< Ayubu 26 >
2 “Tazama jinsi ulivyomsaidia mtu asiye na uwezo! Jinsi ulivyouokoa mkono ulio dhaifu!
Comme tu as aidé celui qui n’avait pas de puissance! Comme tu as délivré le bras qui était sans force!
3 Ni shauri gani ulilompa yeye asiye na hekima? Nayo ni busara gani kubwa uliyoonyesha!
Quel conseil tu as donné à celui qui n’avait pas de sagesse! et quelle abondance d’intelligence tu as montrée!
4 Ni nani aliyekusaidia kutamka maneno hayo? Nayo ni roho ya nani iliyosema kutoka kinywani mwako?
Pour qui as-tu prononcé des paroles, et de qui est le souffle qui est sorti de toi?
5 “Wafu wako katika maumivu makuu, wale walio chini ya maji na wale waishio ndani yake.
Les trépassés tremblent au-dessous des eaux et de ceux qui les habitent.
6 Mauti iko wazi mbele za Mungu; Uharibifu haukufunikwa. (Sheol )
Le shéol est à nu devant lui, et l’abîme n’a pas de voile. (Sheol )
7 Hutandaza anga la kaskazini mahali patupu; naye huiningʼiniza dunia mahali pasipo na kitu.
Il étend le nord sur le vide, il suspend la terre sur le néant.
8 Huyafungia maji kwenye mawingu yake, hata hivyo mawingu hayapasuki kwa uzito wake.
Il serre les eaux dans ses nuages, et la nuée ne se fend pas sous elles;
9 Huufunika uso wa mwezi mpevu, akitandaza mawingu juu yake.
Il couvre la face de son trône et étend ses nuées par-dessus.
10 Amechora mstari wa upeo juu ya uso wa maji, ameweka mpaka wa nuru na giza.
Il a tracé un cercle fixe sur la face des eaux, jusqu’à la limite extrême où la lumière confine aux ténèbres.
11 Nguzo za mbingu nazo zatetemeka, zinatishika anapozikemea.
Les colonnes des cieux branlent et s’étonnent à sa menace.
12 Kwa nguvu zake aliisukasuka bahari; kwa hekima yake alimkata Rahabu vipande vipande.
Il soulève la mer par sa puissance, et, par son intelligence, il brise Rahab.
13 Aliisafisha anga kwa pumzi yake; kwa mkono wake alimchoma joka aendaye mbio.
Par son Esprit le ciel est beau; sa main a formé le serpent fuyard.
14 Haya ni mambo madogo tu katika matendo yake; tazama jinsi ulivyo mdogo mnongʼono tunaousikia kumhusu! Ni nani basi awezaye kuelewa ngurumo za nguvu zake?”
Voici, ces choses sont les bords de ses voies, et combien faible est le murmure que nous en avons entendu! Et le tonnerre de sa force, qui peut le comprendre?