< Ayubu 29 >
1 Ayubu akaendelea na hoja yake, akasema:
Et Job, ajoutant à ce qui précède, dit:
2 “Tazama jinsi ninavyoitamani miezi iliyopita, zile siku ambazo Mungu alikuwa akinilinda,
Qui me rendra les jours d'autrefois, le temps où Dieu prenait de soin de me garder?
3 wakati taa yake iliniangazia kichwani changu, na kwa mwanga wake Mungu nikapita katikati ya giza!
Alors sa lampe brillait sur ma tête: alors avec sa lumière je ne craignais pas de marcher dans les ténèbres.
4 Natamani siku zile nilizokuwa katika ustawi wangu, wakati urafiki wa Mungu wa ndani ulipoibariki nyumba yangu,
Alors je foulais de mes pieds la voie; alors Dieu veillait sur ma maison.
5 wakati Mwenyezi alikuwa pamoja nami, nao watoto wangu walikuwa wamenizunguka,
Alors je m'asseyais à l'ombre de mes arbres, et mes enfants étaient autour de moi.
6 wakati njia yangu ilikuwa imenyweshewa siagi, nao mwamba ukanimiminia vijito vya mafuta ya zeituni.
Alors mes sentiers ruisselaient de beurre et mes collines de lait.
7 “Wakati nilipokwenda kwenye lango la mji na kuketi katika kiwanja,
Alors j'entrais dès l'aurore en la ville, et un siège m'était réservé sur les places.
8 vijana waliniona wakakaa kando, nao wazee walioketi wakasimama;
Les jeunes gens à mon aspect se voilaient; et les anciens restaient debout.
9 wakuu wakaacha kuzungumza na kuziba vinywa vyao kwa mikono yao;
Les forts cessaient de parler; ils se mettaient un doigt sur la bouche.
10 wenye vyeo wakanyamazishwa, nazo ndimi zao zikagandamana na makaakaa ya vinywa vyao.
Attentifs à mes discours, ils me déclaraient heureux, après quoi leur langue était collée à leur gosier.
11 Yeyote aliyenisikia alinena mema juu yangu, nao walioniona walinisifu,
L'oreille m'avait ouï et l'on me proclamait heureux; l'œil m'avait vu et l'on s'inclinait.
12 kwa sababu nilimwokoa maskini aliyeomba msaada, naye yatima aliyekuwa hana wa kumsaidia.
Car j'avais délivré le pauvre des mains du riche; j'avais protégé l'orphelin qui manquait d'appui.
13 Mtu aliyekuwa karibu kufa alinibariki, nami niliufanya moyo wa mjane kuimba.
La bénédiction de l'abandonné s'adressait à moi; la bouche de la veuve aussi me bénissait.
14 Niliivaa haki kama vazi langu; uadilifu ulikuwa joho langu na kilemba changu.
Je m'étais revêtu de justice; je m'étais enveloppé d'équité comme d'un manteau double.
15 Nilikuwa macho ya kipofu na miguu kwa kiwete.
J'étais l'œil de l'aveugle et le pied du boiteux.
16 Nilikuwa baba kwa mhitaji; nilimtetea mgeni.
J'étais le père des faibles; j'étudiais des causes que je ne connaissais pas.
17 Niliyavunja meno makali ya waovu, na kuwapokonya wahanga kwenye meno yao.
Aussi j'ai brisé les mâchoires de l'injuste; j'ai arraché de ses dents la proie qu'il avait saisie.
18 “Nikafikiri, ‘Nitafia katika nyumba yangu mwenyewe, nazo siku zangu zitakuwa nyingi kama chembechembe za mchanga.
Et j'ai dit: Mon âge se prolongera comme celui du palmier; ma vie sera de longue durée.
19 Mizizi yangu itafika mpaka kwenye maji, nao umande utakaa juu ya matawi yangu usiku kucha.
La racine se montrera hors de l'eau, et la rosée passera la nuit dans ma moisson.
20 Utukufu wangu utabakia kuwa mpya ndani yangu, upinde wangu daima utaendelea kuwa mpya mkononi mwangu.’
Ma gloire est pour moi chose vaine, et elle marche mon arc à la main.
21 “Watu walinisikiliza kwa tumaini, wakingojea ushauri wangu kwa utulivu.
A peine m'avait-on entendu que l'on s'attachait à moi; on gardait le silence en recueillant mes conseils.
22 Baada ya mimi kuzungumza, hawakusema zaidi; maneno yangu yaliingia masikioni mwao kwa makini.
Nul n'ajoutait à mes discours, et les hommes étaient pleins de joie que je leur avais parlé.
23 Waliningojea kama manyunyu ya mvua na kuyapokea maneno yangu kama ardhi inyonyavyo mvua ya vuli.
Comme la terre altérée reçoit la pluie, de même ils recevaient mes paroles.
24 Walipokata tamaa niliwaonyesha uso wa furaha; nuru ya uso wangu ilikuwa ya thamani kwao.
Lorsque je riais avec eux, ils n'y pouvaient croire, et l'éclat de mon visage n'en était pas amoindri.
25 Niliwachagulia njia na kukaa kama mkuu wao; niliishi kama mfalme katikati ya majeshi yake; nikawa kama yeye anayewafariji waombolezaji.
Je leur avais indiqué la voie, ils m'avaient institué leur chef, et ma demeure semblait celle d'un roi entouré de gardes ou d'un consolateur des affligés.