< Ayubu 28 >

1 “Kuna machimbo ya fedha, na mahali dhahabu isafishwapo.
银子有矿; 炼金有方。
2 Chuma hupatikana ardhini, nayo shaba huyeyushwa kutoka mawe ya madini.
铁从地里挖出; 铜从石中熔化。
3 Mwanadamu hukomesha giza; huyatafuta hadi sehemu iliyo mbali, kwa ajili ya kuchimbua mawe yenye madini katika giza jeusi sana.
人为黑暗定界限, 查究幽暗阴翳的石头,直到极处,
4 Huchimba shimo jembamba mbali na makao ya watu, mahali paliposahaulika na nyayo za wanadamu; mbali na wanadamu huningʼinia na kupembea kwa kamba.
在无人居住之处刨开矿穴, 过路的人也想不到他们; 又与人远离,悬在空中摇来摇去。
5 Ardhi, ambako chakula hutoka, chini hugeuzwa kwa moto;
至于地,能出粮食, 地内好像被火翻起来。
6 yakuti samawi hutoka katika miamba yake, nalo vumbi lake lina vipande vya dhahabu.
地中的石头有蓝宝石, 并有金沙。
7 Hakuna ndege awindaye aijuaye njia ile iliyofichika, wala hakuna jicho la mwewe lililoiona.
矿中的路鸷鸟不得知道; 鹰眼也未见过。
8 Wanyama wa porini wanaotamba hawajawahi kupakanyaga, wala simba azungukaye huko.
狂傲的野兽未曾行过; 猛烈的狮子也未曾经过。
9 Mikono ya mwanadamu hushambulia miamba migumu sana, na kuiacha wazi mizizi ya milima.
人伸手凿开坚石, 倾倒山根,
10 Hutoboa shimo refu la kupenya chini kwa chini kwenye miamba; macho yake huona hazina zake zote.
在磐石中凿出水道, 亲眼看见各样宝物。
11 Hutafuta vyanzo vya mito na kuvileta vitu vilivyofichika katika nuru.
他封闭水不得滴流, 使隐藏的物显露出来。
12 “Lakini hekima inaweza kupatikana wapi? Ufahamu unakaa wapi?
然而,智慧有何处可寻? 聪明之处在哪里呢?
13 Mwanadamu hatambui thamani yake; haiwezi kupatikana katika nchi ya walio hai.
智慧的价值无人能知, 在活人之地也无处可寻。
14 Kilindi husema, ‘Haiko ndani yangu’; bahari nayo husema, ‘Haiko pamoja nami.’
深渊说:不在我内; 沧海说:不在我中。
15 Haiwezi kununuliwa kwa dhahabu safi kuliko zote, wala thamani yake haiwezi kupimwa kwa fedha.
智慧非用黄金可得, 也不能平白银为它的价值。
16 Haiwezi kununuliwa kwa dhahabu ya Ofiri, kwa shohamu ya thamani kubwa au yakuti samawi ya thamani kubwa.
俄斐金和贵重的红玛瑙, 并蓝宝石,不足与较量;
17 Dhahabu wala mawe maangavu haviwezi kulinganishwa nayo, wala haiwezi hubadilishwa na vito vya dhahabu.
黄金和玻璃不足与比较; 精金的器皿不足与兑换。
18 Marijani na yaspi hazistahili kutajwa; thamani ya hekima ni zaidi ya akiki nyekundu.
珊瑚、水晶都不足论; 智慧的价值胜过珍珠。
19 Yakuti manjano ipatikanayo Kushi haiwezi kulinganishwa nayo, wala haiwezi kununuliwa kwa dhahabu safi.
古实的红璧玺不足与比较; 精金也不足与较量。
20 “Ni wapi basi hekima itokako? Ufahamu hukaa wapi?
智慧从何处来呢? 聪明之处在哪里呢?
21 Imefichika machoni pa kila kitu kilicho hai, imesitiriwa hata kwa ndege wa angani.
是向一切有生命的眼目隐藏, 向空中的飞鸟掩蔽。
22 Uharibifu na Mauti husema, ‘Ni uvumi wake tu uliotufikia masikioni mwetu.’
灭没和死亡说: 我们风闻其名。
23 Mungu anaifahamu njia ya kuiendea hekima na ndiye peke yake anayefahamu inakokaa,
神明白智慧的道路, 晓得智慧的所在。
24 kwa maana yeye huitazama miisho ya dunia na huona kila kitu chini ya mbingu.
因他鉴察直到地极, 遍观普天之下,
25 Alipofanyiza nguvu za upepo na kuyapima maji,
要为风定轻重, 又度量诸水;
26 alipofanya maagizo kwa ajili ya mvua na njia kwa ajili ya umeme wa radi,
他为雨露定命令, 为雷电定道路。
27 ndipo alipoitazama hekima na kuikadiria thamani yake, akaithibitisha na kuihakikisha.
那时他看见智慧,而且述说; 他坚定,并且查究。
28 Naye Mungu akamwambia mwanadamu, ‘Kumcha Bwana: hiyo ndiyo hekima, nako kujitenga na uovu ndio ufahamu.’”
他对人说:敬畏主就是智慧; 远离恶便是聪明。

< Ayubu 28 >