< Ayubu 22 >

1 Ndipo Elifazi Mtemani akajibu:
是においてテマン人エリパズこたへて曰く
2 “Je, mwanadamu aweza kuwa wa faida kwa Mungu? Je, hata mtu mwenye hekima aweza kumfaidi?
人 神を益する事をえんや 智人も唯みづから益する而已なるぞかし
3 Je, Mwenyezi angefurahia nini kama ungekuwa mwadilifu? Au je, yeye angepata faida gani kama njia zako zingekuwa kamilifu?
なんぢ義かるとも全能者に何の歡喜かあらん なんぢ行爲を全たふするとも彼に何の利益かあらん
4 “Je, ni kwa ajili ya utaua wako ndiyo maana anakukemea na kuleta mashtaka dhidi yako?
彼汝の畏懼の故によりて汝を責め汝を鞫きたまはんや
5 Je, uovu wako si mkuu? Dhambi zako si hazina mwisho?
なんぢの惡大なるにあらずや 汝の罪はきはまり無し
6 Umedai dhamana kwa ndugu zako bila sababu; umewavua watu nguo zao, ukawaacha uchi.
即ち汝は故なくその兄弟の物を抑へて質となし 裸なる者の衣服を剥て取り
7 Hukumpa maji aliyechoka, nawe ulimnyima chakula mwenye njaa,
渇く者に水を與へて飮しめず 饑る者に食物を施こさず
8 ingawa ulikuwa mtu mwenye uwezo ukimiliki nchi: mtu uliyeheshimiwa, ukiishi ndani yake.
力ある者土地を得 貴き者その中に住む
9 Umewafukuza wajane mikono mitupu na kuzivunja nguvu za yatima.
なんぢは寡婦に手を空しうして去しむ 孤子の腕は折る
10 Ndiyo sababu mitego imekuzunguka pande zote, hatari ya ghafula inakutia hofu,
是をもて網羅なんぢを環り 畏懼にはかに汝を擾す
11 ndiyo sababu ni giza sana huwezi kuona, tena ndiyo sababu mafuriko ya maji yamekufunika.
なんぢ黒暗を見ずや 洪水のなんぢを覆ふを見ずや
12 “Je, Mungu hayuko katika mbingu za juu? Juu kuliko nyota zilizo juu sana!
神は天の高に在すならずや 星辰の巓ああ如何に高きぞや
13 Hivyo wewe wasema, ‘Mungu anajua nini?’ Je, yeye huhukumu katika giza kama hilo?
是によりて汝は言ふ 神なにをか知しめさん 豈よく黒雲の中より審判するを得たまはんや
14 Mawingu mazito ni pazia lake, hivyo hatuoni sisi atembeapo juu ya anga la dunia.
濃雲かれを蔽へば彼は見たまふ所なし 唯天の蒼穹を歩みたまふ
15 Je, utaifuata njia ya zamani, ambayo watu waovu waliikanyaga?
なんぢ古昔の世の道を行なはんとするや 是あしき人の踐たりし者ならずや
16 Waliondolewa kabla ya wakati wao, misingi yao ikachukuliwa na mafuriko.
彼等は時いまだ至らざるに打絶れ その根基は大水に押流されたり
17 Walimwambia Mungu, ‘Tuache sisi! Huyo Mwenyezi aweza kutufanyia nini?’
彼ら神に言けらく我儕を離れたまへ 全能者われらのために何を爲ことを得んと
18 Lakini ndiye alizijaza nyumba zao na vitu vizuri, hivyo ninajitenga mbali na mashauri ya waovu.
しかるに彼は却つて佳物を彼らの家に盈したまへり 但し惡人の計畫は我に與する所にあらず
19 “Wenye haki wanaona maangamizi yao na kufurahi, nao wasio na hatia huwadhihaki, wakisema,
義しき者は之を見て喜び 無辜者は彼らを笑ふ
20 ‘Hakika adui zetu wameangamizwa, nao moto umeteketeza mali zao.’
曰く我らの仇は誠に滅ぼされ 其盈餘れる物は火にて焚つくさる
21 “Mjue sana Mungu ili uwe na amani, ndipo mema yatakapokujia.
請ふ汝神と和らぎて平安を得よ 然らば福祿なんぢに來らん
22 Uyapokee mafundisho toka kinywani mwake, na maneno yake uyaweke moyoni mwako.
請ふかれの口より教晦を受け その言語をなんぢの心に藏めよ
23 Kama ukimrudia Mwenyezi, utarudishwa upya: Kama ukiuondoa uovu uwe mbali na hema lako,
なんぢもし全能者に歸向り且なんぢの家より惡を除き去ば汝の身再び興されん
24 kama dhahabu yako ukiihesabu kama mavumbi, dhahabu yako ya Ofiri kama miamba ya mabondeni,
なんぢの寳を土の上に置き オフルの黄金を谿河の石の中に置け
25 ndipo Mwenyezi atakuwa dhahabu yako, naye atakuwa fedha yako iliyo bora.
然れば全能者なんぢの寳となり汝のために白銀となりたまふべし
26 Hakika ndipo utakapojifurahisha kwa Mwenyezi, nawe utamwinulia Mungu uso wako.
而してなんぢは又全能者を喜び且神にむかひて面をあげん
27 Utamwomba yeye, naye atakusikia, nawe utazitimiza nadhiri zako.
なんぢ彼に祈らば彼なんぢに聽きたまはん 而して汝その誓願をつくのひ果さん
28 Utakusudia jambo nalo litatendeka, nao mwanga utaangazia njia zako.
なんぢ事を爲んと定めなばその事なんぢに成ん 汝の道には光照ん
29 Watu watakaposhushwa, nawe ukasema, ‘Wainue!’ ndipo atamwokoa aliyevunjika moyo.
其卑く降る時は汝いふ昇る哉と 彼は謙遜者を拯ひたまふべし
30 Atamwokoa hata yule ambaye ana hatia, ataokolewa kwa sababu ya usafi wa mikono yako.”
かれは罪なきに非ざる者をも拯ひたまはん 汝の手の潔淨によりて斯る者も拯はるべし

< Ayubu 22 >