< Ayubu 29 >
1 Ayubu akaendelea na hoja yake, akasema:
Job reprit encore son discours et dit:
2 “Tazama jinsi ninavyoitamani miezi iliyopita, zile siku ambazo Mungu alikuwa akinilinda,
Oh! Qui me rendra les mois d’autrefois, les jours où Dieu veillait à ma garde;
3 wakati taa yake iliniangazia kichwani changu, na kwa mwanga wake Mungu nikapita katikati ya giza!
quand sa lampe brillait sur ma tête, et que sa lumière me guidait dans les ténèbres!
4 Natamani siku zile nilizokuwa katika ustawi wangu, wakati urafiki wa Mungu wa ndani ulipoibariki nyumba yangu,
Tel que j’étais aux jours de mon âge mûr, quand Dieu me visitait familièrement dans ma tente,
5 wakati Mwenyezi alikuwa pamoja nami, nao watoto wangu walikuwa wamenizunguka,
quand le Tout-Puissant était encore avec moi, et que mes fils m’entouraient;
6 wakati njia yangu ilikuwa imenyweshewa siagi, nao mwamba ukanimiminia vijito vya mafuta ya zeituni.
quand je lavais mes pieds dans le lait, et que le rocher me versait des flots d’huile!
7 “Wakati nilipokwenda kwenye lango la mji na kuketi katika kiwanja,
Lorsque je sortais pour me rendre à la porte de la ville, et que j’établissais mon siège sur la place publique,
8 vijana waliniona wakakaa kando, nao wazee walioketi wakasimama;
en me voyant, les jeunes gens se cachaient, les vieillards se levaient et se tenaient debout.
9 wakuu wakaacha kuzungumza na kuziba vinywa vyao kwa mikono yao;
Les princes retenaient leurs paroles, et mettaient leur main sur la bouche.
10 wenye vyeo wakanyamazishwa, nazo ndimi zao zikagandamana na makaakaa ya vinywa vyao.
La voix des chefs restait muette, leur langue s’attachait à leur palais.
11 Yeyote aliyenisikia alinena mema juu yangu, nao walioniona walinisifu,
L’oreille qui m’entendait me proclamait heureux, l’œil qui me voyait me rendait témoignage.
12 kwa sababu nilimwokoa maskini aliyeomba msaada, naye yatima aliyekuwa hana wa kumsaidia.
Car je sauvais le pauvre qui implorait du secours, et l’orphelin dénué de tout appui.
13 Mtu aliyekuwa karibu kufa alinibariki, nami niliufanya moyo wa mjane kuimba.
La bénédiction de celui qui allait périr venait sur moi, je remplissais de joie le cœur de la veuve.
14 Niliivaa haki kama vazi langu; uadilifu ulikuwa joho langu na kilemba changu.
Je me revêtais de la justice comme d’un vêtement, mon équité était mon manteau et mon turban.
15 Nilikuwa macho ya kipofu na miguu kwa kiwete.
J’étais l’œil de l’aveugle, et le pied du boiteux.
16 Nilikuwa baba kwa mhitaji; nilimtetea mgeni.
J’étais le père des pauvres, j’examinais avec soin la cause de l’inconnu.
17 Niliyavunja meno makali ya waovu, na kuwapokonya wahanga kwenye meno yao.
Je brisais la mâchoire de l’injuste, et j’arrachais sa proie d’entre les dents.
18 “Nikafikiri, ‘Nitafia katika nyumba yangu mwenyewe, nazo siku zangu zitakuwa nyingi kama chembechembe za mchanga.
Je disais: « Je mourrai dans mon nid, j’aurai des jours nombreux comme le sable.
19 Mizizi yangu itafika mpaka kwenye maji, nao umande utakaa juu ya matawi yangu usiku kucha.
Mes racines s’étendent vers les eaux, la rosée passe la nuit dans mon feuillage.
20 Utukufu wangu utabakia kuwa mpya ndani yangu, upinde wangu daima utaendelea kuwa mpya mkononi mwangu.’
Ma gloire reverdira sans cesse, et mon arc reprendra sa vigueur dans ma main. »
21 “Watu walinisikiliza kwa tumaini, wakingojea ushauri wangu kwa utulivu.
On m’écoutait et l’on attendait, on recueillait en silence mon avis.
22 Baada ya mimi kuzungumza, hawakusema zaidi; maneno yangu yaliingia masikioni mwao kwa makini.
Après que j’avais parlé, personne n’ajoutait rien; ma parole coulait sur eux comme la rosée.
23 Waliningojea kama manyunyu ya mvua na kuyapokea maneno yangu kama ardhi inyonyavyo mvua ya vuli.
Ils m’attendaient comme on attend la pluie; ils ouvraient la bouche comme aux ondées du printemps.
24 Walipokata tamaa niliwaonyesha uso wa furaha; nuru ya uso wangu ilikuwa ya thamani kwao.
Si je leur souriais, ils ne pouvaient le croire; ils recueillaient avidement ce signe de faveur.
25 Niliwachagulia njia na kukaa kama mkuu wao; niliishi kama mfalme katikati ya majeshi yake; nikawa kama yeye anayewafariji waombolezaji.
Quand j’allais vers eux, j’avais la première place, je siégeais comme un roi entouré de sa troupe, comme un consolateur au milieu des affligés.