< Ayubu 3 >

1 Baada ya jambo hili, Ayubu akafumbua kinywa chake na kuilaani siku ya kuzaliwa kwake.
Napokon otvori Job usta i prokle dan svoj;
2 Kisha akasema:
poče svoju besjedu i reče:
3 “Siku ya kuzaliwa kwangu na ipotelee mbali, nao usiku ule iliposemekana, ‘Mtoto wa kiume amezaliwa!’
“O, ne bilo dana kad sam se rodio i noći što javi: 'Začeo se dječak!'
4 Siku ile na iwe giza; Mungu juu na asiiangalie; nayo nuru isiiangazie.
U crnu tminu dan taj nek se prometne! S visina se njega Bog ne spominjao, svjetlost sunčeva ne svijetlila mu više!
5 Giza na kivuli kikuu kiikalie tena; wingu na likae juu yake; weusi na uifunike nuru yake.
Mrak i sjena smrtna o nj se otimali, posvema ga tmina gusta prekrila, pomrčine dnevne stravom ga morile!
6 Usiku ule na ushikwe na giza kuu; usihesabiwe katika siku za mwaka, wala usihesabiwe katika siku za mwezi wowote.
O, da bi ga tama svega presvojila, nek' se ne dodaje danima godine, nek' ne ulazi u brojenje mjeseci!
7 Usiku ule na uwe tasa; sauti ya furaha na isisikike ndani yake.
A noć ona bila žalosna dovijeka, ne čulo se u njoj radosno klicanje!
8 Wale wazilaanio siku wailaani hiyo siku, wale walio tayari kumwamsha Lewiathani.
Prokleli je oni štono dan proklinju i Levijatana probudit' su kadri!
9 Nyota zake za alfajiri na ziwe giza; nao ungojee mwanga bila mafanikio, wala usiuone mwonzi wa kwanza wa mapambazuko,
Pomrčale zvijezde njezina svanuća, zaludu se ona vidjelu nadala, i zorinih vjeđa ne gledala nigda!
10 kwa sababu huo usiku haukunifungia mlango wa tumbo la mama yangu, ili kuyaficha macho yangu kutokana na taabu.
Što mi od utrobe ne zatvori vrata da sakrije muku od mojih očiju!
11 “Kwa nini sikuangamia wakati wa kuzaliwa? Kwa nini sikufa nilipokuwa ninatoka tumboni?
Što nisam mrtav od krila materina, što ne izdahnuh izlazeć' iz utrobe?
12 Kwa nini pakawa na magoti ya kunipokea na matiti ili nipate kunyonyeshwa?
Čemu su me dva koljena prihvatila i dojke dvije da me nejaka podoje?
13 Kwa maana sasa ningekuwa nimepumzika kwa amani. Ningekuwa nimelala na kupumzika
U miru bih vječnom počivao sada, spavao bih, pokoj svoj bih uživao
14 pamoja na wafalme na washauri wa dunia, waliojijengea mahali ambapo sasa ni magofu,
s kraljevima i savjetnicima zemlje koji su sebi pogradili grobnice,
15 pamoja na watawala waliokuwa na dhahabu, waliozijaza nyumba zao kwa fedha.
ili s knezovima, zlatom bogatima, što su kuće svoje srebrom napunili.
16 Au kwa nini sikufichwa ardhini kama mtoto aliyezaliwa mfu, kama mtoto mchanga ambaye kamwe hakuuona mwanga?
Ne bih bio - k'o nedonošče zakopano, k'o novorođenče što svjetla ne vidje.
17 Huko waovu huacha kusumbua na huko waliochoka hupumzika.
Zlikovci se više ne obijeste ondje, iznemogli tamo nalaze počinka.
18 Wafungwa nao hufurahia utulivu wao, hawasikii tena sauti ya kukemea ya kiongozi wa watumwa.
Sužnjeve na miru tamo ostavljaju: ne slušaju više poviku stražara.
19 Wadogo na wakubwa wamo humo, na mtumwa ameachiwa huru kutoka kwa bwana wake.
Malen ondje leži zajedno s velikim, rob je slobodan od gospodara svoga.
20 “Mbona nuru inawaangazia wale walio taabuni, na hao wenye uchungu kupewa uhai,
Čemu darovati svjetlo nesretniku i život ljudima zagorčene duše
21 wale wanaotamani kifo ambacho hakiji, wale watafutao kufa zaidi ya kutafuta hazina iliyofichwa,
koji smrt ištu, a ona ne dolazi, i kao za blagom za njome kopaju?
22 ambao hujawa na furaha, na hushangilia wafikapo kaburini?
Grobnom bi se humku oni radovali, klicali od sreće kad bi grob svoj našli.
23 Kwa nini uhai hupewa mtu ambaye njia yake imefichika, ambaye Mungu amemzungushia boma?
Što će to čovjeku kom je put sakriven, koga je Bog sa svih strana zapriječio?
24 Kwa maana kulia kwangu kwa uchungu kwanijia badala ya chakula; kusononeka kwangu kunamwagika kama maji.
Zato videć' hranu, uzdahnuti moram, k'o voda se moji razlijevaju krici.
25 Lile nililokuwa naliogopa limenijia; lile nililokuwa ninalihofia limenipata.
Obistinjuje se moje strahovanje, snalazi me, evo, čega god se bojah.
26 Sina amani, wala utulivu; sina pumziko, bali taabu tu.”
Pokoja ni mira meni više nema, u mukama mojim nikad mi počinka.”

< Ayubu 3 >