< Ayubu 28 >
1 “Kuna machimbo ya fedha, na mahali dhahabu isafishwapo.
Certo, per l'argento vi sono miniere e per l'oro luoghi dove esso si raffina.
2 Chuma hupatikana ardhini, nayo shaba huyeyushwa kutoka mawe ya madini.
Il ferro si cava dal suolo e la pietra fusa libera il rame.
3 Mwanadamu hukomesha giza; huyatafuta hadi sehemu iliyo mbali, kwa ajili ya kuchimbua mawe yenye madini katika giza jeusi sana.
L'uomo pone un termine alle tenebre e fruga fino all'estremo limite le rocce nel buio più fondo.
4 Huchimba shimo jembamba mbali na makao ya watu, mahali paliposahaulika na nyayo za wanadamu; mbali na wanadamu huningʼinia na kupembea kwa kamba.
Forano pozzi lungi dall'abitato coloro che perdono l'uso dei piedi: pendono sospesi lontano dalla gente e vacillano.
5 Ardhi, ambako chakula hutoka, chini hugeuzwa kwa moto;
Una terra, da cui si trae pane, di sotto è sconvolta come dal fuoco.
6 yakuti samawi hutoka katika miamba yake, nalo vumbi lake lina vipande vya dhahabu.
Le sue pietre contengono zaffiri e oro la sua polvere.
7 Hakuna ndege awindaye aijuaye njia ile iliyofichika, wala hakuna jicho la mwewe lililoiona.
L'uccello rapace ne ignora il sentiero, non lo scorge neppure l'occhio dell'aquila,
8 Wanyama wa porini wanaotamba hawajawahi kupakanyaga, wala simba azungukaye huko.
non battuto da bestie feroci, né mai attraversato dal leopardo.
9 Mikono ya mwanadamu hushambulia miamba migumu sana, na kuiacha wazi mizizi ya milima.
Contro la selce l'uomo porta la mano, sconvolge le montagne:
10 Hutoboa shimo refu la kupenya chini kwa chini kwenye miamba; macho yake huona hazina zake zote.
nelle rocce scava gallerie e su quanto è prezioso posa l'occhio:
11 Hutafuta vyanzo vya mito na kuvileta vitu vilivyofichika katika nuru.
scandaglia il fondo dei fiumi e quel che vi è nascosto porta alla luce.
12 “Lakini hekima inaweza kupatikana wapi? Ufahamu unakaa wapi?
Ma la sapienza da dove si trae? E il luogo dell'intelligenza dov'è?
13 Mwanadamu hatambui thamani yake; haiwezi kupatikana katika nchi ya walio hai.
L'uomo non ne conosce la via, essa non si trova sulla terra dei viventi.
14 Kilindi husema, ‘Haiko ndani yangu’; bahari nayo husema, ‘Haiko pamoja nami.’
L'abisso dice: «Non è in me!» e il mare dice: «Neppure presso di me!».
15 Haiwezi kununuliwa kwa dhahabu safi kuliko zote, wala thamani yake haiwezi kupimwa kwa fedha.
Non si scambia con l'oro più scelto, né per comprarla si pesa l'argento.
16 Haiwezi kununuliwa kwa dhahabu ya Ofiri, kwa shohamu ya thamani kubwa au yakuti samawi ya thamani kubwa.
Non si acquista con l'oro di Ofir, con il prezioso berillo o con lo zaffiro.
17 Dhahabu wala mawe maangavu haviwezi kulinganishwa nayo, wala haiwezi hubadilishwa na vito vya dhahabu.
Non la pareggia l'oro e il cristallo, né si permuta con vasi di oro puro.
18 Marijani na yaspi hazistahili kutajwa; thamani ya hekima ni zaidi ya akiki nyekundu.
Coralli e perle non meritano menzione, vale più scoprire la sapienza che le gemme.
19 Yakuti manjano ipatikanayo Kushi haiwezi kulinganishwa nayo, wala haiwezi kununuliwa kwa dhahabu safi.
Non la eguaglia il topazio d'Etiopia; con l'oro puro non si può scambiare a peso.
20 “Ni wapi basi hekima itokako? Ufahamu hukaa wapi?
Ma da dove viene la sapienza? E il luogo dell'intelligenza dov'è?
21 Imefichika machoni pa kila kitu kilicho hai, imesitiriwa hata kwa ndege wa angani.
E' nascosta agli occhi di ogni vivente ed è ignota agli uccelli del cielo.
22 Uharibifu na Mauti husema, ‘Ni uvumi wake tu uliotufikia masikioni mwetu.’
L'abisso e la morte dicono: «Con gli orecchi ne udimmo la fama».
23 Mungu anaifahamu njia ya kuiendea hekima na ndiye peke yake anayefahamu inakokaa,
Dio solo ne conosce la via, lui solo sa dove si trovi,
24 kwa maana yeye huitazama miisho ya dunia na huona kila kitu chini ya mbingu.
perché volge lo sguardo fino alle estremità della terra, vede quanto è sotto la volta del cielo.
25 Alipofanyiza nguvu za upepo na kuyapima maji,
Quando diede al vento un peso e ordinò alle acque entro una misura,
26 alipofanya maagizo kwa ajili ya mvua na njia kwa ajili ya umeme wa radi,
quando impose una legge alla pioggia e una via al lampo dei tuoni;
27 ndipo alipoitazama hekima na kuikadiria thamani yake, akaithibitisha na kuihakikisha.
allora la vide e la misurò, la comprese e la scrutò appieno
28 Naye Mungu akamwambia mwanadamu, ‘Kumcha Bwana: hiyo ndiyo hekima, nako kujitenga na uovu ndio ufahamu.’”
e disse all'uomo: «Ecco, temere Dio, questo è sapienza e schivare il male, questo è intelligenza».