< Ayubu 26 >

1 Kisha Ayubu akajibu:
Da antwortete Hiob folgendermaßen:
2 “Tazama jinsi ulivyomsaidia mtu asiye na uwezo! Jinsi ulivyouokoa mkono ulio dhaifu!
»Wie hast du doch dem Schwachen beigestanden und den kraftlosen Arm gestützt!
3 Ni shauri gani ulilompa yeye asiye na hekima? Nayo ni busara gani kubwa uliyoonyesha!
Wie gut hast du doch den Unweisen beraten und tiefes Wissen in Fülle kundgetan!
4 Ni nani aliyekusaidia kutamka maneno hayo? Nayo ni roho ya nani iliyosema kutoka kinywani mwako?
Wem hast du einen Lehrvortrag gehalten, und wessen Odem ist dir entströmt?«
5 “Wafu wako katika maumivu makuu, wale walio chini ya maji na wale waishio ndani yake.
»Die Schatten erzittern (vor Gott) tief unter den Wassern und deren Bewohnern;
6 Mauti iko wazi mbele za Mungu; Uharibifu haukufunikwa. (Sheol h7585)
nackt liegt das Totenreich vor ihm da und unverhüllt der Abgrund. (Sheol h7585)
7 Hutandaza anga la kaskazini mahali patupu; naye huiningʼiniza dunia mahali pasipo na kitu.
Er spannt den Norden (der Erde) über der Leere aus, hängt die Erde an dem Nichts auf.
8 Huyafungia maji kwenye mawingu yake, hata hivyo mawingu hayapasuki kwa uzito wake.
Er bindet die Wasser in seine Wolken ein, ohne daß das Gewölk unter ihrer Last zerplatzt.
9 Huufunika uso wa mwezi mpevu, akitandaza mawingu juu yake.
Er verhüllt den Anblick seines Thrones, indem er sein Gewölk über ihn ausbreitet.
10 Amechora mstari wa upeo juu ya uso wa maji, ameweka mpaka wa nuru na giza.
Eine Grenzlinie hat er über den weiten Wassern abgezirkelt bis zur äußersten Grenze, wo das Licht mit der Finsternis zusammentrifft.
11 Nguzo za mbingu nazo zatetemeka, zinatishika anapozikemea.
Die Säulen des Himmels geraten ins Wanken und beben infolge seines Scheltens.
12 Kwa nguvu zake aliisukasuka bahari; kwa hekima yake alimkata Rahabu vipande vipande.
Durch seine Kraft beruhigt er das Meer, und durch seine Klugheit hat er Rahab zerschmettert.
13 Aliisafisha anga kwa pumzi yake; kwa mkono wake alimchoma joka aendaye mbio.
Durch seinen Hauch gewinnt der Himmel Heiterkeit; durchbohrt hat seine Hand den flüchtigen Drachen.
14 Haya ni mambo madogo tu katika matendo yake; tazama jinsi ulivyo mdogo mnongʼono tunaousikia kumhusu! Ni nani basi awezaye kuelewa ngurumo za nguvu zake?”
Siehe, das sind nur die Säume seines Waltens, und welch ein leises Flüstern nur ist es, das wir von ihm vernehmen! Doch die Donnersprache seiner Machterweise – wer versteht diese?«

< Ayubu 26 >