< Ayubu 29 >

1 Ayubu akaendelea na hoja yake, akasema:
Et Job continuant, reprit son discours sentencieux, et dit:
2 “Tazama jinsi ninavyoitamani miezi iliyopita, zile siku ambazo Mungu alikuwa akinilinda,
Oh! qui me ferait être comme j'étais autrefois, comme j'étais en ces jours où Dieu me gardait.
3 wakati taa yake iliniangazia kichwani changu, na kwa mwanga wake Mungu nikapita katikati ya giza!
Quand il faisait luire sa lampe sur ma tête, et quand je marchais parmi les ténèbres, [éclairé] par sa lumière.
4 Natamani siku zile nilizokuwa katika ustawi wangu, wakati urafiki wa Mungu wa ndani ulipoibariki nyumba yangu,
Comme j'étais aux jours de mon automne, lorsque le secret de Dieu était dans ma tente.
5 wakati Mwenyezi alikuwa pamoja nami, nao watoto wangu walikuwa wamenizunguka,
Quand le Tout-puissant était encore avec moi, et mes gens autour de moi.
6 wakati njia yangu ilikuwa imenyweshewa siagi, nao mwamba ukanimiminia vijito vya mafuta ya zeituni.
Quand je lavais mes pas dans le beurre, et que des ruisseaux d'huile découlaient pour moi du rocher.
7 “Wakati nilipokwenda kwenye lango la mji na kuketi katika kiwanja,
Quand je sortais vers la porte passant par la ville, et que je me faisais préparer un siège dans la place,
8 vijana waliniona wakakaa kando, nao wazee walioketi wakasimama;
Les jeunes gens me voyant se cachaient, les vieillards se levaient, et se tenaient debout.
9 wakuu wakaacha kuzungumza na kuziba vinywa vyao kwa mikono yao;
Les principaux s'abstenaient de parler, et mettaient la main sur leur bouche.
10 wenye vyeo wakanyamazishwa, nazo ndimi zao zikagandamana na makaakaa ya vinywa vyao.
Les Conducteurs retenaient leur voix, et leur langue était attachée à leur palais.
11 Yeyote aliyenisikia alinena mema juu yangu, nao walioniona walinisifu,
L'oreille qui m'entendait, disait que j'étais bienheureux, et l'œil qui me voyait, déposait en ma faveur.
12 kwa sababu nilimwokoa maskini aliyeomba msaada, naye yatima aliyekuwa hana wa kumsaidia.
Car je délivrais l'affligé qui criait, et l'orphelin qui n'avait personne pour le secourir.
13 Mtu aliyekuwa karibu kufa alinibariki, nami niliufanya moyo wa mjane kuimba.
La bénédiction de celui qui s'en allait périr, venait sur moi, et je faisais que le cœur de la veuve chantait de joie.
14 Niliivaa haki kama vazi langu; uadilifu ulikuwa joho langu na kilemba changu.
J'étais revêtu de la justice, elle me servait de vêtement, et mon équité m'était comme un manteau, et [comme] une tiare.
15 Nilikuwa macho ya kipofu na miguu kwa kiwete.
Je servais d'œil à l'aveugle, et de pieds au boiteux.
16 Nilikuwa baba kwa mhitaji; nilimtetea mgeni.
J'étais le père des pauvres, et je m'informais diligemment de la cause qui ne m'était point connue.
17 Niliyavunja meno makali ya waovu, na kuwapokonya wahanga kwenye meno yao.
Je cassais les grosses dents de l'injuste, et je lui arrachais la proie d'entre ses dents.
18 “Nikafikiri, ‘Nitafia katika nyumba yangu mwenyewe, nazo siku zangu zitakuwa nyingi kama chembechembe za mchanga.
C'est pourquoi je disais: Je mourrai dans mon lit, et je multiplierai mes jours comme les grains de sable.
19 Mizizi yangu itafika mpaka kwenye maji, nao umande utakaa juu ya matawi yangu usiku kucha.
Ma racine était ouverte aux eaux, et la rosée demeurait toute la nuit sur mes branches.
20 Utukufu wangu utabakia kuwa mpya ndani yangu, upinde wangu daima utaendelea kuwa mpya mkononi mwangu.’
Ma gloire se renouvelait en moi, et mon arc était renforcé en ma main.
21 “Watu walinisikiliza kwa tumaini, wakingojea ushauri wangu kwa utulivu.
On m'écoutait, et on attendait [que j'eusse parlé]; et lorsque j'avais dit mon avis, on se tenait dans le silence.
22 Baada ya mimi kuzungumza, hawakusema zaidi; maneno yangu yaliingia masikioni mwao kwa makini.
Ils ne répliquaient rien après ce que je disais, et ma parole se répandait sur eux [comme une rosée].
23 Waliningojea kama manyunyu ya mvua na kuyapokea maneno yangu kama ardhi inyonyavyo mvua ya vuli.
Ils m'attendaient comme on attend la pluie; ils ouvraient leur bouche, comme après la pluie de la dernière saison.
24 Walipokata tamaa niliwaonyesha uso wa furaha; nuru ya uso wangu ilikuwa ya thamani kwao.
Riais-je avec eux? ils ne le croyaient point; et ils ne faisaient point disparaître la sérénité de mon visage.
25 Niliwachagulia njia na kukaa kama mkuu wao; niliishi kama mfalme katikati ya majeshi yake; nikawa kama yeye anayewafariji waombolezaji.
Voulais-je aller avec eux? j'étais assis au haut bout, j'étais entr'eux comme un Roi dans son armée, et comme un homme qui console les affligés.

< Ayubu 29 >