< Ayubu 29 >
1 Ayubu akaendelea na hoja yake, akasema:
Also Joob addide, takynge his parable, and seide,
2 “Tazama jinsi ninavyoitamani miezi iliyopita, zile siku ambazo Mungu alikuwa akinilinda,
Who yyueth to me, that I be bisidis the elde monethis, bi the daies in whiche God kepte me?
3 wakati taa yake iliniangazia kichwani changu, na kwa mwanga wake Mungu nikapita katikati ya giza!
Whanne his lanterne schynede on myn heed, and Y yede in derknessis at his liyt.
4 Natamani siku zile nilizokuwa katika ustawi wangu, wakati urafiki wa Mungu wa ndani ulipoibariki nyumba yangu,
As Y was in the daies of my yongthe, whanne in priuete God was in my tabernacle.
5 wakati Mwenyezi alikuwa pamoja nami, nao watoto wangu walikuwa wamenizunguka,
Whanne Almyyti God was with me, and my children weren in my cumpas;
6 wakati njia yangu ilikuwa imenyweshewa siagi, nao mwamba ukanimiminia vijito vya mafuta ya zeituni.
whanne Y waischide my feet in botere, and the stoon schedde out to me the stremes of oile;
7 “Wakati nilipokwenda kwenye lango la mji na kuketi katika kiwanja,
whanne Y yede forth to the yate of the citee, and in the street thei maden redi a chaier to me.
8 vijana waliniona wakakaa kando, nao wazee walioketi wakasimama;
Yonge men, `that is, wantoun, sien me, and weren hid, and elde men risynge vp stoden;
9 wakuu wakaacha kuzungumza na kuziba vinywa vyao kwa mikono yao;
princes ceessiden to speke, and puttiden the fyngur on her mouth;
10 wenye vyeo wakanyamazishwa, nazo ndimi zao zikagandamana na makaakaa ya vinywa vyao.
duykis refreyneden her vois, and her tunge cleuyde to her throte.
11 Yeyote aliyenisikia alinena mema juu yangu, nao walioniona walinisifu,
An eere herynge blesside me, and an iye seynge yeldide witnessyng to me;
12 kwa sababu nilimwokoa maskini aliyeomba msaada, naye yatima aliyekuwa hana wa kumsaidia.
for Y hadde delyueride a pore man criynge, and a fadirles child, that hadde noon helpere.
13 Mtu aliyekuwa karibu kufa alinibariki, nami niliufanya moyo wa mjane kuimba.
The blessyng of a man `to perische cam on me, and Y coumfortide the herte of a widewe.
14 Niliivaa haki kama vazi langu; uadilifu ulikuwa joho langu na kilemba changu.
Y was clothid with riytfulnesse; and Y clothide me as with a cloth, and with my `doom a diademe.
15 Nilikuwa macho ya kipofu na miguu kwa kiwete.
Y was iye `to a blynde man, and foot to a crokyd man.
16 Nilikuwa baba kwa mhitaji; nilimtetea mgeni.
Y was a fadir of pore men; and Y enqueride most diligentli the cause, which Y knew not.
17 Niliyavunja meno makali ya waovu, na kuwapokonya wahanga kwenye meno yao.
Y al tobrak the grete teeth of the wickid man, and Y took awei prey fro hise teeth.
18 “Nikafikiri, ‘Nitafia katika nyumba yangu mwenyewe, nazo siku zangu zitakuwa nyingi kama chembechembe za mchanga.
And Y seide, Y schal die in my nest; and as a palm tre Y schal multiplie daies.
19 Mizizi yangu itafika mpaka kwenye maji, nao umande utakaa juu ya matawi yangu usiku kucha.
My roote is openyde bisidis watris, and deew schal dwelle in my repyng.
20 Utukufu wangu utabakia kuwa mpya ndani yangu, upinde wangu daima utaendelea kuwa mpya mkononi mwangu.’
My glorie schal euere be renulid, and my bouwe schal be astorid in myn hond.
21 “Watu walinisikiliza kwa tumaini, wakingojea ushauri wangu kwa utulivu.
Thei, that herden me, abiden my sentence; and thei weren ententif, and weren stille to my counsel.
22 Baada ya mimi kuzungumza, hawakusema zaidi; maneno yangu yaliingia masikioni mwao kwa makini.
Thei dursten no thing adde to my wordis; and my speche droppide on hem.
23 Waliningojea kama manyunyu ya mvua na kuyapokea maneno yangu kama ardhi inyonyavyo mvua ya vuli.
Thei abididen me as reyn; and thei openyden her mouth as to the softe reyn `comynge late.
24 Walipokata tamaa niliwaonyesha uso wa furaha; nuru ya uso wangu ilikuwa ya thamani kwao.
If ony tyme Y leiyide to hem, thei bileueden not; and the liyt of my cheer felde not doun in to erthe.
25 Niliwachagulia njia na kukaa kama mkuu wao; niliishi kama mfalme katikati ya majeshi yake; nikawa kama yeye anayewafariji waombolezaji.
If Y wolde go to hem, Y sat the firste; and whanne Y sat as kyng, while the oost stood aboute, netheles Y was comfortour of hem that morenyden.