< Ayubu 26 >
2 “Tazama jinsi ulivyomsaidia mtu asiye na uwezo! Jinsi ulivyouokoa mkono ulio dhaifu!
“How you have helped the powerless and saved the arm that is feeble!
3 Ni shauri gani ulilompa yeye asiye na hekima? Nayo ni busara gani kubwa uliyoonyesha!
How you have counseled the unwise and provided fully sound insight!
4 Ni nani aliyekusaidia kutamka maneno hayo? Nayo ni roho ya nani iliyosema kutoka kinywani mwako?
To whom have you uttered these words? And whose spirit spoke through you?
5 “Wafu wako katika maumivu makuu, wale walio chini ya maji na wale waishio ndani yake.
The dead tremble— those beneath the waters and those who dwell in them.
6 Mauti iko wazi mbele za Mungu; Uharibifu haukufunikwa. (Sheol )
Sheol is naked before God, and Abaddon has no covering. (Sheol )
7 Hutandaza anga la kaskazini mahali patupu; naye huiningʼiniza dunia mahali pasipo na kitu.
He stretches out the north over empty space; He hangs the earth upon nothing.
8 Huyafungia maji kwenye mawingu yake, hata hivyo mawingu hayapasuki kwa uzito wake.
He wraps up the waters in His clouds, yet the clouds do not burst under their own weight.
9 Huufunika uso wa mwezi mpevu, akitandaza mawingu juu yake.
He covers the face of the full moon, spreading over it His cloud.
10 Amechora mstari wa upeo juu ya uso wa maji, ameweka mpaka wa nuru na giza.
He has inscribed a horizon on the face of the waters at the boundary between light and darkness.
11 Nguzo za mbingu nazo zatetemeka, zinatishika anapozikemea.
The foundations of heaven quake, astounded at His rebuke.
12 Kwa nguvu zake aliisukasuka bahari; kwa hekima yake alimkata Rahabu vipande vipande.
By His power He stirred the sea; by His understanding He shattered Rahab.
13 Aliisafisha anga kwa pumzi yake; kwa mkono wake alimchoma joka aendaye mbio.
By His breath the skies were cleared; His hand pierced the fleeing serpent.
14 Haya ni mambo madogo tu katika matendo yake; tazama jinsi ulivyo mdogo mnongʼono tunaousikia kumhusu! Ni nani basi awezaye kuelewa ngurumo za nguvu zake?”
Indeed, these are but the fringes of His ways; how faint is the whisper we hear of Him! Who then can understand the thunder of His power?”