< Ayubu 19 >

1 Ndipo Ayubu akajibu:
آنگاه ایوب پاسخ داد:
2 “Je, mtaendelea kunitesa mpaka lini, na kuniponda kwa maneno yenu?
تا به کی می‌خواهید عذابم بدهید و با سخنانتان مرا خرد کنید؟
3 Mara kumi hizi mmenishutumu; bila aibu mnanishambulia.
پی‌درپی به من اهانت می‌کنید و از این رفتارتان شرم نمی‌کنید.
4 Kama ni kweli nimepotoka, kosa langu ninabaki kuhusika nalo mwenyewe.
اگر من خطا کرده‌ام، خطای من چه صدمه‌ای به شما زده است؟
5 Kama kweli mngejitukuza wenyewe juu yangu, na kutumia unyonge wangu dhidi yangu,
شما خود را بهتر از من می‌پندارید و این مصیبت مرا نتیجهٔ گناه من می‌دانید،
6 basi jueni kuwa Mungu amenitendea yaliyo mabaya, naye amekokota wavu wake kunizunguka.
در حالی که این خداست که مرا به چنین روزی انداخته و در دام خود گرفتار کرده است.
7 “Ingawa ninalia, ‘Nimetendewa mabaya!’ sipati jibu; ingawa ninaomba msaada, hakuna haki.
فریاد برمی‌آورم و کمک می‌خواهم، اما هیچ‌کس صدایم را نمی‌شنود و کسی به فریادم نمی‌رسد.
8 Yeye ameizuia njia yangu hivyo siwezi kupita; ameyafunika mapito yangu na giza.
خدا راهم را سد کرده و روشنایی مرا به تاریکی مبدل نموده است.
9 Amenivua heshima yangu, na kuniondolea taji kichwani pangu.
او عزت و فخر را از من گرفته
10 Amenibomoa kila upande hadi nimeisha; amelingʼoa tegemeo langu kama mti.
و از هر طرف مرا خرد کرده است. او مرا از پا درآورده و درخت امیدم را از ریشه برکنده است.
11 Hasira yake imewaka juu yangu; amenihesabu kuwa miongoni mwa adui zake.
خشم او علیه من شعله‌ور است و او مرا دشمن خود به حساب می‌آورد.
12 Majeshi yake yananisogelea kwa nguvu; yamenizingira, yamepiga kambi kulizunguka hema langu.
لشکریانش به پیش می‌تازد و بر ضد من سنگر می‌سازند، و گرداگردِ خیمه‌ام اردو می‌زنند.
13 “Amewatenga ndugu zangu mbali nami; wale tunaojuana nao wamefarakana nami kabisa.
برادرانم را از من دور کرده است، و آشنایانم بر ضد من برخاسته‌اند.
14 Watu wa jamaa yangu wamekwenda mbali; rafiki zangu wamenisahau.
بستگانم از من روگردانیده و همهٔ دوستانم مرا ترک گفته‌اند.
15 Wageni wangu na watumishi wangu wa kike wananiona kama mgeni; wananitazama kama mgeni.
اهل خانه و حتی خدمتکارانم با من مانند یک غریبه رفتار می‌کنند و من برای آنها بیگانه شده‌ام.
16 Namwita mtumishi wangu, wala haitiki, ingawa namwomba kwa kinywa changu mwenyewe.
خدمتکارم را صدا می‌کنم، حتی به او التماس می‌نمایم، ولی او جوابم را نمی‌دهد.
17 Pumzi ya kinywa changu ni kinyaa kwa mke wangu; nimekuwa chukizo mno kwa ndugu zangu mwenyewe.
نَفَسم برای زنم مشمئزکننده است، و برادرانم طاقت تحمل مرا ندارند.
18 Hata watoto wadogo hunidhihaki; ninapojitokeza, hunifanyia mzaha.
بچه‌های کوچک هم مرا خوار می‌شمارند و وقتی مرا می‌بینند مسخره‌ام می‌کنند.
19 Rafiki zangu wa moyoni wote wananichukia kabisa; wale niwapendao wamekuwa kinyume nami.
حتی نزدیکترین دوستانم از من منزجرند و آنانی که دوستشان می‌داشتم از من روگردان شده‌اند.
20 Mimi nimebaki mifupa na ngozi tu; nimeponea nikiwa karibu kufa.
از من پوست و استخوانی بیش نمانده است، به زحمت از چنگ مرگ گریخته‌ام.
21 “Nihurumieni, rafiki zangu, kuweni na huruma, kwa kuwa mkono wa Mungu umenipiga.
آه ای دوستان، به من رحم کنید، زیرا دست خدا بر من سنگین شده است.
22 Kwa nini mnanifuatia kama Mungu afanyavyo? Hamtosheki kamwe na mwili wangu?
چرا شما هم مثل خدا مرا عذاب می‌دهید؟ آیا از خوردن گوشت بدنم سیر نشده‌اید؟
23 “Laiti maneno yangu yangewekwa kwenye kumbukumbu, laiti kwamba yangeandikwa kwenye kitabu,
ای کاش می‌توانستم درد دلم را با قلمی آهنین برای همیشه در دل سنگ بنویسم.
24 kwamba yangechorwa kwenye risasi kwa kifaa cha chuma, au kuyachonga juu ya mwamba milele!
25 Ninajua kwamba Mkombozi wangu yu hai, naye kwamba mwishoni atasimama juu ya nchi.
اما من می‌دانم که رهاننده‌ام زنده است و سرانجام بر زمین خواهد ایستاد؛
26 Nami baada ya ngozi yangu kuharibiwa, bado nikiwa na mwili huu nitamwona Mungu;
و می‌دانم حتی بعد از اینکه بدن من هم بپوسد، خدا را خواهم دید!
27 mimi nitamwona kwa macho yangu mwenyewe: mimi, wala si mwingine. Tazama jinsi moyo wangu unavyomtamani sana!
من خود با این چشمانم او را خواهم دید! چه امید پرشکوهی!
28 “Kama mkisema, ‘Tazama tutakavyomwinda, maadamu mzizi wa tatizo uko ndani yake,’
چطور جرات می‌کنید به آزار من ادامه دهید و بگویید: «مقصر خودش است»؟
29 ninyi wenyewe uogopeni upanga, kwa kuwa ghadhabu italeta adhabu kwa upanga, nanyi ndipo mtakapojua kwamba kuna hukumu.”
از شمشیر مجازات خدا بترسید و بدانید که او شما را داوری خواهد کرد.

< Ayubu 19 >