< Ayubu 26 >
Job prit la parole et dit:
2 “Tazama jinsi ulivyomsaidia mtu asiye na uwezo! Jinsi ulivyouokoa mkono ulio dhaifu!
Comme tu sais bien venir en aide à la faiblesse! Comme tu prêtes secours au bras sans force!
3 Ni shauri gani ulilompa yeye asiye na hekima? Nayo ni busara gani kubwa uliyoonyesha!
Quels bons conseils tu donnes à celui qui manque d’intelligence! Quelle abondance de sagesse tu fais paraître!
4 Ni nani aliyekusaidia kutamka maneno hayo? Nayo ni roho ya nani iliyosema kutoka kinywani mwako?
A qui s’adressent tes paroles? Et qui est-ce qui t’inspire?
5 “Wafu wako katika maumivu makuu, wale walio chini ya maji na wale waishio ndani yake.
Devant Dieu les ombres tremblent Au-dessous des eaux et de leurs habitants;
6 Mauti iko wazi mbele za Mungu; Uharibifu haukufunikwa. (Sheol )
Devant lui le séjour des morts est nu, L’abîme n’a point de voile. (Sheol )
7 Hutandaza anga la kaskazini mahali patupu; naye huiningʼiniza dunia mahali pasipo na kitu.
Il étend le septentrion sur le vide, Il suspend la terre sur le néant.
8 Huyafungia maji kwenye mawingu yake, hata hivyo mawingu hayapasuki kwa uzito wake.
Il renferme les eaux dans ses nuages, Et les nuages n’éclatent pas sous leur poids.
9 Huufunika uso wa mwezi mpevu, akitandaza mawingu juu yake.
Il couvre la face de son trône, Il répand sur lui sa nuée.
10 Amechora mstari wa upeo juu ya uso wa maji, ameweka mpaka wa nuru na giza.
Il a tracé un cercle à la surface des eaux, Comme limite entre la lumière et les ténèbres.
11 Nguzo za mbingu nazo zatetemeka, zinatishika anapozikemea.
Les colonnes du ciel s’ébranlent, Et s’étonnent à sa menace.
12 Kwa nguvu zake aliisukasuka bahari; kwa hekima yake alimkata Rahabu vipande vipande.
Par sa force il soulève la mer, Par son intelligence il en brise l’orgueil.
13 Aliisafisha anga kwa pumzi yake; kwa mkono wake alimchoma joka aendaye mbio.
Son souffle donne au ciel la sérénité, Sa main transperce le serpent fuyard.
14 Haya ni mambo madogo tu katika matendo yake; tazama jinsi ulivyo mdogo mnongʼono tunaousikia kumhusu! Ni nani basi awezaye kuelewa ngurumo za nguvu zake?”
Ce sont là les bords de ses voies, C’est le bruit léger qui nous en parvient; Mais qui entendra le tonnerre de sa puissance?