< Ayubu 26 >

1 Kisha Ayubu akajibu:
Then Job answered,
2 “Tazama jinsi ulivyomsaidia mtu asiye na uwezo! Jinsi ulivyouokoa mkono ulio dhaifu!
“How have you helped him who is without power! How have you saved the arm that has no strength!
3 Ni shauri gani ulilompa yeye asiye na hekima? Nayo ni busara gani kubwa uliyoonyesha!
How have you counselled him who has no wisdom, and plentifully declared sound knowledge!
4 Ni nani aliyekusaidia kutamka maneno hayo? Nayo ni roho ya nani iliyosema kutoka kinywani mwako?
To whom have you uttered words? Whose spirit came out of you?
5 “Wafu wako katika maumivu makuu, wale walio chini ya maji na wale waishio ndani yake.
“The departed spirits tremble, those beneath the waters and all that live in them.
6 Mauti iko wazi mbele za Mungu; Uharibifu haukufunikwa. (Sheol h7585)
Sheol is naked before God, and Abaddon has no covering. (Sheol h7585)
7 Hutandaza anga la kaskazini mahali patupu; naye huiningʼiniza dunia mahali pasipo na kitu.
He stretches out the north over empty space, and hangs the earth on nothing.
8 Huyafungia maji kwenye mawingu yake, hata hivyo mawingu hayapasuki kwa uzito wake.
He binds up the waters in his thick clouds, and the cloud is not burst under them.
9 Huufunika uso wa mwezi mpevu, akitandaza mawingu juu yake.
He encloses the face of his throne, and spreads his cloud on it.
10 Amechora mstari wa upeo juu ya uso wa maji, ameweka mpaka wa nuru na giza.
He has described a boundary on the surface of the waters, and to the confines of light and darkness.
11 Nguzo za mbingu nazo zatetemeka, zinatishika anapozikemea.
The pillars of heaven tremble and are astonished at his rebuke.
12 Kwa nguvu zake aliisukasuka bahari; kwa hekima yake alimkata Rahabu vipande vipande.
He stirs up the sea with his power, and by his understanding he strikes through Rahab.
13 Aliisafisha anga kwa pumzi yake; kwa mkono wake alimchoma joka aendaye mbio.
By his Spirit the heavens are garnished. His hand has pierced the swift serpent.
14 Haya ni mambo madogo tu katika matendo yake; tazama jinsi ulivyo mdogo mnongʼono tunaousikia kumhusu! Ni nani basi awezaye kuelewa ngurumo za nguvu zake?”
Behold, these are but the outskirts of his ways. How small a whisper do we hear of him! But the thunder of his power who can understand?”

< Ayubu 26 >