< Ayubu 26 >

1 Kisha Ayubu akajibu:
そこでヨブは答えて言った、
2 “Tazama jinsi ulivyomsaidia mtu asiye na uwezo! Jinsi ulivyouokoa mkono ulio dhaifu!
「あなたは力のない者をどれほど助けたかしれない。気力のない腕をどれほど救ったかしれない。
3 Ni shauri gani ulilompa yeye asiye na hekima? Nayo ni busara gani kubwa uliyoonyesha!
知恵のない者をどれほど教えたかしれない。悟りをどれほど多く示したかしれない。
4 Ni nani aliyekusaidia kutamka maneno hayo? Nayo ni roho ya nani iliyosema kutoka kinywani mwako?
あなたはだれの助けによって言葉をだしたのか。あなたから出たのはだれの霊なのか。
5 “Wafu wako katika maumivu makuu, wale walio chini ya maji na wale waishio ndani yake.
亡霊は水およびその中に住むものの下に震う。
6 Mauti iko wazi mbele za Mungu; Uharibifu haukufunikwa. (Sheol h7585)
神の前では陰府も裸である。滅びの穴もおおい隠すものはない。 (Sheol h7585)
7 Hutandaza anga la kaskazini mahali patupu; naye huiningʼiniza dunia mahali pasipo na kitu.
彼は北の天を空間に張り、地を何もない所に掛けられる。
8 Huyafungia maji kwenye mawingu yake, hata hivyo mawingu hayapasuki kwa uzito wake.
彼は水を濃い雲の中に包まれるが、その下の雲は裂けない。
9 Huufunika uso wa mwezi mpevu, akitandaza mawingu juu yake.
彼は月のおもてをおおい隠して、雲をその上にのべ、
10 Amechora mstari wa upeo juu ya uso wa maji, ameweka mpaka wa nuru na giza.
水のおもてに円を描いて、光とやみとの境とされた。
11 Nguzo za mbingu nazo zatetemeka, zinatishika anapozikemea.
彼が戒めると、天の柱は震い、かつ驚く。
12 Kwa nguvu zake aliisukasuka bahari; kwa hekima yake alimkata Rahabu vipande vipande.
彼はその力をもって海を静め、その知恵をもってラハブを打ち砕き、
13 Aliisafisha anga kwa pumzi yake; kwa mkono wake alimchoma joka aendaye mbio.
その息をもって天を晴れわたらせ、その手をもって逃げるへびを突き通される。
14 Haya ni mambo madogo tu katika matendo yake; tazama jinsi ulivyo mdogo mnongʼono tunaousikia kumhusu! Ni nani basi awezaye kuelewa ngurumo za nguvu zake?”
見よ、これらはただ彼の道の端にすぎない。われわれが彼について聞く所はいかにかすかなささやきであろう。しかし、その力のとどろきに至っては、だれが悟ることができるか」。

< Ayubu 26 >