< Ayubu 21 >
2 “Yasikilizeni maneno yangu kwa makini; hii na iwe faraja mnayonipa mimi.
너희는 내 말을 자세히 들으라 이것이 너희의 위로가 될 것이니라
3 Nivumilieni ninapozungumza, nami nikishazungumza, endeleeni kunidhihaki.
나를 용납하여 말하게 하라 내가 말한 후에 또 조롱할지니라
4 “Je, kwani malalamiko yangu yanaelekezwa kwa mwanadamu? Kwa nini nisikose subira?
나의 원망이 사람을 향하여 하는 것이냐 내가 어찌 초급하지 아니하겠느냐
5 Niangalieni mkastaajabu; mkaweke mkono juu ya vinywa vyenu.
너희는 나를 보아라, 놀라라, 손으로 입을 가리우라
6 Ninapowaza juu ya hili, ninaogopa, nao mwili wangu unatetemeka.
내가 추억하기만 하여도 답답하고 두려움이 내 몸을 잡는구나
7 Kwa nini waovu wanaendelea kuishi, wakifikia umri wa uzee na kuendelea kuwa na nguvu?
어찌하여 악인이 살고 수를 누리고 세력이 강하냐
8 Huwaona watoto wao wakithibitika wakiwa wamewazunguka, wazao wao mbele za macho yao.
씨가 그들의 앞에서 그들과 함께 굳게 서고 자손이 그들의 목전에서 그러하구나
9 Nyumba zao zi salama wala hakuna hofu; fimbo ya Mungu haiko juu yao.
그 집이 평안하여 두려움이 없고 하나님의 매가 그 위에 임하지 아니하며
10 Madume yao ya ngʼombe huvyaza bila kushindwa kamwe; ngʼombe wao huzaa wala hawaharibu mimba.
그 수소는 영락없이 새끼를 배게 하고 그 암소는 새끼를 낳고 낙태하지 않는구나
11 Huwatoa watoto wao nje kama kundi; wadogo wao huchezacheza.
그들은 아이들을 내어보냄이 양떼 같고 그 자녀들은 춤추는구나
12 Huimba nyimbo kwa matari na kwa kinubi, nao huifurahia sauti ya filimbi.
그들이 소고와 수금으로 노래하고 피리 불어 즐기며
13 Huitumia miaka yao katika mafanikio nao hushuka kaburini kwa amani. (Sheol )
그 날을 형통하게 지내다가 경각간에 음부에 내려가느니라 (Sheol )
14 Lakini humwambia Mungu, ‘Tuache sisi!’ Hatuna haja ya kufahamu njia zako.
그러할지라도 그들은 하나님께 말하기를 우리를 떠나소서 우리가 주의 도리 알기를 즐겨하지 아니하나이다
15 Mwenyezi ni nani hata tumtumikie? Tutapata faida gani kumwomba?
전능자가 누구기에 우리가 섬기며 우리가 그에게 기도한들 무슨 이익을 얻으랴 하는구나
16 Lakini kufanikiwa kwao hakupo mikononi mwao wenyewe, hivyo najitenga mbali na shauri la waovu.
그들의 복록이 그들의 손으로 말미암은 것이 아니니라 악인의 계획은 나와 판이하니라
17 “Lakini ni mara ngapi taa ya waovu huzimwa? Ni mara ngapi maafa huwajia, yale yawapatayo ambayo Mungu huwapangia katika hasira yake?
악인의 등불이 꺼짐이나 재앙이 그들에게 임함이나 하나님이 진노하사 그들을 곤고케 하심이나
18 Ni mara ngapi huwa kama majani makavu mbele ya upepo, kama makapi yachukuliwayo na dhoruba?
그들이 바람 앞에 검불 같이, 폭풍에 불려가는 겨 같이 되는 일이 몇 번이나 있었느냐
19 Imesemekana, ‘Mungu huiweka akiba adhabu ya mtu kwa ajili ya wanawe.’ Mungu na amlipe mtu mwenyewe, ili apate kulijua!
하나님이 그의 죄악을 쌓아 두셨다가 그 자손에게 갚으신다 하거니와 그 몸에 갚으셔서 그로 깨닫게 하셔야 할 것이라
20 Macho yake mwenyewe na yaone maangamizi yake; yeye na ainywe ghadhabu ya Mwenyezi.
자기의 멸망을 자기의 눈으로 보게 하시며 전능자의 진노를 마시게 하셔야 할 것이니라
21 Kwani anajali nini kuhusu jamaa anayoiacha nyuma, miezi yake aliyopangiwa ifikapo mwisho?
그의 달 수가 진하면 자기 집에 대하여 무슨 관계가 있겠느냐
22 “Je, yuko mtu yeyote awezaye kumfundisha Mungu maarifa, iwapo yeye ndiye ahukumuye hata walio juu ya wote?
그러나 하나님은 높은 자들을 심판하시나니 누가 능히 하나님께 지식을 가르치겠느냐
23 Mtu mmoja hufa akiwa na nguvu zake kamili, akiwa salama na mwenye raha kamili,
어떤 사람은 죽도록 기운이 충실하여 평강하며 안일하고
24 mwili wake ukiwa umenawiri, nayo mifupa yake ikiwa imejaa mafuta ndani yake.
그 그릇에는 젖이 가득하며 그 골수는 윤택하였고
25 Mtu mwingine hufa katika uchungu wa nafsi, akiwa hajafurahia kamwe jambo lolote zuri.
어떤 사람은 죽도록 마음에 고통하고 복을 맛보지 못하였어도
26 Hao wote hulala mavumbini, nao mabuu huwafunika wote.
이 둘이 일반으로 흙 속에 눕고 그 위에 구더기가 덮이는구나
27 “Ninayajua kikamilifu yale mnayoyafikiri, mipango ambayo kwayo mngenitendea mabaya.
내가 너희의 생각을 알고 너희가 나를 해하려는 궤휼도 아노라
28 Mwasema, ‘Iko wapi sasa nyumba ya huyo mtu mkuu, mahema ambayo watu waovu walikaa?’
너희의 말이 왕후의 집이 어디 있으며 악인의 거하던 장막이 어디 있느뇨 하는구나
29 Je, hamkuwahi kuwauliza hao wanaosafiri? Je, hamkutafakari taarifa zao:
너희가 길 가는 사람들에게 묻지 아니하였느냐 그들의 증거를 알지 못하느냐
30 kwamba mtu mwovu huepushwa kutoka siku ya maafa, kwamba huokolewa kutoka siku ya ghadhabu?
악인은 남기워서 멸망의 날을 기다리움이 되고 멸망의 날을 맞으러 끌려 나감이 된다 하느니라
31 Ni nani hulaumu matendo yake mbele ya uso wake? Ni nani ampatilizaye kwa yale aliyoyatenda?
누가 능히 그의 행위를 면박하며 누가 능히 그의 소위를 보응하랴마는
32 Hupelekwa kaburini, nao ulinzi ukawekwa kwenye kaburi lake.
그를 무덤으로 메어 가고 사람이 그 무덤을 지키리라
33 Udongo ulio bondeni ni mtamu kwake; watu wote watamfuata, nao umati wa watu usiohesabika umemtangulia.
그는 골짜기의 흙덩이를 달게 여기고 그 앞선 자가 무수함 같이 모든 사람이 그 뒤를 좇으리라
34 “Hivyo ninyi mnawezaje kunifariji kwa upuzi wenu? Hakuna kilichosalia cha majibu yenu isipokuwa uongo!”
이러한즉 너희의 위로가 헛되지 아니하냐 너희의 대답은 거짓뿐이니라