< Ayubu 19 >

1 Ndipo Ayubu akajibu:
ויען איוב ויאמר׃
2 “Je, mtaendelea kunitesa mpaka lini, na kuniponda kwa maneno yenu?
עד אנה תוגיון נפשי ותדכאונני במלים׃
3 Mara kumi hizi mmenishutumu; bila aibu mnanishambulia.
זה עשר פעמים תכלימוני לא תבשו תהכרו לי׃
4 Kama ni kweli nimepotoka, kosa langu ninabaki kuhusika nalo mwenyewe.
ואף אמנם שגיתי אתי תלין משוגתי׃
5 Kama kweli mngejitukuza wenyewe juu yangu, na kutumia unyonge wangu dhidi yangu,
אם אמנם עלי תגדילו ותוכיחו עלי חרפתי׃
6 basi jueni kuwa Mungu amenitendea yaliyo mabaya, naye amekokota wavu wake kunizunguka.
דעו אפו כי אלוה עותני ומצודו עלי הקיף׃
7 “Ingawa ninalia, ‘Nimetendewa mabaya!’ sipati jibu; ingawa ninaomba msaada, hakuna haki.
הן אצעק חמס ולא אענה אשוע ואין משפט׃
8 Yeye ameizuia njia yangu hivyo siwezi kupita; ameyafunika mapito yangu na giza.
ארחי גדר ולא אעבור ועל נתיבותי חשך ישים׃
9 Amenivua heshima yangu, na kuniondolea taji kichwani pangu.
כבודי מעלי הפשיט ויסר עטרת ראשי׃
10 Amenibomoa kila upande hadi nimeisha; amelingʼoa tegemeo langu kama mti.
יתצני סביב ואלך ויסע כעץ תקותי׃
11 Hasira yake imewaka juu yangu; amenihesabu kuwa miongoni mwa adui zake.
ויחר עלי אפו ויחשבני לו כצריו׃
12 Majeshi yake yananisogelea kwa nguvu; yamenizingira, yamepiga kambi kulizunguka hema langu.
יחד יבאו גדודיו ויסלו עלי דרכם ויחנו סביב לאהלי׃
13 “Amewatenga ndugu zangu mbali nami; wale tunaojuana nao wamefarakana nami kabisa.
אחי מעלי הרחיק וידעי אך זרו ממני׃
14 Watu wa jamaa yangu wamekwenda mbali; rafiki zangu wamenisahau.
חדלו קרובי ומידעי שכחוני׃
15 Wageni wangu na watumishi wangu wa kike wananiona kama mgeni; wananitazama kama mgeni.
גרי ביתי ואמהתי לזר תחשבני נכרי הייתי בעיניהם׃
16 Namwita mtumishi wangu, wala haitiki, ingawa namwomba kwa kinywa changu mwenyewe.
לעבדי קראתי ולא יענה במו פי אתחנן לו׃
17 Pumzi ya kinywa changu ni kinyaa kwa mke wangu; nimekuwa chukizo mno kwa ndugu zangu mwenyewe.
רוחי זרה לאשתי וחנתי לבני בטני׃
18 Hata watoto wadogo hunidhihaki; ninapojitokeza, hunifanyia mzaha.
גם עוילים מאסו בי אקומה וידברו בי׃
19 Rafiki zangu wa moyoni wote wananichukia kabisa; wale niwapendao wamekuwa kinyume nami.
תעבוני כל מתי סודי וזה אהבתי נהפכו בי׃
20 Mimi nimebaki mifupa na ngozi tu; nimeponea nikiwa karibu kufa.
בעורי ובבשרי דבקה עצמי ואתמלטה בעור שני׃
21 “Nihurumieni, rafiki zangu, kuweni na huruma, kwa kuwa mkono wa Mungu umenipiga.
חנני חנני אתם רעי כי יד אלוה נגעה בי׃
22 Kwa nini mnanifuatia kama Mungu afanyavyo? Hamtosheki kamwe na mwili wangu?
למה תרדפני כמו אל ומבשרי לא תשבעו׃
23 “Laiti maneno yangu yangewekwa kwenye kumbukumbu, laiti kwamba yangeandikwa kwenye kitabu,
מי יתן אפו ויכתבון מלי מי יתן בספר ויחקו׃
24 kwamba yangechorwa kwenye risasi kwa kifaa cha chuma, au kuyachonga juu ya mwamba milele!
בעט ברזל ועפרת לעד בצור יחצבון׃
25 Ninajua kwamba Mkombozi wangu yu hai, naye kwamba mwishoni atasimama juu ya nchi.
ואני ידעתי גאלי חי ואחרון על עפר יקום׃
26 Nami baada ya ngozi yangu kuharibiwa, bado nikiwa na mwili huu nitamwona Mungu;
ואחר עורי נקפו זאת ומבשרי אחזה אלוה׃
27 mimi nitamwona kwa macho yangu mwenyewe: mimi, wala si mwingine. Tazama jinsi moyo wangu unavyomtamani sana!
אשר אני אחזה לי ועיני ראו ולא זר כלו כליתי בחקי׃
28 “Kama mkisema, ‘Tazama tutakavyomwinda, maadamu mzizi wa tatizo uko ndani yake,’
כי תאמרו מה נרדף לו ושרש דבר נמצא בי׃
29 ninyi wenyewe uogopeni upanga, kwa kuwa ghadhabu italeta adhabu kwa upanga, nanyi ndipo mtakapojua kwamba kuna hukumu.”
גורו לכם מפני חרב כי חמה עונות חרב למען תדעון שדין׃

< Ayubu 19 >