< Ayubu 29 >

1 Ayubu akaendelea na hoja yake, akasema:
Hiob ciągnął swoją przypowieść i mówił:
2 “Tazama jinsi ninavyoitamani miezi iliyopita, zile siku ambazo Mungu alikuwa akinilinda,
Obym był taki jak za dawnych miesięcy, za [tych] dni, w których Bóg mnie strzegł;
3 wakati taa yake iliniangazia kichwani changu, na kwa mwanga wake Mungu nikapita katikati ya giza!
Gdy jego pochodnia świeciła nad moją głową, a przy jego świetle przechodziłem w ciemności;
4 Natamani siku zile nilizokuwa katika ustawi wangu, wakati urafiki wa Mungu wa ndani ulipoibariki nyumba yangu,
Taki, jaki byłem za dni swojej młodości, gdy tajemnica Boga pozostawała nad moim namiotem;
5 wakati Mwenyezi alikuwa pamoja nami, nao watoto wangu walikuwa wamenizunguka,
Gdy Wszechmocny był jeszcze ze mną i otaczały mnie moje dzieci;
6 wakati njia yangu ilikuwa imenyweshewa siagi, nao mwamba ukanimiminia vijito vya mafuta ya zeituni.
Gdy moje ścieżki opływały w masło, a opoka wylewała mi źródła oliwy;
7 “Wakati nilipokwenda kwenye lango la mji na kuketi katika kiwanja,
Gdy wychodziłem do bramy przez miasto i na rynku przygotowałem sobie miejsce.
8 vijana waliniona wakakaa kando, nao wazee walioketi wakasimama;
Widząc mnie, młodzi ukrywali się, a starcy podnosili się i stali.
9 wakuu wakaacha kuzungumza na kuziba vinywa vyao kwa mikono yao;
Książęta przestawali mówić i kładli rękę na swoich ustach.
10 wenye vyeo wakanyamazishwa, nazo ndimi zao zikagandamana na makaakaa ya vinywa vyao.
Głos dostojników cichł, a ich język przylegał im do podniebienia.
11 Yeyote aliyenisikia alinena mema juu yangu, nao walioniona walinisifu,
Ucho, które mnie słyszało, błogosławiło mnie, a oko, które mnie widziało, dawało o mnie świadectwo;
12 kwa sababu nilimwokoa maskini aliyeomba msaada, naye yatima aliyekuwa hana wa kumsaidia.
Bo wybawiałem ubogiego, gdy wołał, sierotę oraz tego, który nie miał pomocnika.
13 Mtu aliyekuwa karibu kufa alinibariki, nami niliufanya moyo wa mjane kuimba.
Błogosławieństwo ginącego przychodziło do mnie, a serce wdowy radowałem.
14 Niliivaa haki kama vazi langu; uadilifu ulikuwa joho langu na kilemba changu.
Przyoblekłem się w sprawiedliwość i ona mnie okryła. Mój sąd był jak płaszcz i korona.
15 Nilikuwa macho ya kipofu na miguu kwa kiwete.
Byłem oczami dla ślepego, a nogami dla chromego.
16 Nilikuwa baba kwa mhitaji; nilimtetea mgeni.
Byłem ojcem ubogich, a sprawę, której nie znałem, badałem.
17 Niliyavunja meno makali ya waovu, na kuwapokonya wahanga kwenye meno yao.
I kruszyłem szczękę niegodziwca, a z jego zębów wydzierałem łup.
18 “Nikafikiri, ‘Nitafia katika nyumba yangu mwenyewe, nazo siku zangu zitakuwa nyingi kama chembechembe za mchanga.
Dlatego powiedziałem: Umrę w swoim gnieździe, rozmnożę [swoje] dni jak piasek.
19 Mizizi yangu itafika mpaka kwenye maji, nao umande utakaa juu ya matawi yangu usiku kucha.
Mój korzeń rozciągnął się przy wodach, a rosa trwała całą noc na moich gałązkach.
20 Utukufu wangu utabakia kuwa mpya ndani yangu, upinde wangu daima utaendelea kuwa mpya mkononi mwangu.’
Moja chwała odświeżała się we mnie, a mój łuk odnowił się w mojej ręce.
21 “Watu walinisikiliza kwa tumaini, wakingojea ushauri wangu kwa utulivu.
Słuchali mnie i oczekiwali, przyjmowali moją radę w milczeniu.
22 Baada ya mimi kuzungumza, hawakusema zaidi; maneno yangu yaliingia masikioni mwao kwa makini.
Po moich słowach już nie mówili, moja mowa kropiła na nich.
23 Waliningojea kama manyunyu ya mvua na kuyapokea maneno yangu kama ardhi inyonyavyo mvua ya vuli.
Oczekiwali mnie jak deszczu, otwierali swe usta jak na późny deszcz.
24 Walipokata tamaa niliwaonyesha uso wa furaha; nuru ya uso wangu ilikuwa ya thamani kwao.
[Jeśli] się śmiałem do nich, nie wierzyli, a światła mojej twarzy nie odrzucali.
25 Niliwachagulia njia na kukaa kama mkuu wao; niliishi kama mfalme katikati ya majeshi yake; nikawa kama yeye anayewafariji waombolezaji.
Wytyczałem im drogę, siadałem na czele i przybywałem jak król wśród wojska, jak [ten], który smutnych pociesza.

< Ayubu 29 >