< Ayubu 28 >

1 “Kuna machimbo ya fedha, na mahali dhahabu isafishwapo.
은은 나는 광이 있고 연단하는 금은 나는 곳이 있으며
2 Chuma hupatikana ardhini, nayo shaba huyeyushwa kutoka mawe ya madini.
철은 흙에서 취하고 동은 돌에서 녹여 얻느니라
3 Mwanadamu hukomesha giza; huyatafuta hadi sehemu iliyo mbali, kwa ajili ya kuchimbua mawe yenye madini katika giza jeusi sana.
사람이 흑암을 파하고 끝까지 궁구하여 음예와 유암 중의 광석을 구하되
4 Huchimba shimo jembamba mbali na makao ya watu, mahali paliposahaulika na nyayo za wanadamu; mbali na wanadamu huningʼinia na kupembea kwa kamba.
사람 사는 곳에서 멀리 떠나 구멍을 깊이 뚫고 발이 땅에 닿지 않게 달려 내리니 멀리 사람과 격절되고 흔들흔들 하느니라
5 Ardhi, ambako chakula hutoka, chini hugeuzwa kwa moto;
지면은 식물을 내나 지하는 불로 뒤집는 것같고
6 yakuti samawi hutoka katika miamba yake, nalo vumbi lake lina vipande vya dhahabu.
그 돌 가운데에는 남보석이 있고 사금도 있으며
7 Hakuna ndege awindaye aijuaye njia ile iliyofichika, wala hakuna jicho la mwewe lililoiona.
그 길은 솔개도 알지 못하고 매의 눈도 보지 못하며
8 Wanyama wa porini wanaotamba hawajawahi kupakanyaga, wala simba azungukaye huko.
위엄스러운 짐승도 밟지 못하였고 사나운 사자도 그리로 지나가지 못하였느니라
9 Mikono ya mwanadamu hushambulia miamba migumu sana, na kuiacha wazi mizizi ya milima.
사람이 굳은 바위에 손을 대고 산을 뿌리까지 무너뜨리며
10 Hutoboa shimo refu la kupenya chini kwa chini kwenye miamba; macho yake huona hazina zake zote.
돌 가운데로 도랑을 파서 각종 보물을 눈으로 발견하고
11 Hutafuta vyanzo vya mito na kuvileta vitu vilivyofichika katika nuru.
시냇물을 막아 스미지 않게 하고 감취었던 것을 밝은 데로 내느니라
12 “Lakini hekima inaweza kupatikana wapi? Ufahamu unakaa wapi?
그러나 지혜는 어디서 얻으며 명철의 곳은 어디인고
13 Mwanadamu hatambui thamani yake; haiwezi kupatikana katika nchi ya walio hai.
그 값을 사람이 알지 못하나니 사람 사는 땅에서 찾을 수 없구나
14 Kilindi husema, ‘Haiko ndani yangu’; bahari nayo husema, ‘Haiko pamoja nami.’
깊은 물이 이르기를 내 속에 있지 아니하다 하며 바다가 이르기를 나와 함께 있지 아니하다 하느니라
15 Haiwezi kununuliwa kwa dhahabu safi kuliko zote, wala thamani yake haiwezi kupimwa kwa fedha.
정금으로도 바꿀 수 없고 은을 달아도 그 값을 당치 못하리니
16 Haiwezi kununuliwa kwa dhahabu ya Ofiri, kwa shohamu ya thamani kubwa au yakuti samawi ya thamani kubwa.
오빌의 금이나 귀한 수마노나 남보석으로도 그 값을 당치 못하겠고
17 Dhahabu wala mawe maangavu haviwezi kulinganishwa nayo, wala haiwezi hubadilishwa na vito vya dhahabu.
황금이나 유리라도 비교할 수 없고 정금 장식으로도 바꿀 수 없으며
18 Marijani na yaspi hazistahili kutajwa; thamani ya hekima ni zaidi ya akiki nyekundu.
산호나 수정으로도 말할 수 없나니 지혜의 값은 홍보석보다 귀하구나
19 Yakuti manjano ipatikanayo Kushi haiwezi kulinganishwa nayo, wala haiwezi kununuliwa kwa dhahabu safi.
구스의 황옥으로도 비교할 수 없고 순금으로도 그 값을 측량하지못하리니
20 “Ni wapi basi hekima itokako? Ufahamu hukaa wapi?
그런즉 지혜는 어디서 오며 명철의 곳은 어디인고
21 Imefichika machoni pa kila kitu kilicho hai, imesitiriwa hata kwa ndege wa angani.
모든 생물의 눈에 숨겨졌고 공중의 새에게 가리워졌으며
22 Uharibifu na Mauti husema, ‘Ni uvumi wake tu uliotufikia masikioni mwetu.’
멸망과 사망도 이르기를 우리가 귀로 그 소문은 들었다 하느니라
23 Mungu anaifahamu njia ya kuiendea hekima na ndiye peke yake anayefahamu inakokaa,
하나님이 그 길을 깨달으시며 있는 곳을 아시나니
24 kwa maana yeye huitazama miisho ya dunia na huona kila kitu chini ya mbingu.
이는 그가 땅 끝까지 감찰하시며 온 천하를 두루 보시며
25 Alipofanyiza nguvu za upepo na kuyapima maji,
바람의 경중을 정하시며 물을 되어 그 분량을 정하시며
26 alipofanya maagizo kwa ajili ya mvua na njia kwa ajili ya umeme wa radi,
비를 위하여 명령하시고 우뢰의 번개를 위하여 길을 정하셨음이라
27 ndipo alipoitazama hekima na kuikadiria thamani yake, akaithibitisha na kuihakikisha.
그 때에 지혜를 보시고 선포하시며 굳게 세우시며 궁구하셨고
28 Naye Mungu akamwambia mwanadamu, ‘Kumcha Bwana: hiyo ndiyo hekima, nako kujitenga na uovu ndio ufahamu.’”
또 사람에게 이르시기를 주를 경외함이 곧 지혜요 악을 떠남이 명철이라 하셨느니라

< Ayubu 28 >