< Ayubu 28 >

1 “Kuna machimbo ya fedha, na mahali dhahabu isafishwapo.
“Surely there is a mine for silver, and a place for gold which they refine.
2 Chuma hupatikana ardhini, nayo shaba huyeyushwa kutoka mawe ya madini.
Iron is taken out of the earth, and copper is smelted out of the ore.
3 Mwanadamu hukomesha giza; huyatafuta hadi sehemu iliyo mbali, kwa ajili ya kuchimbua mawe yenye madini katika giza jeusi sana.
Man sets an end to darkness, and searches out, to the furthest bound, the stones of obscurity and of thick darkness.
4 Huchimba shimo jembamba mbali na makao ya watu, mahali paliposahaulika na nyayo za wanadamu; mbali na wanadamu huningʼinia na kupembea kwa kamba.
He breaks open a shaft away from where people live. They are forgotten by the foot. They hang far from men, they swing back and forth.
5 Ardhi, ambako chakula hutoka, chini hugeuzwa kwa moto;
As for the earth, out of it comes bread. Underneath it is turned up as it were by fire.
6 yakuti samawi hutoka katika miamba yake, nalo vumbi lake lina vipande vya dhahabu.
Sapphires come from its rocks. It has dust of gold.
7 Hakuna ndege awindaye aijuaye njia ile iliyofichika, wala hakuna jicho la mwewe lililoiona.
That path no bird of prey knows, neither has the falcon’s eye seen it.
8 Wanyama wa porini wanaotamba hawajawahi kupakanyaga, wala simba azungukaye huko.
The proud animals have not trodden it, nor has the fierce lion passed by there.
9 Mikono ya mwanadamu hushambulia miamba migumu sana, na kuiacha wazi mizizi ya milima.
He puts his hand on the flinty rock, and he overturns the mountains by the roots.
10 Hutoboa shimo refu la kupenya chini kwa chini kwenye miamba; macho yake huona hazina zake zote.
He cuts out channels amongst the rocks. His eye sees every precious thing.
11 Hutafuta vyanzo vya mito na kuvileta vitu vilivyofichika katika nuru.
He binds the streams that they don’t trickle. The thing that is hidden he brings out to light.
12 “Lakini hekima inaweza kupatikana wapi? Ufahamu unakaa wapi?
“But where will wisdom be found? Where is the place of understanding?
13 Mwanadamu hatambui thamani yake; haiwezi kupatikana katika nchi ya walio hai.
Man doesn’t know its price, and it isn’t found in the land of the living.
14 Kilindi husema, ‘Haiko ndani yangu’; bahari nayo husema, ‘Haiko pamoja nami.’
The deep says, ‘It isn’t in me.’ The sea says, ‘It isn’t with me.’
15 Haiwezi kununuliwa kwa dhahabu safi kuliko zote, wala thamani yake haiwezi kupimwa kwa fedha.
It can’t be gotten for gold, neither will silver be weighed for its price.
16 Haiwezi kununuliwa kwa dhahabu ya Ofiri, kwa shohamu ya thamani kubwa au yakuti samawi ya thamani kubwa.
It can’t be valued with the gold of Ophir, with the precious onyx, or the sapphire.
17 Dhahabu wala mawe maangavu haviwezi kulinganishwa nayo, wala haiwezi hubadilishwa na vito vya dhahabu.
Gold and glass can’t equal it, neither will it be exchanged for jewels of fine gold.
18 Marijani na yaspi hazistahili kutajwa; thamani ya hekima ni zaidi ya akiki nyekundu.
No mention will be made of coral or of crystal. Yes, the price of wisdom is above rubies.
19 Yakuti manjano ipatikanayo Kushi haiwezi kulinganishwa nayo, wala haiwezi kununuliwa kwa dhahabu safi.
The topaz of Ethiopia will not equal it. It won’t be valued with pure gold.
20 “Ni wapi basi hekima itokako? Ufahamu hukaa wapi?
Where then does wisdom come from? Where is the place of understanding?
21 Imefichika machoni pa kila kitu kilicho hai, imesitiriwa hata kwa ndege wa angani.
Seeing it is hidden from the eyes of all living, and kept close from the birds of the sky.
22 Uharibifu na Mauti husema, ‘Ni uvumi wake tu uliotufikia masikioni mwetu.’
Destruction and Death say, ‘We have heard a rumour of it with our ears.’
23 Mungu anaifahamu njia ya kuiendea hekima na ndiye peke yake anayefahamu inakokaa,
“God understands its way, and he knows its place.
24 kwa maana yeye huitazama miisho ya dunia na huona kila kitu chini ya mbingu.
For he looks to the ends of the earth, and sees under the whole sky.
25 Alipofanyiza nguvu za upepo na kuyapima maji,
He establishes the force of the wind. Yes, he measures out the waters by measure.
26 alipofanya maagizo kwa ajili ya mvua na njia kwa ajili ya umeme wa radi,
When he made a decree for the rain, and a way for the lightning of the thunder,
27 ndipo alipoitazama hekima na kuikadiria thamani yake, akaithibitisha na kuihakikisha.
then he saw it, and declared it. He established it, yes, and searched it out.
28 Naye Mungu akamwambia mwanadamu, ‘Kumcha Bwana: hiyo ndiyo hekima, nako kujitenga na uovu ndio ufahamu.’”
To man he said, ‘Behold, the fear of the Lord, that is wisdom. To depart from evil is understanding.’”

< Ayubu 28 >