< Ayubu 24 >
1 “Kwa nini Mwenyezi asiweke nyakati kwa ajili ya hukumu? Kwa nini wale wamjuao wazitafute siku kama hizo bila mafanikio?
Les temps ne sont pas cachés au Tout-Puissant; mais ceux qui le connaissent ignorent ses jours.
2 Watu husogeza mawe ya mpaka; huchunga makundi ya wanyama waliyonyangʼanya kwa nguvu.
Les uns ont transporté des bornes, ravi des troupeaux, et les ont fait paître.
3 Huwanyangʼanya yatima punda wao, na kumchukua rehani fahali wa mjane.
Ils ont chassé l’âne des pupilles, et ils ont enlevé pour gage le bœuf de la veuve.
4 Humsukuma mhitaji kutoka njia, na kuwafanya maskini wote wa nchi kulazimika kujificha.
Ils ont détruit la voie du pauvre, et ils ont pareillement opprimé les hommes doux de la terre,
5 Kama punda-mwitu jangwani, maskini huzunguka katika kazi zao za kutafuta chakula; mahali palipo jangwa huwapa chakula cha watoto wao.
Les autres, comme les onagres dans le désert, sortent pour leur ouvrage; veillant à leur proie, ils préparent du pain à leurs enfants.
6 Hukusanya chakula mashambani na kuokota masazo katika mashamba ya mizabibu ya waovu.
Ils moissonnent le champ qui n’est pas à eux; ils vendangent la vigne de celui qu’ils ont opprimé par la force.
7 Kwa kukosa nguo, usiku kucha hukaa uchi; hawana chochote cha kujifunika baridi.
Ils renvoient des hommes tout nus, enlevant les vêtements à ceux qui n’ont pas de quoi se couvrir pendant le froid,
8 Hutota kwa mvua za mlimani, nao huikumbatia miamba kwa ajili ya kukosa pa kujisitiri.
Que les pluies des montagnes inondent, et qui n’ayant pas de vêtement, se réfugient dans des rochers.
9 Mtoto yatima hupokonywa matitini; mtoto wachanga wa maskini hunyakuliwa kwa ajili ya deni.
Ils ont usé de violence, pillant des orphelins; et le pauvre peuple, ils l’ont dépouillé.
10 Kwa kukosa nguo, hutembea uchi; hubeba miganda ya ngano, lakini huwa na njaa.
À ceux qui étaient nus et qui allaient sans vêtements, et à ceux qui avaient faim, ils ont pris des épis.
11 Hukamua zeituni katika mawe ya kusagia; hukanyaga mashinikizo, lakini wanaona kiu.
Ils ont fait la méridienne au milieu des tas de fruits de ceux qui, après avoir foulé des pressoirs, avaient soif.
12 Kilio cha huzuni cha wanaokufa kinapaa kutoka mjini, nazo nafsi za waliojeruhiwa zinalilia msaada. Lakini Mungu hamlaumu mtu yeyote kwa kutenda mabaya.
Dans les villes, ils ont fait gémir les hommes, et l’âme des blessés a crié, et Dieu ne souffre pas que ce mal passe impuni.
13 “Wako wale wanaoiasi nuru, wasiofahamu njia zake wala hawakai katika mapito yake.
Ils ont été rebelles à la lumière; ils n’ont pas connu les voies de Dieu, et ils ne sont pas revenus par ses sentiers,
14 Wakati mwanga wa mchana unapotoweka, muuaji huinuka naye huwaua maskini na mhitaji; wakati wa usiku hunyemelea kama mwizi.
L’homicide se lève dès le grand matin, il tue l’indigent et le pauvre; et pendant la nuit, il sera comme un voleur.
15 Jicho la mzinzi hungojea wakati wa giza, naye hufikiri, ‘Hakuna jicho litakaloniona,’ naye huuficha uso wake.
L’œil d’un adultère épie l’obscurité, disant: Aucun œil ne me verra; et il couvrira son visage.
16 Katika giza, huvunja majumba, lakini wakati wa mchana hujifungia ndani; hawataki kufanya lolote nuruni.
Il perce des maisons dans les ténèbres, comme ils en étaient convenus pendant le jour; et ils n’ont pas connu la lumière.
17 Kwa wote hawa, giza nene ndiyo asubuhi yao; hujifanya rafiki na vitisho vya gizani.
Si tout d’un coup apparaît l’aurore, ils croient que c’est l’ombre de la mort; et ainsi dans les ténèbres, ils marchent comme à la lumière.
18 “Lakini wao ni povu juu ya maji; sehemu yao juu ya nchi imelaaniwa, hivyo hakuna hata mmoja aendaye kwenye shamba la mizabibu.
Il est plus léger que la face de l’eau; maudite soit sa part sur la terre, et qu’il ne marche point par le chemin des vignes.
19 Kama vile joto na hari vinyakuavyo theluji iliyoyeyuka, ndivyo kuzimu kuwanyakuavyo waliotenda dhambi. (Sheol )
Qu’il passe des eaux des neiges à une excessive chaleur, et que jusques aux enfers son péché le conduise. (Sheol )
20 Tumbo lililowazaa huwasahau, nao huwa karamu ya mabuu; watu waovu hawakumbukwi tena, lakini huvunjika kama mti.
Que la miséricorde l’oublie; que les vers soient ses délices; qu’il ne soit point dans le souvenir des hommes; mais qu’il soit brisé comme un arbre infructueux.
21 Huwafanya mawindo wanawake tasa na wasio na watoto, nao hawaonyeshi huruma kwa wajane.
Car il a nourri la femme stérile, qui n’enfante pas, et il n’a pas fait de bien à la veuve.
22 Lakini Mungu huwakokota wenye nguvu kwa uwezo wake; ingawa wamestawi, hawana hakika ya maisha.
il a abattu des hommes forts par sa puissance; et lorsqu’il sera ferme, il ne croira pas en sa vie.
23 Aweza akawaacha wakapumzika wakijihisi salama, lakini macho yake yanaona njia zao.
Dieu lui a donné lieu de faire pénitence, et lui en abuse pour s’enorgueillir; mais les yeux de Dieu sont sur ses voies.
24 Kwa kitambo kidogo hutukuka, hatimaye hutoweka; hushushwa na kukusanywa kama wengine wote, hukatwa kama masuke ya nafaka.
Ils se sont élevés pour un moment, et ils ne subsisteront pas; ils seront humiliés comme toutes choses, puis ils seront emportés, et brisés comme des sommités d’épis.
25 “Kama hili sivyo, ni nani awezaye kunithibitisha kuwa mwongo, na kuyafanya maneno yangu kuwa si kitu?”
Que s’il n’en est pas ainsi, qui peut me convaincre d’avoir menti, et mettre devant Dieu mes paroles?