< Ayubu 26 >

1 Kisha Ayubu akajibu:
Respondens autem Iob, dixit:
2 “Tazama jinsi ulivyomsaidia mtu asiye na uwezo! Jinsi ulivyouokoa mkono ulio dhaifu!
Cuius adiutor es? numquid imbecillis? et sustentas brachium eius, qui non est fortis?
3 Ni shauri gani ulilompa yeye asiye na hekima? Nayo ni busara gani kubwa uliyoonyesha!
Cui dedisti consilium? forsitan illi qui non habet sapientiam, et prudentiam tuam ostendisti plurimam.
4 Ni nani aliyekusaidia kutamka maneno hayo? Nayo ni roho ya nani iliyosema kutoka kinywani mwako?
Quem docere voluisti? nonne eum, qui fecit spiramentum?
5 “Wafu wako katika maumivu makuu, wale walio chini ya maji na wale waishio ndani yake.
Ecce gigantes gemunt sub aquis, et qui habitant cum eis.
6 Mauti iko wazi mbele za Mungu; Uharibifu haukufunikwa. (Sheol h7585)
Nudus est infernus coram illo, et nullum est operimentum perditioni. (Sheol h7585)
7 Hutandaza anga la kaskazini mahali patupu; naye huiningʼiniza dunia mahali pasipo na kitu.
Qui extendit Aquilonem super vacuum, et appendit terram super nihilum.
8 Huyafungia maji kwenye mawingu yake, hata hivyo mawingu hayapasuki kwa uzito wake.
Qui ligat aquas in nubibus suis, ut non erumpant pariter deorsum.
9 Huufunika uso wa mwezi mpevu, akitandaza mawingu juu yake.
Qui tenet vultum solii sui, et expandit super illud nebulam suam.
10 Amechora mstari wa upeo juu ya uso wa maji, ameweka mpaka wa nuru na giza.
Terminum circumdedit aquis, usque dum finiantur lux et tenebræ.
11 Nguzo za mbingu nazo zatetemeka, zinatishika anapozikemea.
Columnæ cæli contremiscunt, et pavent ad nutum eius.
12 Kwa nguvu zake aliisukasuka bahari; kwa hekima yake alimkata Rahabu vipande vipande.
In fortitudine illius repente maria congregata sunt, et prudentia eius percussit superbum.
13 Aliisafisha anga kwa pumzi yake; kwa mkono wake alimchoma joka aendaye mbio.
Spiritus eius ornavit cælos: et obstetricante manu eius, eductus est coluber tortuosus.
14 Haya ni mambo madogo tu katika matendo yake; tazama jinsi ulivyo mdogo mnongʼono tunaousikia kumhusu! Ni nani basi awezaye kuelewa ngurumo za nguvu zake?”
Ecce, hæc ex parte dicta sunt viarum eius: et cum vix parvam stillam sermonis eius audierimus, quis poterit tonitruum magnitudinis illius intueri?

< Ayubu 26 >