< Ayubu 28 >
1 “Kuna machimbo ya fedha, na mahali dhahabu isafishwapo.
Ha una miniera l’argento, e l’oro un luogo dove lo si affina.
2 Chuma hupatikana ardhini, nayo shaba huyeyushwa kutoka mawe ya madini.
Il ferro si cava dal suolo, e la pietra fusa dà il rame.
3 Mwanadamu hukomesha giza; huyatafuta hadi sehemu iliyo mbali, kwa ajili ya kuchimbua mawe yenye madini katika giza jeusi sana.
L’uomo ha posto fine alle tenebre, egli esplora i più profondi recessi, per trovar le pietre che son nel buio, nell’ombra di morte.
4 Huchimba shimo jembamba mbali na makao ya watu, mahali paliposahaulika na nyayo za wanadamu; mbali na wanadamu huningʼinia na kupembea kwa kamba.
Scava un pozzo lontan dall’abitato; il piede più non serve a quei che vi lavorano; son sospesi, oscillano lungi dai mortali.
5 Ardhi, ambako chakula hutoka, chini hugeuzwa kwa moto;
Dalla terra esce il pane, ma, nelle sue viscere, è sconvolta come dal fuoco.
6 yakuti samawi hutoka katika miamba yake, nalo vumbi lake lina vipande vya dhahabu.
Le sue rocce son la dimora dello zaffiro, e vi si trova della polvere d’oro.
7 Hakuna ndege awindaye aijuaye njia ile iliyofichika, wala hakuna jicho la mwewe lililoiona.
L’uccello di rapina non conosce il sentiero che vi mena, né l’ha mai scorto l’occhio del falco.
8 Wanyama wa porini wanaotamba hawajawahi kupakanyaga, wala simba azungukaye huko.
Le fiere superbe non vi hanno messo piede, e il leone non v’è passato mai.
9 Mikono ya mwanadamu hushambulia miamba migumu sana, na kuiacha wazi mizizi ya milima.
L’uomo stende la mano sul granito, rovescia dalle radici le montagne.
10 Hutoboa shimo refu la kupenya chini kwa chini kwenye miamba; macho yake huona hazina zake zote.
Pratica trafori per entro le rocce, e l’occhio suo scorge quanto v’è di prezioso.
11 Hutafuta vyanzo vya mito na kuvileta vitu vilivyofichika katika nuru.
Infrena le acque perché non gemano, e le cose nascoste trae fuori alla luce.
12 “Lakini hekima inaweza kupatikana wapi? Ufahamu unakaa wapi?
Ma la Sapienza, dove trovarla? E dov’è il luogo della Intelligenza?
13 Mwanadamu hatambui thamani yake; haiwezi kupatikana katika nchi ya walio hai.
L’uomo non ne sa la via, non la si trova sulla terra de’ viventi.
14 Kilindi husema, ‘Haiko ndani yangu’; bahari nayo husema, ‘Haiko pamoja nami.’
L’abisso dice: “Non è in me”; il mare dice: “Non sta da me”.
15 Haiwezi kununuliwa kwa dhahabu safi kuliko zote, wala thamani yake haiwezi kupimwa kwa fedha.
Non la si ottiene in cambio d’oro, né la si compra a peso d’argento.
16 Haiwezi kununuliwa kwa dhahabu ya Ofiri, kwa shohamu ya thamani kubwa au yakuti samawi ya thamani kubwa.
Non la si acquista con l’oro di Ofir, con l’onice prezioso o con lo zaffiro.
17 Dhahabu wala mawe maangavu haviwezi kulinganishwa nayo, wala haiwezi hubadilishwa na vito vya dhahabu.
L’oro ed il vetro non reggono al suo confronto, non la si dà in cambio di vasi d’oro fino.
18 Marijani na yaspi hazistahili kutajwa; thamani ya hekima ni zaidi ya akiki nyekundu.
Non si parli di corallo, di cristallo; la Sapienza val più delle perle.
19 Yakuti manjano ipatikanayo Kushi haiwezi kulinganishwa nayo, wala haiwezi kununuliwa kwa dhahabu safi.
Il topazio d’Etiopia non può starle a fronte, l’oro puro non ne bilancia il valore.
20 “Ni wapi basi hekima itokako? Ufahamu hukaa wapi?
Donde vien dunque la Sapienza? E dov’è il luogo della Intelligenza?
21 Imefichika machoni pa kila kitu kilicho hai, imesitiriwa hata kwa ndege wa angani.
Essa è nascosta agli occhi d’ogni vivente, è celata agli uccelli del cielo.
22 Uharibifu na Mauti husema, ‘Ni uvumi wake tu uliotufikia masikioni mwetu.’
L’abisso e la morte dicono: “Ne abbiamo avuto qualche sentore”.
23 Mungu anaifahamu njia ya kuiendea hekima na ndiye peke yake anayefahamu inakokaa,
Dio solo conosce la via che vi mena, egli solo sa il luogo dove dimora,
24 kwa maana yeye huitazama miisho ya dunia na huona kila kitu chini ya mbingu.
perché il suo sguardo giunge sino alle estremità della terra, perch’egli vede tutto quel ch’è sotto i cieli.
25 Alipofanyiza nguvu za upepo na kuyapima maji,
Quando regolò il peso del vento e fissò la misura dell’acque,
26 alipofanya maagizo kwa ajili ya mvua na njia kwa ajili ya umeme wa radi,
quando dette una legge alla pioggia e tracciò la strada al lampo dei tuoni,
27 ndipo alipoitazama hekima na kuikadiria thamani yake, akaithibitisha na kuihakikisha.
allora la vide e la rivelò, la stabilì ed anche l’investigò.
28 Naye Mungu akamwambia mwanadamu, ‘Kumcha Bwana: hiyo ndiyo hekima, nako kujitenga na uovu ndio ufahamu.’”
E disse all’uomo: “Ecco: temere il Signore: questa è la Sapienza, e fuggire il male è l’Intelligenza”.”