< Ayubu 28 >

1 “Kuna machimbo ya fedha, na mahali dhahabu isafishwapo.
L’argent a des sources de ses veines, et il y a pour l’or un lieu où il est mis en fusion.
2 Chuma hupatikana ardhini, nayo shaba huyeyushwa kutoka mawe ya madini.
Le fer est tiré de la terre, et une pierre dissoute par la chaleur est changée en airain.
3 Mwanadamu hukomesha giza; huyatafuta hadi sehemu iliyo mbali, kwa ajili ya kuchimbua mawe yenye madini katika giza jeusi sana.
Il a posé un temps déterminé aux ténèbres, et il considère lui-même la fin de toutes choses, aussi bien qu’une pierre cachée dans l’obscurité, et que l’ombre de la mort.
4 Huchimba shimo jembamba mbali na makao ya watu, mahali paliposahaulika na nyayo za wanadamu; mbali na wanadamu huningʼinia na kupembea kwa kamba.
Un torrent sépare d’un peuple étranger ceux que le pied de l’homme indigent a oubliés, et qui sont inaccessibles.
5 Ardhi, ambako chakula hutoka, chini hugeuzwa kwa moto;
Une terre d’où naissait du pain, a été bouleversée en son lieu par le feu.
6 yakuti samawi hutoka katika miamba yake, nalo vumbi lake lina vipande vya dhahabu.
Ses pierres sont le lieu du saphir, et ses glèbes sont de l’or.
7 Hakuna ndege awindaye aijuaye njia ile iliyofichika, wala hakuna jicho la mwewe lililoiona.
L’oiseau en a ignoré le sentier, et l’œil d’un vautour ne l’a pas regardé.
8 Wanyama wa porini wanaotamba hawajawahi kupakanyaga, wala simba azungukaye huko.
Les fils des marchands ne l’ont pas foulé, et la lionne ne l’a pas traversé.
9 Mikono ya mwanadamu hushambulia miamba migumu sana, na kuiacha wazi mizizi ya milima.
Il a étendu sa main contre des rochers, il a renversé des montagnes jusqu’à leurs racines.
10 Hutoboa shimo refu la kupenya chini kwa chini kwenye miamba; macho yake huona hazina zake zote.
Il a creusé des ruisseaux dans les pierres, et son œil a vu tout ce qu’il y a de précieux.
11 Hutafuta vyanzo vya mito na kuvileta vitu vilivyofichika katika nuru.
Il a scruté aussi les profondeurs des fleuves, et il a produit à la lumière des choses cachées.
12 “Lakini hekima inaweza kupatikana wapi? Ufahamu unakaa wapi?
Mais la sagesse, où se trouve-t-elle? Et quel est le lieu de l’intelligence?
13 Mwanadamu hatambui thamani yake; haiwezi kupatikana katika nchi ya walio hai.
L’homme n’en connaît pas le prix, et elle ne se trouve pas dans la terre de ceux qui vivent dans les délices.
14 Kilindi husema, ‘Haiko ndani yangu’; bahari nayo husema, ‘Haiko pamoja nami.’
L’abîme dit: Elle n’est pas en moi; la mer dit aussi; Elle n’est pas avec moi.
15 Haiwezi kununuliwa kwa dhahabu safi kuliko zote, wala thamani yake haiwezi kupimwa kwa fedha.
On ne la donnera pas pour l’or le plus affiné, et on ne l’échangera pas contre de l’argent au poids.
16 Haiwezi kununuliwa kwa dhahabu ya Ofiri, kwa shohamu ya thamani kubwa au yakuti samawi ya thamani kubwa.
On ne la comparera point aux tissus colorés de l’Inde, ni à la sardoine la plus précieuse ou au saphir.
17 Dhahabu wala mawe maangavu haviwezi kulinganishwa nayo, wala haiwezi hubadilishwa na vito vya dhahabu.
On ne lui égalera point l’or ou le verre, et on ne l’échangera point contre des vases d’or.
18 Marijani na yaspi hazistahili kutajwa; thamani ya hekima ni zaidi ya akiki nyekundu.
Ce qu’il y a de plus grand et de plus élevé ne sera pas même nommé auprès d’elle, mais la sagesse a une origine secrète.
19 Yakuti manjano ipatikanayo Kushi haiwezi kulinganishwa nayo, wala haiwezi kununuliwa kwa dhahabu safi.
On ne lui égalera pas la topaze de l’Ethiopie, et on ne la comparera pas aux teintures les plus éclatantes.
20 “Ni wapi basi hekima itokako? Ufahamu hukaa wapi?
D’où vient donc la sagesse, et quel est le lieu de l’intelligence?
21 Imefichika machoni pa kila kitu kilicho hai, imesitiriwa hata kwa ndege wa angani.
Elle est cachée aux yeux de tous les vivants, elle est inconnue aux oiseaux mêmes du ciel.
22 Uharibifu na Mauti husema, ‘Ni uvumi wake tu uliotufikia masikioni mwetu.’
La perdition et la mort ont dit: Nous avons ouï son nom de nos oreilles.
23 Mungu anaifahamu njia ya kuiendea hekima na ndiye peke yake anayefahamu inakokaa,
C’est Dieu qui comprend sa voie, et c’est lui qui connaît son lieu.
24 kwa maana yeye huitazama miisho ya dunia na huona kila kitu chini ya mbingu.
Car c’est lui qui observe les extrémités du monde, et qui considère tout ce qui est sous le ciel.
25 Alipofanyiza nguvu za upepo na kuyapima maji,
C’est lui qui a fait un poids aux vents, et qui a pesé les eaux avec une mesure.
26 alipofanya maagizo kwa ajili ya mvua na njia kwa ajili ya umeme wa radi,
Quand il imposait aux pluies une loi, et une voix aux tempêtes tonnantes,
27 ndipo alipoitazama hekima na kuikadiria thamani yake, akaithibitisha na kuihakikisha.
C’est alors qu’il l’a vue, qu’il l’a proclamée, et qu’il l’a scrutée.
28 Naye Mungu akamwambia mwanadamu, ‘Kumcha Bwana: hiyo ndiyo hekima, nako kujitenga na uovu ndio ufahamu.’”
Et il a dit à l’homme: Voici; la crainte du Seigneur, c’est la sagesse, et s’éloigner du mal, l’intelligence.

< Ayubu 28 >