< Ayubu 26 >

1 Kisha Ayubu akajibu:
Then answered Job, and said,
2 “Tazama jinsi ulivyomsaidia mtu asiye na uwezo! Jinsi ulivyouokoa mkono ulio dhaifu!
What assistance hast thou given to the powerless? [how] hast thou helped the arm without strength?
3 Ni shauri gani ulilompa yeye asiye na hekima? Nayo ni busara gani kubwa uliyoonyesha!
How hast thou counselled the unwise? and what sound wisdom hast thou made known so plentifully?
4 Ni nani aliyekusaidia kutamka maneno hayo? Nayo ni roho ya nani iliyosema kutoka kinywani mwako?
To whom hast thou told words? and whose spirit came from thee?
5 “Wafu wako katika maumivu makuu, wale walio chini ya maji na wale waishio ndani yake.
The departed are called into being beneath the waters, and their inhabitants.
6 Mauti iko wazi mbele za Mungu; Uharibifu haukufunikwa. (Sheol h7585)
Naked is the nether world before him, and there is no covering for the place of corruption. (Sheol h7585)
7 Hutandaza anga la kaskazini mahali patupu; naye huiningʼiniza dunia mahali pasipo na kitu.
He stretched out the north over empty space; he suspended the earth on nothing;
8 Huyafungia maji kwenye mawingu yake, hata hivyo mawingu hayapasuki kwa uzito wake.
He bound up the waters in his clouds; and the cloud bursteth not under their weight;
9 Huufunika uso wa mwezi mpevu, akitandaza mawingu juu yake.
He closed up the surface of his throne, spreading over it his cloud;
10 Amechora mstari wa upeo juu ya uso wa maji, ameweka mpaka wa nuru na giza.
A fixed limit he compassed off over the face of the waters, for the division of the light and darkness.
11 Nguzo za mbingu nazo zatetemeka, zinatishika anapozikemea.
The pillars of heaven tremble greatly, and are astounded at his rebuke.
12 Kwa nguvu zake aliisukasuka bahari; kwa hekima yake alimkata Rahabu vipande vipande.
By his power he split in pieces the sea, and by his understanding he crushed [its] pride:
13 Aliisafisha anga kwa pumzi yake; kwa mkono wake alimchoma joka aendaye mbio.
By his breath the heavens [acquired] beauty; his hand hath created the flying serpent.
14 Haya ni mambo madogo tu katika matendo yake; tazama jinsi ulivyo mdogo mnongʼono tunaousikia kumhusu! Ni nani basi awezaye kuelewa ngurumo za nguvu zake?”
Lo, these are ends of his ways; for how slight a whisper is heard [by us] of him! but the thunder of his mighty deeds who can understand?

< Ayubu 26 >