< Ayubu 29 >

1 Ayubu akaendelea na hoja yake, akasema:
Job, poursuivant l’exposé de son thème, dit:
2 “Tazama jinsi ninavyoitamani miezi iliyopita, zile siku ambazo Mungu alikuwa akinilinda,
Ah! Que ne suis-je tel que j’étais aux temps passés, aux jours où Dieu me protégeait;
3 wakati taa yake iliniangazia kichwani changu, na kwa mwanga wake Mungu nikapita katikati ya giza!
où son flambeau brillait sur ma tête, et où sa lumière me guidait dans les ténèbres;
4 Natamani siku zile nilizokuwa katika ustawi wangu, wakati urafiki wa Mungu wa ndani ulipoibariki nyumba yangu,
tel que j’étais aux jours de mon automne, alors que l’amitié de Dieu s’étendait sur ma demeure;
5 wakati Mwenyezi alikuwa pamoja nami, nao watoto wangu walikuwa wamenizunguka,
que le Tout-Puissant était encore avec moi et que j’étais entouré de mes jeunes gens;
6 wakati njia yangu ilikuwa imenyweshewa siagi, nao mwamba ukanimiminia vijito vya mafuta ya zeituni.
quand je baignais mes pieds dans la crème, et que le rocher ruisselait pour moi de flots d’huile!
7 “Wakati nilipokwenda kwenye lango la mji na kuketi katika kiwanja,
Quand je me dirigeais vers la Porte, au seuil de la cité, et fixais mon siège sur la place publique,
8 vijana waliniona wakakaa kando, nao wazee walioketi wakasimama;
les jeunes, en me voyant, se cachaient; les vieillards se levaient et se tenaient debout.
9 wakuu wakaacha kuzungumza na kuziba vinywa vyao kwa mikono yao;
Les grands retenaient leurs paroles et posaient la main sur la bouche.
10 wenye vyeo wakanyamazishwa, nazo ndimi zao zikagandamana na makaakaa ya vinywa vyao.
La voix des seigneurs expirait sur leurs lèvres, et leur langue se collait à leur palais;
11 Yeyote aliyenisikia alinena mema juu yangu, nao walioniona walinisifu,
car l’oreille qui m’entendait me proclamait heureux, et l’œil qui me voyait rendait témoignage pour moi.
12 kwa sababu nilimwokoa maskini aliyeomba msaada, naye yatima aliyekuwa hana wa kumsaidia.
C’Est que je sauvais le pauvre, criant au secours, et l’orphelin sans soutien.
13 Mtu aliyekuwa karibu kufa alinibariki, nami niliufanya moyo wa mjane kuimba.
La bénédiction du désespéré allait à moi, et je mettais de la joie au cœur de la veuve.
14 Niliivaa haki kama vazi langu; uadilifu ulikuwa joho langu na kilemba changu.
Je me revêtais d’équité comme d’une parure, mon esprit de justice était mon manteau et mon turban.
15 Nilikuwa macho ya kipofu na miguu kwa kiwete.
J’Étais les yeux de l’aveugle, j’étais les pieds du boiteux.
16 Nilikuwa baba kwa mhitaji; nilimtetea mgeni.
J’Étais un père pour les malheureux; la cause de l’inconnu, je l’étudiais à fond.
17 Niliyavunja meno makali ya waovu, na kuwapokonya wahanga kwenye meno yao.
Je brisais la mâchoire du malfaiteur, et j’arrachais la proie d’entre ses dents.
18 “Nikafikiri, ‘Nitafia katika nyumba yangu mwenyewe, nazo siku zangu zitakuwa nyingi kama chembechembe za mchanga.
Et je disais: "Je finirai avec mon nid; comme le phénix je vivrai de longs jours.
19 Mizizi yangu itafika mpaka kwenye maji, nao umande utakaa juu ya matawi yangu usiku kucha.
Ma racine sera en contact avec l’eau, la rosée se posera, la nuit, sur mon branchage.
20 Utukufu wangu utabakia kuwa mpya ndani yangu, upinde wangu daima utaendelea kuwa mpya mkononi mwangu.’
Ma gloire se renouvellera sans cesse, et mon arc se rajeunira dans ma main."
21 “Watu walinisikiliza kwa tumaini, wakingojea ushauri wangu kwa utulivu.
Ils m’écoutaient, pleins d’attente; ils faisaient silence pour entendre mon avis.
22 Baada ya mimi kuzungumza, hawakusema zaidi; maneno yangu yaliingia masikioni mwao kwa makini.
Quand j’avais fini de parler, ils ne répliquaient pas, et mes discours s’épandaient sur eux.
23 Waliningojea kama manyunyu ya mvua na kuyapokea maneno yangu kama ardhi inyonyavyo mvua ya vuli.
Ils m’attendaient comme la pluie; ils ouvraient la bouche comme pour l’ondée printanière.
24 Walipokata tamaa niliwaonyesha uso wa furaha; nuru ya uso wangu ilikuwa ya thamani kwao.
Je leur souriais et ils n’osaient y croire; jamais ils n’éteignaient le rayonnement de ma face.
25 Niliwachagulia njia na kukaa kama mkuu wao; niliishi kama mfalme katikati ya majeshi yake; nikawa kama yeye anayewafariji waombolezaji.
Volontiers j’allais vers eux, m’asseyant à leur tête, et j’étais comme un roi dans son armée, comme quelqu’un: qui console des affligés.

< Ayubu 29 >