< Ayubu 22 >

1 Ndipo Elifazi Mtemani akajibu:
ויען אליפז התמני ויאמר׃
2 “Je, mwanadamu aweza kuwa wa faida kwa Mungu? Je, hata mtu mwenye hekima aweza kumfaidi?
הלאל יסכן גבר כי יסכן עלימו משכיל׃
3 Je, Mwenyezi angefurahia nini kama ungekuwa mwadilifu? Au je, yeye angepata faida gani kama njia zako zingekuwa kamilifu?
החפץ לשדי כי תצדק ואם בצע כי תתם דרכיך׃
4 “Je, ni kwa ajili ya utaua wako ndiyo maana anakukemea na kuleta mashtaka dhidi yako?
המיראתך יכיחך יבוא עמך במשפט׃
5 Je, uovu wako si mkuu? Dhambi zako si hazina mwisho?
הלא רעתך רבה ואין קץ לעונתיך׃
6 Umedai dhamana kwa ndugu zako bila sababu; umewavua watu nguo zao, ukawaacha uchi.
כי תחבל אחיך חנם ובגדי ערומים תפשיט׃
7 Hukumpa maji aliyechoka, nawe ulimnyima chakula mwenye njaa,
לא מים עיף תשקה ומרעב תמנע לחם׃
8 ingawa ulikuwa mtu mwenye uwezo ukimiliki nchi: mtu uliyeheshimiwa, ukiishi ndani yake.
ואיש זרוע לו הארץ ונשוא פנים ישב בה׃
9 Umewafukuza wajane mikono mitupu na kuzivunja nguvu za yatima.
אלמנות שלחת ריקם וזרעות יתמים ידכא׃
10 Ndiyo sababu mitego imekuzunguka pande zote, hatari ya ghafula inakutia hofu,
על כן סביבותיך פחים ויבהלך פחד פתאם׃
11 ndiyo sababu ni giza sana huwezi kuona, tena ndiyo sababu mafuriko ya maji yamekufunika.
או חשך לא תראה ושפעת מים תכסך׃
12 “Je, Mungu hayuko katika mbingu za juu? Juu kuliko nyota zilizo juu sana!
הלא אלוה גבה שמים וראה ראש כוכבים כי רמו׃
13 Hivyo wewe wasema, ‘Mungu anajua nini?’ Je, yeye huhukumu katika giza kama hilo?
ואמרת מה ידע אל הבעד ערפל ישפוט׃
14 Mawingu mazito ni pazia lake, hivyo hatuoni sisi atembeapo juu ya anga la dunia.
עבים סתר לו ולא יראה וחוג שמים יתהלך׃
15 Je, utaifuata njia ya zamani, ambayo watu waovu waliikanyaga?
הארח עולם תשמר אשר דרכו מתי און׃
16 Waliondolewa kabla ya wakati wao, misingi yao ikachukuliwa na mafuriko.
אשר קמטו ולא עת נהר יוצק יסודם׃
17 Walimwambia Mungu, ‘Tuache sisi! Huyo Mwenyezi aweza kutufanyia nini?’
האמרים לאל סור ממנו ומה יפעל שדי למו׃
18 Lakini ndiye alizijaza nyumba zao na vitu vizuri, hivyo ninajitenga mbali na mashauri ya waovu.
והוא מלא בתיהם טוב ועצת רשעים רחקה מני׃
19 “Wenye haki wanaona maangamizi yao na kufurahi, nao wasio na hatia huwadhihaki, wakisema,
יראו צדיקים וישמחו ונקי ילעג למו׃
20 ‘Hakika adui zetu wameangamizwa, nao moto umeteketeza mali zao.’
אם לא נכחד קימנו ויתרם אכלה אש׃
21 “Mjue sana Mungu ili uwe na amani, ndipo mema yatakapokujia.
הסכן נא עמו ושלם בהם תבואתך טובה׃
22 Uyapokee mafundisho toka kinywani mwake, na maneno yake uyaweke moyoni mwako.
קח נא מפיו תורה ושים אמריו בלבבך׃
23 Kama ukimrudia Mwenyezi, utarudishwa upya: Kama ukiuondoa uovu uwe mbali na hema lako,
אם תשוב עד שדי תבנה תרחיק עולה מאהלך׃
24 kama dhahabu yako ukiihesabu kama mavumbi, dhahabu yako ya Ofiri kama miamba ya mabondeni,
ושית על עפר בצר ובצור נחלים אופיר׃
25 ndipo Mwenyezi atakuwa dhahabu yako, naye atakuwa fedha yako iliyo bora.
והיה שדי בצריך וכסף תועפות לך׃
26 Hakika ndipo utakapojifurahisha kwa Mwenyezi, nawe utamwinulia Mungu uso wako.
כי אז על שדי תתענג ותשא אל אלוה פניך׃
27 Utamwomba yeye, naye atakusikia, nawe utazitimiza nadhiri zako.
תעתיר אליו וישמעך ונדריך תשלם׃
28 Utakusudia jambo nalo litatendeka, nao mwanga utaangazia njia zako.
ותגזר אומר ויקם לך ועל דרכיך נגה אור׃
29 Watu watakaposhushwa, nawe ukasema, ‘Wainue!’ ndipo atamwokoa aliyevunjika moyo.
כי השפילו ותאמר גוה ושח עינים יושע׃
30 Atamwokoa hata yule ambaye ana hatia, ataokolewa kwa sababu ya usafi wa mikono yako.”
ימלט אי נקי ונמלט בבר כפיך׃

< Ayubu 22 >