< Ayubu 28 >

1 “Kuna machimbo ya fedha, na mahali dhahabu isafishwapo.
Il y a des contrées où naît l'argent, d'autres où l'on épure l'or.
2 Chuma hupatikana ardhini, nayo shaba huyeyushwa kutoka mawe ya madini.
Le fer se tire du sol, et l'airain, semblable à de la pierre, est extrait des mines.
3 Mwanadamu hukomesha giza; huyatafuta hadi sehemu iliyo mbali, kwa ajili ya kuchimbua mawe yenye madini katika giza jeusi sana.
Le Seigneur a réglé les ténèbres; il maintient ponctuellement les limites qu'il a tracées; la roche sombre se distingue de l'ombre de la mort,
4 Huchimba shimo jembamba mbali na makao ya watu, mahali paliposahaulika na nyayo za wanadamu; mbali na wanadamu huningʼinia na kupembea kwa kamba.
Le lit du torrent d'un amas de poussière; ceux qui abandonnent leur chemin s'affaiblissent, ils sont rejetés du reste des mortels.
5 Ardhi, ambako chakula hutoka, chini hugeuzwa kwa moto;
Le fond du sol d'où sortira le pain a été tourmenté comme du feu.
6 yakuti samawi hutoka katika miamba yake, nalo vumbi lake lina vipande vya dhahabu.
Parmi ses pierres on trouve le saphir, et il y a là aussi des amas d'or.
7 Hakuna ndege awindaye aijuaye njia ile iliyofichika, wala hakuna jicho la mwewe lililoiona.
Le sentier? L'oiseau ne l'a pas connu; l'œil du vautour ne s'y est point arrêté.
8 Wanyama wa porini wanaotamba hawajawahi kupakanyaga, wala simba azungukaye huko.
Les fils des vaniteux n'y ont point porté leurs pas; le lion n'a point passé auprès.
9 Mikono ya mwanadamu hushambulia miamba migumu sana, na kuiacha wazi mizizi ya milima.
L'homme a étendu sa main jusqu'à la cime des monts, il a ouvert leurs racines.
10 Hutoboa shimo refu la kupenya chini kwa chini kwenye miamba; macho yake huona hazina zake zote.
Il a fendu le tourbillon des fleuves, et mon œil a vu ce qu'il y a de précieux.
11 Hutafuta vyanzo vya mito na kuvileta vitu vilivyofichika katika nuru.
L'homme a exploré le fond des rivières, et il a mis au jour sa puissance.
12 “Lakini hekima inaweza kupatikana wapi? Ufahamu unakaa wapi?
Mais la sagesse, où est-elle trouvée? où la science réside-t-elle?
13 Mwanadamu hatambui thamani yake; haiwezi kupatikana katika nchi ya walio hai.
L'homme n'en sait pas le chemin, nul des mortels ne l'a découvert.
14 Kilindi husema, ‘Haiko ndani yangu’; bahari nayo husema, ‘Haiko pamoja nami.’
L'abîme dit: Elle n'est point en moi; la mer a dit: Elle n'est pas avec moi.
15 Haiwezi kununuliwa kwa dhahabu safi kuliko zote, wala thamani yake haiwezi kupimwa kwa fedha.
On ne l'obtient pas au prix de trésors; elle ne s'échange pas contre de l'argent.
16 Haiwezi kununuliwa kwa dhahabu ya Ofiri, kwa shohamu ya thamani kubwa au yakuti samawi ya thamani kubwa.
On ne la mettra point dans la balance avec de l'or d'Ophir, des saphirs et des onyx.
17 Dhahabu wala mawe maangavu haviwezi kulinganishwa nayo, wala haiwezi hubadilishwa na vito vya dhahabu.
Ni l'or ni le cristal ne la vaudront; on ne lui égalera pas des vases d'or.
18 Marijani na yaspi hazistahili kutajwa; thamani ya hekima ni zaidi ya akiki nyekundu.
On oubliera éclat et grandeurs; place la sagesse au-dessus de ce qu'il y a de plus intime.
19 Yakuti manjano ipatikanayo Kushi haiwezi kulinganishwa nayo, wala haiwezi kununuliwa kwa dhahabu safi.
On ne lui comparera pas la topaze de l'Ethiopie; on ne la pèsera pas avec de l'or pur.
20 “Ni wapi basi hekima itokako? Ufahamu hukaa wapi?
Où la sagesse a-t-elle été trouvée? En quel lieu est l'intelligence?
21 Imefichika machoni pa kila kitu kilicho hai, imesitiriwa hata kwa ndege wa angani.
Elle a échappé aux recherches de tous les hommes; elle est cachée pour les oiseaux du ciel.
22 Uharibifu na Mauti husema, ‘Ni uvumi wake tu uliotufikia masikioni mwetu.’
La perdition et la mort ont dit: Nous avons entendu parler de sa gloire.
23 Mungu anaifahamu njia ya kuiendea hekima na ndiye peke yake anayefahamu inakokaa,
Dieu seul a tracé sa voie; seul il sait où elle est.
24 kwa maana yeye huitazama miisho ya dunia na huona kila kitu chini ya mbingu.
Seul il voit tout sous le ciel; il connaît tout sur la terre.
25 Alipofanyiza nguvu za upepo na kuyapima maji,
Il voit et il connaît ce qu'il a créé: la force des vents et la mesure des eaux.
26 alipofanya maagizo kwa ajili ya mvua na njia kwa ajili ya umeme wa radi,
Aux jours de la création, après avoir tout considéré, il a tout réglé jusqu'aux ébranlements du tonnerre.
27 ndipo alipoitazama hekima na kuikadiria thamani yake, akaithibitisha na kuihakikisha.
Alors il a vu la sagesse et il lui a montré le chemin; il l'a préparée et observée avec attention.
28 Naye Mungu akamwambia mwanadamu, ‘Kumcha Bwana: hiyo ndiyo hekima, nako kujitenga na uovu ndio ufahamu.’”
Et il a dit à l'homme: Ecoute, la sagesse c'est la piété; la science c'est s'abstenir du mal.

< Ayubu 28 >