< Ayubu 26 >

1 Kisha Ayubu akajibu:
約伯回答說:
2 “Tazama jinsi ulivyomsaidia mtu asiye na uwezo! Jinsi ulivyouokoa mkono ulio dhaifu!
無能為力的人,你怎樣援助了他﹖無力的手臂,你怎樣支持了他﹖
3 Ni shauri gani ulilompa yeye asiye na hekima? Nayo ni busara gani kubwa uliyoonyesha!
你給無知的人出過什麼主義,表現了你豐富的智慧﹖
4 Ni nani aliyekusaidia kutamka maneno hayo? Nayo ni roho ya nani iliyosema kutoka kinywani mwako?
你說這些話是指教誰﹖從你心裏發出的是什麼精神﹖
5 “Wafu wako katika maumivu makuu, wale walio chini ya maji na wale waishio ndani yake.
幽魂在地下打顫,海底與居於海底的,驚恐不已。
6 Mauti iko wazi mbele za Mungu; Uharibifu haukufunikwa. (Sheol h7585)
陰府在他前面顯露,死域也沒有遮掩。 (Sheol h7585)
7 Hutandaza anga la kaskazini mahali patupu; naye huiningʼiniza dunia mahali pasipo na kitu.
他將北極伸張到太虛,將大地懸於虛無之上。
8 Huyafungia maji kwenye mawingu yake, hata hivyo mawingu hayapasuki kwa uzito wake.
他將水包裹在濃雲中,托水的雲彩卻不破裂。
9 Huufunika uso wa mwezi mpevu, akitandaza mawingu juu yake.
他遮蔽了滿月的面貌,使雲彩散佈其上。
10 Amechora mstari wa upeo juu ya uso wa maji, ameweka mpaka wa nuru na giza.
在水面上劃了一圓圈,當作光明與黑暗的分界。
11 Nguzo za mbingu nazo zatetemeka, zinatishika anapozikemea.
支天的柱子震動,因他的呵叱而戰慄。
12 Kwa nguvu zake aliisukasuka bahari; kwa hekima yake alimkata Rahabu vipande vipande.
他以威力使海洋動盪,以明智擊傷了海怪。
13 Aliisafisha anga kwa pumzi yake; kwa mkono wake alimchoma joka aendaye mbio.
他一噓氣,天氣清朗;他親手戮穿了飛龍。
14 Haya ni mambo madogo tu katika matendo yake; tazama jinsi ulivyo mdogo mnongʼono tunaousikia kumhusu! Ni nani basi awezaye kuelewa ngurumo za nguvu zake?”
看啊! 這只是他行動的一端,我們所聽到的語句,何其細微! 他轟轟烈烈的作為,有誰能明瞭﹖

< Ayubu 26 >