< Ayubu 26 >

1 Kisha Ayubu akajibu:
Job antwoordde, en sprak
2 “Tazama jinsi ulivyomsaidia mtu asiye na uwezo! Jinsi ulivyouokoa mkono ulio dhaifu!
Hoe goed weet ge den zwakke te helpen, De krachteloze arm te stutten?
3 Ni shauri gani ulilompa yeye asiye na hekima? Nayo ni busara gani kubwa uliyoonyesha!
Hoe weet ge den onwetende raad te geven, En wat wijze lessen spreidt ge ten toon?
4 Ni nani aliyekusaidia kutamka maneno hayo? Nayo ni roho ya nani iliyosema kutoka kinywani mwako?
Met wiens hulp hebt ge uw woord gesproken Wiens geest is van u uitgegaan?
5 “Wafu wako katika maumivu makuu, wale walio chini ya maji na wale waishio ndani yake.
De schimmen beven onder de aarde De wateren sidderen met die erin wonen;
6 Mauti iko wazi mbele za Mungu; Uharibifu haukufunikwa. (Sheol h7585)
Het dodenrijk ligt naakt voor zijn oog, De onderwereld zonder bedekking. (Sheol h7585)
7 Hutandaza anga la kaskazini mahali patupu; naye huiningʼiniza dunia mahali pasipo na kitu.
Hij spant het Noorden over de baaierd, Hangt de aarde boven het niet;
8 Huyafungia maji kwenye mawingu yake, hata hivyo mawingu hayapasuki kwa uzito wake.
Hij knevelt de wateren in zijn zwerk, De wolken bersten niet onder haar last;
9 Huufunika uso wa mwezi mpevu, akitandaza mawingu juu yake.
Hij bedekt het gelaat der volle maan, En spreidt er zijn nevel over uit.
10 Amechora mstari wa upeo juu ya uso wa maji, ameweka mpaka wa nuru na giza.
Hij trekt een kring langs de waterspiegel, Waar het licht aan de duisternis grenst;
11 Nguzo za mbingu nazo zatetemeka, zinatishika anapozikemea.
De zuilen van de hemel staan te waggelen, Rillen van angst voor zijn donderende stem.
12 Kwa nguvu zake aliisukasuka bahari; kwa hekima yake alimkata Rahabu vipande vipande.
Hij zwiept de zee door zijn kracht, Ranselt Ráhab door zijn beleid;
13 Aliisafisha anga kwa pumzi yake; kwa mkono wake alimchoma joka aendaye mbio.
Zijn adem blaast de hemel schoon, Zijn hand doorboort de vluchtende Slang!
14 Haya ni mambo madogo tu katika matendo yake; tazama jinsi ulivyo mdogo mnongʼono tunaousikia kumhusu! Ni nani basi awezaye kuelewa ngurumo za nguvu zake?”
Is dit nog enkel de zoom van zijn wegen Hoe weinig verstaan wij ervan, En wie begrijpt dan de kracht van zijn donder?

< Ayubu 26 >