< Ayubu 28 >

1 “Kuna machimbo ya fedha, na mahali dhahabu isafishwapo.
CIERTAMENTE la plata tiene sus veneros, y el oro lugar [donde] se forma.
2 Chuma hupatikana ardhini, nayo shaba huyeyushwa kutoka mawe ya madini.
El hierro se saca del polvo, y de la piedra es fundido el metal.
3 Mwanadamu hukomesha giza; huyatafuta hadi sehemu iliyo mbali, kwa ajili ya kuchimbua mawe yenye madini katika giza jeusi sana.
A las tinieblas puso término, y examina todo á la perfección, las piedras [que hay] en la oscuridad y en la sombra de muerte.
4 Huchimba shimo jembamba mbali na makao ya watu, mahali paliposahaulika na nyayo za wanadamu; mbali na wanadamu huningʼinia na kupembea kwa kamba.
Brota el torrente de junto al morador, [aguas] que el pie había olvidado: sécanse luego, vanse del hombre.
5 Ardhi, ambako chakula hutoka, chini hugeuzwa kwa moto;
De la tierra nace el pan, y debajo de ella estará como convertida en fuego.
6 yakuti samawi hutoka katika miamba yake, nalo vumbi lake lina vipande vya dhahabu.
Lugar hay cuyas piedras son zafiro, y sus polvos de oro.
7 Hakuna ndege awindaye aijuaye njia ile iliyofichika, wala hakuna jicho la mwewe lililoiona.
Senda que nunca la conoció ave, ni ojo de buitre la vió:
8 Wanyama wa porini wanaotamba hawajawahi kupakanyaga, wala simba azungukaye huko.
Nunca la pisaron animales fieros, ni león pasó por ella.
9 Mikono ya mwanadamu hushambulia miamba migumu sana, na kuiacha wazi mizizi ya milima.
En el pedernal puso su mano, y trastornó los montes de raíz.
10 Hutoboa shimo refu la kupenya chini kwa chini kwenye miamba; macho yake huona hazina zake zote.
De los peñascos cortó ríos, y sus ojos vieron todo lo preciado.
11 Hutafuta vyanzo vya mito na kuvileta vitu vilivyofichika katika nuru.
Detuvo los ríos en su nacimiento, é hizo salir á luz lo escondido.
12 “Lakini hekima inaweza kupatikana wapi? Ufahamu unakaa wapi?
Empero ¿dónde se hallará la sabiduría? ¿y dónde está el lugar de la prudencia?
13 Mwanadamu hatambui thamani yake; haiwezi kupatikana katika nchi ya walio hai.
No conoce su valor el hombre, ni se halla en la tierra de los vivientes.
14 Kilindi husema, ‘Haiko ndani yangu’; bahari nayo husema, ‘Haiko pamoja nami.’
El abismo dice: No está en mí: y la mar dijo: Ni conmigo.
15 Haiwezi kununuliwa kwa dhahabu safi kuliko zote, wala thamani yake haiwezi kupimwa kwa fedha.
No se dará por oro, ni su precio será á peso de plata.
16 Haiwezi kununuliwa kwa dhahabu ya Ofiri, kwa shohamu ya thamani kubwa au yakuti samawi ya thamani kubwa.
No puede ser apreciada con oro de Ophir, ni con onique precioso, ni con zafiro.
17 Dhahabu wala mawe maangavu haviwezi kulinganishwa nayo, wala haiwezi hubadilishwa na vito vya dhahabu.
El oro no se le igualará, ni el diamante; ni se trocará por vaso de oro fino.
18 Marijani na yaspi hazistahili kutajwa; thamani ya hekima ni zaidi ya akiki nyekundu.
De coral ni de perlas no se hará mención: la sabiduría es mejor que piedras preciosas.
19 Yakuti manjano ipatikanayo Kushi haiwezi kulinganishwa nayo, wala haiwezi kununuliwa kwa dhahabu safi.
No se igualará con ella esmeralda de Ethiopía; no se podrá apreciar con oro fino.
20 “Ni wapi basi hekima itokako? Ufahamu hukaa wapi?
¿De dónde pues vendrá la sabiduría? ¿y dónde está el lugar de la inteligencia?
21 Imefichika machoni pa kila kitu kilicho hai, imesitiriwa hata kwa ndege wa angani.
Porque encubierta está á los ojos de todo viviente, y á toda ave del cielo es oculta.
22 Uharibifu na Mauti husema, ‘Ni uvumi wake tu uliotufikia masikioni mwetu.’
El infierno y la muerte dijeron: Su fama hemos oído con nuestros oídos. (questioned)
23 Mungu anaifahamu njia ya kuiendea hekima na ndiye peke yake anayefahamu inakokaa,
Dios entiende el camino de ella, y él conoce su lugar.
24 kwa maana yeye huitazama miisho ya dunia na huona kila kitu chini ya mbingu.
Porque él mira hasta los fines de la tierra, y ve debajo de todo el cielo.
25 Alipofanyiza nguvu za upepo na kuyapima maji,
Al dar peso al viento, y poner las aguas por medida;
26 alipofanya maagizo kwa ajili ya mvua na njia kwa ajili ya umeme wa radi,
Cuando él hizo ley á la lluvia, y camino al relámpago de los truenos;
27 ndipo alipoitazama hekima na kuikadiria thamani yake, akaithibitisha na kuihakikisha.
Entonces la veía él, y la manifestaba; preparóla y descubrióla también.
28 Naye Mungu akamwambia mwanadamu, ‘Kumcha Bwana: hiyo ndiyo hekima, nako kujitenga na uovu ndio ufahamu.’”
Y dijo al hombre: He aquí que el temor del Señor es la sabiduría, y el apartarse del mal la inteligencia.

< Ayubu 28 >