< Ayubu 28 >

1 “Kuna machimbo ya fedha, na mahali dhahabu isafishwapo.
Gümüş maden ocağından elde edilir, Altını arıtmak için de bir yer vardır.
2 Chuma hupatikana ardhini, nayo shaba huyeyushwa kutoka mawe ya madini.
Demir topraktan çıkarılır, Bakırsa taştan.
3 Mwanadamu hukomesha giza; huyatafuta hadi sehemu iliyo mbali, kwa ajili ya kuchimbua mawe yenye madini katika giza jeusi sana.
İnsan karanlığa son verir, Koyu karanlığın, ölüm gölgesinin taşlarını Son sınırına kadar araştırır.
4 Huchimba shimo jembamba mbali na makao ya watu, mahali paliposahaulika na nyayo za wanadamu; mbali na wanadamu huningʼinia na kupembea kwa kamba.
Maden kuyusunu insanların oturduğu yerden uzakta açar, İnsan ayağının unuttuğu yerlerde, Herkesten uzak iplere sarılıp sallanır.
5 Ardhi, ambako chakula hutoka, chini hugeuzwa kwa moto;
Ekmek topraktan çıkar, Toprağın altı ise yanmış, altüst olmuştur.
6 yakuti samawi hutoka katika miamba yake, nalo vumbi lake lina vipande vya dhahabu.
Kayalarından laciverttaşı çıkar, Yüzeyi altın tozunu andırır.
7 Hakuna ndege awindaye aijuaye njia ile iliyofichika, wala hakuna jicho la mwewe lililoiona.
Yırtıcı kuş yolu bilmez, Doğanın gözü onu görmemiştir.
8 Wanyama wa porini wanaotamba hawajawahi kupakanyaga, wala simba azungukaye huko.
Güçlü hayvanlar oraya ayak basmamış, Aslan oradan geçmemiştir.
9 Mikono ya mwanadamu hushambulia miamba migumu sana, na kuiacha wazi mizizi ya milima.
Madenci elini çakmak taşına uzatır, Dağları kökünden altüst eder.
10 Hutoboa shimo refu la kupenya chini kwa chini kwenye miamba; macho yake huona hazina zake zote.
Kayaların içinden tüneller açar, Gözleri değerli ne varsa görür.
11 Hutafuta vyanzo vya mito na kuvileta vitu vilivyofichika katika nuru.
Irmakların kaynağını tıkar, Gizli olanı ışığa çıkarır.
12 “Lakini hekima inaweza kupatikana wapi? Ufahamu unakaa wapi?
Ama bilgelik nerede bulunur? Aklın yeri neresi?
13 Mwanadamu hatambui thamani yake; haiwezi kupatikana katika nchi ya walio hai.
İnsan onun değerini bilmez, Yaşayanlar diyarında ona rastlanmaz.
14 Kilindi husema, ‘Haiko ndani yangu’; bahari nayo husema, ‘Haiko pamoja nami.’
Engin, “Bende değil” der, Deniz, “Yanımda değil.”
15 Haiwezi kununuliwa kwa dhahabu safi kuliko zote, wala thamani yake haiwezi kupimwa kwa fedha.
Onun bedeli saf altınla ödenmez, Değeri gümüşle ölçülmez.
16 Haiwezi kununuliwa kwa dhahabu ya Ofiri, kwa shohamu ya thamani kubwa au yakuti samawi ya thamani kubwa.
Ona Ofir altınıyla, değerli oniksle, Laciverttaşıyla değer biçilmez.
17 Dhahabu wala mawe maangavu haviwezi kulinganishwa nayo, wala haiwezi hubadilishwa na vito vya dhahabu.
Ne altın ne cam onunla karşılaştırılabilir, Saf altın kaplara değişilmez.
18 Marijani na yaspi hazistahili kutajwa; thamani ya hekima ni zaidi ya akiki nyekundu.
Yanında mercanla billurun sözü edilmez, Bilgeliğin değeri mücevherden üstündür.
19 Yakuti manjano ipatikanayo Kushi haiwezi kulinganishwa nayo, wala haiwezi kununuliwa kwa dhahabu safi.
Kûş topazı onunla denk sayılmaz, Saf altınla ona değer biçilmez.
20 “Ni wapi basi hekima itokako? Ufahamu hukaa wapi?
Öyleyse bilgelik nereden geliyor? Aklın yeri neresi?
21 Imefichika machoni pa kila kitu kilicho hai, imesitiriwa hata kwa ndege wa angani.
O bütün canlıların gözünden uzaktır, Gökte uçan kuşlardan bile saklıdır.
22 Uharibifu na Mauti husema, ‘Ni uvumi wake tu uliotufikia masikioni mwetu.’
Yıkım'la Ölüm: “Kulaklarımız ancak fısıltısını duydu” der.
23 Mungu anaifahamu njia ya kuiendea hekima na ndiye peke yake anayefahamu inakokaa,
Onun yolunu Tanrı anlar, Yerini bilen O'dur.
24 kwa maana yeye huitazama miisho ya dunia na huona kila kitu chini ya mbingu.
Çünkü O yeryüzünün uçlarına kadar bakar, Göklerin altındaki her şeyi görür.
25 Alipofanyiza nguvu za upepo na kuyapima maji,
Rüzgara güç verdiği, Suları ölçtüğü,
26 alipofanya maagizo kwa ajili ya mvua na njia kwa ajili ya umeme wa radi,
Yağmura kural koyduğu, Yıldırıma yol açtığı zaman,
27 ndipo alipoitazama hekima na kuikadiria thamani yake, akaithibitisha na kuihakikisha.
Bilgeliği görüp değerini biçti, Onu onaylayıp araştırdı.
28 Naye Mungu akamwambia mwanadamu, ‘Kumcha Bwana: hiyo ndiyo hekima, nako kujitenga na uovu ndio ufahamu.’”
İnsana, “İşte Rab korkusu, bilgelik budur” dedi, “Kötülükten kaçınmak akıllılıktır.”

< Ayubu 28 >