?
to/for what? not from womb to die from belly: womb to come out: produce and to die
12 Kwa nini pakawa na magoti ya kunipokea na matiti ili nipate kunyonyeshwa?
why? to meet me knee and what? breast for to suckle
13 Kwa maana sasa ningekuwa nimepumzika kwa amani. Ningekuwa nimelala na kupumzika
for now to lie down: lay down and to quiet to sleep then to rest to/for me
14 pamoja na wafalme na washauri wa dunia, waliojijengea mahali ambapo sasa ni magofu,
with king and to advise land: country/planet [the] to build desolation to/for them
15 pamoja na watawala waliokuwa na dhahabu, waliozijaza nyumba zao kwa fedha.
or with ruler gold to/for them [the] to fill house: home their silver: money
16 Au kwa nini sikufichwa ardhini kama mtoto aliyezaliwa mfu, kama mtoto mchanga ambaye kamwe hakuuona mwanga?
or like/as miscarriage to hide not to be like/as infant not to see: see light
17 Huko waovu huacha kusumbua na huko waliochoka hupumzika.
there wicked to cease turmoil and there to rest weary strength
18 Wafungwa nao hufurahia utulivu wao, hawasikii tena sauti ya kukemea ya kiongozi wa watumwa.
unitedness prisoner to rest not to hear: hear voice to oppress
19 Wadogo na wakubwa wamo humo, na mtumwa ameachiwa huru kutoka kwa bwana wake.
small and great: large there he/she/it and servant/slave free from lord his
20 “Mbona nuru inawaangazia wale walio taabuni, na hao wenye uchungu kupewa uhai,
to/for what? to give: give to/for labour(er) light and life to/for bitter soul
21 wale wanaotamani kifo ambacho hakiji, wale watafutao kufa zaidi ya kutafuta hazina iliyofichwa,
[the] to wait to/for death and nothing he and to search him from treasure
22 ambao hujawa na furaha, na hushangilia wafikapo kaburini?
[the] glad to(wards) rejoicing to rejoice for to find grave
23 Kwa nini uhai hupewa mtu ambaye njia yake imefichika, ambaye Mungu amemzungushia boma?
to/for great man which way: journey his to hide and to fence god about/through/for him
24 Kwa maana kulia kwangu kwa uchungu kwanijia badala ya chakula; kusononeka kwangu kunamwagika kama maji.
for to/for face: before food: bread my sighing my to come (in): come and to pour like/as water roaring my
25 Lile nililokuwa naliogopa limenijia; lile nililokuwa ninalihofia limenipata.
for dread to dread and to come me and which to fear to come (in): come to/for me
26 Sina amani, wala utulivu; sina pumziko, bali taabu tu.”
not to prosper and not to quiet and not to rest and to come (in): come turmoil

< Ayubu 3 >