< Ayubu 24 >

1 “Kwa nini Mwenyezi asiweke nyakati kwa ajili ya hukumu? Kwa nini wale wamjuao wazitafute siku kama hizo bila mafanikio?
The times are not hidden from the Almighty; even those who know him, do not know his days.
2 Watu husogeza mawe ya mpaka; huchunga makundi ya wanyama waliyonyangʼanya kwa nguvu.
Some have crossed the boundaries, plundered the flocks, and given them pasture.
3 Huwanyangʼanya yatima punda wao, na kumchukua rehani fahali wa mjane.
They have driven away the donkey of orphans, and have taken the cow from the widow as collateral.
4 Humsukuma mhitaji kutoka njia, na kuwafanya maskini wote wa nchi kulazimika kujificha.
They have undermined the way of the poor, and have pressed together the meek of the earth.
5 Kama punda-mwitu jangwani, maskini huzunguka katika kazi zao za kutafuta chakula; mahali palipo jangwa huwapa chakula cha watoto wao.
Others, like wild asses in the desert, go forth to their work; by watching for prey, they obtain bread for their children.
6 Hukusanya chakula mashambani na kuokota masazo katika mashamba ya mizabibu ya waovu.
They reap a field that is not their own, and they harvest a vineyard that they have taken by force.
7 Kwa kukosa nguo, usiku kucha hukaa uchi; hawana chochote cha kujifunika baridi.
They send men away naked, having taken the clothing of those who have no covering in the cold;
8 Hutota kwa mvua za mlimani, nao huikumbatia miamba kwa ajili ya kukosa pa kujisitiri.
these are wet with the mountain rain, and, having no covering, they embrace the rocks.
9 Mtoto yatima hupokonywa matitini; mtoto wachanga wa maskini hunyakuliwa kwa ajili ya deni.
They have used violence to deprive orphans, and they have robbed the poor common people.
10 Kwa kukosa nguo, hutembea uchi; hubeba miganda ya ngano, lakini huwa na njaa.
From the naked and those who do not have enough clothing, and from the hungry, they have taken away sheaves of grain.
11 Hukamua zeituni katika mawe ya kusagia; hukanyaga mashinikizo, lakini wanaona kiu.
They take their midday rest among the stockpiles of those who, though they have trodden the winepresses, suffer thirst.
12 Kilio cha huzuni cha wanaokufa kinapaa kutoka mjini, nazo nafsi za waliojeruhiwa zinalilia msaada. Lakini Mungu hamlaumu mtu yeyote kwa kutenda mabaya.
In the cities, they caused the men to groan and the spirit of the wounded to cry out, and so God does not allow this to go unpunished.
13 “Wako wale wanaoiasi nuru, wasiofahamu njia zake wala hawakai katika mapito yake.
They have been rebellious against the light; they have not known his ways, nor have they returned by his paths.
14 Wakati mwanga wa mchana unapotoweka, muuaji huinuka naye huwaua maskini na mhitaji; wakati wa usiku hunyemelea kama mwizi.
The killer of men rises at first light; he executes the destitute and the poor, but, in truth, he is like a thief in the night.
15 Jicho la mzinzi hungojea wakati wa giza, naye hufikiri, ‘Hakuna jicho litakaloniona,’ naye huuficha uso wake.
The eye of the adulterer waits for darkness, saying, “No eye will see me,” and he covers his face.
16 Katika giza, huvunja majumba, lakini wakati wa mchana hujifungia ndani; hawataki kufanya lolote nuruni.
He passes through houses in the nighttime, just as they had agreed among themselves in the daytime; and they are ignorant of the light.
17 Kwa wote hawa, giza nene ndiyo asubuhi yao; hujifanya rafiki na vitisho vya gizani.
If sunrise should suddenly appear, it is treated by them like the shadow of death; and they walk in darkness, as if in light.
18 “Lakini wao ni povu juu ya maji; sehemu yao juu ya nchi imelaaniwa, hivyo hakuna hata mmoja aendaye kwenye shamba la mizabibu.
He is nimble on the surface of water. His place on land is to be accursed. May he not walk by way of the vineyards.
19 Kama vile joto na hari vinyakuavyo theluji iliyoyeyuka, ndivyo kuzimu kuwanyakuavyo waliotenda dhambi. (Sheol h7585)
May he cross from the snowy waters to excessive heat, and his sin, all the way to hell. (Sheol h7585)
20 Tumbo lililowazaa huwasahau, nao huwa karamu ya mabuu; watu waovu hawakumbukwi tena, lakini huvunjika kama mti.
Let mercy forget him. His charm is worms. Let him not be remembered, but instead be broken like an unfruitful tree.
21 Huwafanya mawindo wanawake tasa na wasio na watoto, nao hawaonyeshi huruma kwa wajane.
For he has fed on the barren, who does not bear fruit, and he has not done good to the widow.
22 Lakini Mungu huwakokota wenye nguvu kwa uwezo wake; ingawa wamestawi, hawana hakika ya maisha.
He has pulled down the strong by his strength, and, when he stands up, he will not have trust in his life.
23 Aweza akawaacha wakapumzika wakijihisi salama, lakini macho yake yanaona njia zao.
God has given him a place for repentance, and he abuses it with arrogance, but his eyes are upon his ways.
24 Kwa kitambo kidogo hutukuka, hatimaye hutoweka; hushushwa na kukusanywa kama wengine wote, hukatwa kama masuke ya nafaka.
They are lifted up for a little while, but they will not continue, and they will be brought low, just like all things, and they will be taken away, and, like the tops of the ears of grain, they will be crushed.
25 “Kama hili sivyo, ni nani awezaye kunithibitisha kuwa mwongo, na kuyafanya maneno yangu kuwa si kitu?”
But, if this is not so, who is able to prove to me that I have lied and to place my words before God?

< Ayubu 24 >