< Ayubu 23 >

1 Ndipo Ayubu akajibu:
約伯回答說:
2 “Hata leo malalamiko yangu ni chungu; mkono wake ni mzito juu yangu hata nikiugua.
直到今天,我還是痛苦的哀訴,他沉重的手掌,使我不得不呻吟。
3 Laiti ningefahamu mahali pa kumwona; laiti ningeweza kwenda mahali akaapo!
惟願我知道怎樣能尋到天主,能達到他的寶座前,
4 Ningeliweka shauri langu mbele zake, na kukijaza kinywa changu na hoja.
好將我的案情向他陳訴,因為我口中滿了證詞!
5 Ningejua kwamba angenijibu nini, na kuelewa lile ambalo angelisema.
唯願我知道他答覆我的話,明瞭他向我說什麼!
6 Je, angenipinga kwa nguvu nyingi? La, asingenigandamiza.
他豈能靠強力同我爭辯﹖決不,他必留神聽我。
7 Hapo mtu mwadilifu angeweka shauri lake mbele zake, nami ningeokolewa milele na mhukumu wangu.
如此,他會分辨出同他爭論的是個正直人,也許我可永久不再受裁判!
8 “Lakini nikienda mashariki, hayupo; nikienda magharibi, simpati.
可是我往東行,他不在那裏;我往西行,也找不到他;
9 Anapokuwa kazini pande za kaskazini, simwoni; akigeukia kusini, nako simwoni hata kidogo.
往北找,也看不見他;往南去,也見不到他。
10 Lakini anaijua njia niiendeayo; akiisha kunijaribu, nitatoka kama dhahabu.
他洞悉我所有的行動。他若試驗我,我必如純金出現。
11 Nyayo zangu zimefuata hatua zake kwa karibu; nimeishika njia yake bila kukengeuka.
我的腳緊隨著他的足跡,謹守他的道,總沒有偏離。
12 Sijaziacha amri zilizotoka midomoni mwake; nimeyathamini maneno ya kinywa chake kuliko chakula changu cha kila siku.
他所發的命令,我總沒有違背;他口中的訓言,我常保存在心中。
13 “Lakini yeye husimama peke yake; ni nani awezaye kumpinga? Yeye hufanya lolote atakalo.
但他所決定的,誰能變更﹖他所樂意的,必要實行。
14 Hutimiliza maagizo yake dhidi yangu, na bado anayo mipango mingi kama hiyo ambayo ameiweka akiba.
他為我注定的,必要完成;類似的事,還有很多。
15 Hiyo ndiyo sababu ninaingiwa na hofu mbele zake; nifikiriapo haya yote ninamwogopa.
因此,為了他,我很驚慌,一想起來就害怕。
16 Mungu ameufanya moyo wangu kuzimia; yeye Mwenyezi amenitia hofu.
天主使我的心沮喪,全能者使我恐怖。
17 Hata hivyo sijanyamazishwa na giza, wala kwa giza nene linalofunika uso wangu.
因為我雖面臨黑暗,幽暗雖遮蓋我的面,我仍不喪氣。

< Ayubu 23 >